Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Pazia la Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) kwa msimu wa 2018/2019 linatarajiwa kufungwa leo Mei 28, 2019 kwa timu zote 20 kupepetana kunako Viwanja tofauti nchini Tanzania
Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni ambao tayari ametangazwa kuwa Bingwa wa TPL, kwa mara ya pili mfululizo kwa msimu wa 2018/2019, itakuwa ugenini kukipiga na WakataMiwa, Mtibwa Sugar kuanzia saa 9:00 Alasiri kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Mechi ya Mtibwa Sugar, dhidi ya Simba SC, itakuwa sambamba na sherehe za kukabidhiwa kombe la Ligi Kuu Tanzania TPL, huku vita vikiwa kwenye michezo hii ni zile zilizo kwenye nafasi za mwisho katika msimamo wa TPL, Nani kushuka daraja kuungana na Klabu ya African Lyon? Na nani kubakia..?
Tujuzane hapa JF kwa kila ambaye yuko uwanjani katika pembe zote za Tanzania ama yupo karibu na Tv, Kumbuka mechi zitaanza saa 10:00 jioni na mechi Tano kuwa Mubashara Azam Tv.
Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni ambao tayari ametangazwa kuwa Bingwa wa TPL, kwa mara ya pili mfululizo kwa msimu wa 2018/2019, itakuwa ugenini kukipiga na WakataMiwa, Mtibwa Sugar kuanzia saa 9:00 Alasiri kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Mechi ya Mtibwa Sugar, dhidi ya Simba SC, itakuwa sambamba na sherehe za kukabidhiwa kombe la Ligi Kuu Tanzania TPL, huku vita vikiwa kwenye michezo hii ni zile zilizo kwenye nafasi za mwisho katika msimamo wa TPL, Nani kushuka daraja kuungana na Klabu ya African Lyon? Na nani kubakia..?
Tujuzane hapa JF kwa kila ambaye yuko uwanjani katika pembe zote za Tanzania ama yupo karibu na Tv, Kumbuka mechi zitaanza saa 10:00 jioni na mechi Tano kuwa Mubashara Azam Tv.