DOKEZO PCCB wilayani Bunda mfuatilieni kijana huyu anayekagua leseni za biashara

DOKEZO PCCB wilayani Bunda mfuatilieni kijana huyu anayekagua leseni za biashara

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mjukuu wa kigogo

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2023
Posts
445
Reaction score
1,094
Hii ikufikie Boss wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (PCCB) wilaya ya Bunda mkoani Mara. Wiki hii Kuna kijana mmoja ambaye kaanzisha operation ya kupita kwa baadhi ya maduka ya wafanyabiashara na kuwaulizia kama tayari washalipa leseni za biashara au la. Inajulikana wazi wafanyabiashara wote iwe hapa Tanzania au mahali pengine duniani wana wajibu wa kulipa kodi Kwa ajili ya maendeleo ya Taifa lao.

Kijana huyu ambaye hujitambulisha kama afisa maendeleo ya jamii kata ya Bunda mjini anafanya ukaguzi pasipokuwa na kitambulisho kinachomtambulisha ofisi anayotoka na anapoulizwa na wafanyabiashara kwamba watamtambuaje kwamba yeye ni afisa maendeleo ya jamii bila kuwa na kitambulisho,anaanza kutishia na kuibua visababu vya kutishia ambayo ni kama kutoa alert kwamba watakuja kutengenezewa mizengwe ili wakione cha moto siku za baadae na kufunga biashara zao.

Lililoko nyuma ya pazia inaonekana huyu jamaa anatumiwa na baadhi ya watendaji wa kata wasio waaminifu katika kutengeneza mazingira ya rushwa kwa wafanyabiashara. Na inawezekana kabisa watu wakaanza kuundiwa mizengwe ili wafunge biashara zao. Mamlaka imfuatilie kwa kina sababu ya yeye kufanya ukaguzi pasipo kitambulisho huku akitoa vitisho anapoombwa kuonyesha kwa wafanyabiashara. Anaficha kwa sababu zipi? Na pia bado wananchi hatujaelezwa kama maafisa maendeleo ya jamii ndio wanahusika kukagua leseni za biashara.

Na kama wao ndio wahusika iweje mhusika atembee na kufanya ukaguzi bila kuwa na kitambulisho au walau kuambatana na baadhi viongozi ya viongozi wa serikali walau hata balozi, nk. Watu kama hawa wakishirikiana na watendaji wasio waaminifu wapo nchi nzima na wanasababisha wafanyabiashara wengi kufunga biashara zao na mwisho wa siku vita dhidi ya umaskini inakuwa ngumu!

NB: Inadaiwa jina la huyo mhusika ni Mapunda.
 
Ebu ngoja kwanza....
Hivi kweli nyie wote mmeshindwa kukamata hiyo kenge na kuipeleka police kwa utapeli...🤔🤔
 
Wewe umeweza kupata jina lake hadi namba yake kisha unadai hana utambulisho?
Lipa kodi bila shuruti, huko kukwepa kodi ndo kutengeneza mazingira ya rushwa.

Ukifungiwa kibanda chako kwa kutolipa kodi nani mizengwe hapo?
 
Wewe umeweza kupata jina lake hadi namba yake kisha unadai hana utambulisho?
Lipa kodi bila shuruti, huko kukwepa kodi ndo kutengeneza mazingira ya rushwa.

Ukifungiwa kibanda chako kwa kutolipa kodi nani mizengwe hapo?
Afisa Maendeleo ya Jamii anahusika na suala la kukusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara?
 
Afisa Maendeleo ya Jamii anahusika na suala la kukusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara?
Kwenye hili dokezo hakuna popote ameshutumiwa kukusanya kodi, imesemekana amekuwa akipita kuulizia kama wamelipa kodi au laah.

Hii ni kawaida kwa Halmashari nyingi kutumia mtumishi yeyote kwenye operesheni kama hizi, muhimu hachukui pesa yako anaulizia kama bado anahamasisha ukalipe kodi yako sehemu sahihi.

Hizi ni shutuma uchwara, TULIPE KODI KWA WAKATI.... PAMOJA TUIJENGE NCHI YETU.
 
Mtoa Mada unayo Leseni ya Biashara?

Binafsi sijawahi ona Afisa maendeleo akihusika na ukaguzi wa Leseni za Biashara (hata kumwona Afisa maendeleo, sijawahi) lakini kama mfanya Biashara umekidhi Vigezo vyote unapata ugumu gani kuonesha Docs zako, Kisha Mtu aondoke zake?

Leseni hata Mteja anaweza kudai ili kujiridhisha kwamba anafanya Biashara na Mtu anayetambulika na Mamlaka.
 
Afisa Maendeleo ya Jamii anahusika na suala la kukusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara?
TRA huwa wanashirikiana na ofisi za kata mkuu,

Kuna kipindi mtendaji wa kata alitoa ajira kwa vijana wazunguke mtaa mzima na FOMU za TRA kuandikisha nyumba zote za kupangisha, idadi ya vyumba, mmiliki na kodi itolewayo na wapangaji kila mwezi.

Na hao waliopewa hiyo kazi ni watu wa mtaani nq baadhi ya stafs wa ofisi ya kata.

Ajira zote mdogondogo huwa wanapeana wao kwa wao na ukileta ujuaji utajikuta upo polisi. Wana connection kila mahali hadi halmashauri
 
Tatizo ni yeye kukataa kutoa kitambulisho shida IPO wapi
Wewe umeweza kupata jina lake hadi namba yake kisha unadai hana utambulisho?
Lipa kodi bila shuruti, huko kukwepa kodi ndo kutengeneza mazingira ya rushwa.

Ukifungiwa kibanda chako kwa kutolipa kodi nani mizengwe hapo?
 
Mtoa Mada unayo Leseni ya Biashara?

Binafsi sijawahi ona Afisa maendeleo akihusika na ukaguzi wa Leseni za Biashara (hata kumwona Afisa maendeleo, sijawahi) lakini kama mfanya Biashara umekidhi Vigezo vyote unapata ugumu gani kuonesha Docs zako, Kisha Mtu aondoke zake?

Leseni hata Mteja anaweza kudai ili kujiridhisha kwamba anafanya Biashara na Mtu anayetambulika na Mamlaka.
Afisa bila Id?
 
What is the issue, mchukulie tu kwamba ni kiherehere Moja hivi anasumbua, Kisha mwoneshe hiyo Leseni aliyoulizia aondoke zake..
Siyo utaratibu sasa Kwa hiyo akipita pia mpita njia unaonyesha
 
Back
Top Bottom