PDF la oil chafu hili hapa

PDF la oil chafu hili hapa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kutokana na ongezeko kubwa la viwanda Tanganyika, mahitaji ya malighafi nayo yameongezeka kwa kiasi kikubwa sana. Kuna baadhi ya malighafi ambazo zamani hazikuwa na thamani yoyote. Ni aidha ziligawiwa bure, zilitupwa, au ziliuzwa kwa bei rahisi.

Leo twende na hii malighafi ya oil iliyotumika maarufu kama oil chafu. Oil chafu zina aina zake, nitazitaja kwa makundi yake:

Zilizo Maarufu
  • Oil zilizotumika kutoka kwenye injini za magari, mitambo, na mashine mbalimbali.
  • Hydraulic zilizotumika kutoka kwenye gearbox za magari, mitambo, na mashine mbalimbali.
Hizi zipo kila kona ya miji, sehemu za kufanyia service ya vyombo vya moto na kwenye karakana mbali mbali za vyombo vya moto.

Zisizotambulika Sana
  • Tope toka kwenye matank makubwa ya kuhifadhia mafuta.
  • Mabaki ya mafuta toka kwenye meli zinazoleta mafuta.
  • Mabwawa ya kuhifadhia uchafu unaosafishwa (sledge) kutoka kwenye matank na hifadhi za mafuta.
  • Mafuta ghafi.
Zilizo Ngeni Kwa Wengi
  • B.O (Base Oil): Hii ni oil maalum inayotumika kwenye bahari kuu kufukuza maji kwenye mwamba wakati wa kuchoronga kwa ajili ya utafiti wa gesi asilia.
  • O.B.M (Oil Base Mud): Hii haina tofauti na B.O ila hii inakuwa imechanganyika na tope zaidi kuliko B.O.
  • Condensate: Haya ni mabaki ya gesi wakati wa kuchuja gesi asilia.
Aina zote hizo zinawekwa kwenye kundi moja la oil chafu, na zote zinawaka japo zinatofautiana ukali wa moto. Na kuna kati ya hizi aidha zinatumika moja kwa moja ama zinachujwa kwa njia mbalimbali na kupata kitu kinaitwa I.D.O (Industrial Diesel Oil).

Nitaendelea...
 
Biashara ya Oil Chafu

Biashara ya oil chafu ni biashara kubwa inayowaingizia watu mamilioni kwa mwezi, na vituo vikubwa viko maeneo yafuatayo:
  • Tabata Dampo
  • Temeke
  • Mbagala
  • Buza
  • Kigamboni
Kuna baadhi ya wafanyabiashara wanaosafirisha oil chafu mpaka nje ya nchi, hasa katika nchi za:
  • Zambia
  • Kenya
  • Uganda
Hii ni biashara isiyopenda utapeli, ghiliba, uongo wala udanganyifu. Kufanya hivyo ni kujitakia kifo cha mapema na cha fasta sana!

Udanganyifu ambao unavumilika uko kwa wakusanyaji na wasambaji wadogo, ambao huongeza maji na unga wa mfano ili kuongeza ujazo. Hawa kuna mbinu ya kuwabaini na kuwadhibiti.

Oil chafu rangi yake halisi ni nyeusi tii, inawaka haraka, na ina mlipuko mzuri.
Oil chafu iliyochakachuliwa inakuwa na weusi uliochakaa na haiwaki vizuri
Oil chafu iliyochakachuliwa ukiiwasha moto wake hupaparika hauna utulivu kabisa
Test nyingine ni kudondosha tone la oil kwenye karatasi nyeupe baada ya kuikoroga vizuri.. Kama ina maji basi kwenye lile tone kwenye karatasi kutakuwa na mduara wa unyevu.
Test ya mwisho ni kutumbukiza fimbo ndefu ndani ya tank na kuitoa.. Kama kuna maji utaona wazi mafuta yakijitenga na maji
Kwa kifupi hilo ndio faili zima la oil chafu.. Kama kuna niliyosahau ni madogo dogo
 
Biashara kitaa
wauzaji-wa-oil-chafu-1024x1024.jpg
 
Kutokana na ongezeko kubwa la viwanda Tanganyika, mahitaji ya malighafi nayo yameongezeka kwa kiasi kikubwa sana. Kuna baadhi ya malighafi ambazo zamani hazikuwa na thamani yoyote. Ni aidha ziligawiwa bure, zilitupwa, au ziliuzwa kwa bei rahisi.

Leo twende na hii malighafi ya oil iliyotumika maarufu kama oil chafu. Oil chafu zina aina zake, nitazitaja kwa makundi yake:

Zilizo Maarufu
  • Oil zilizotumika kutoka kwenye injini za magari, mitambo, na mashine mbalimbali.
  • Hydraulic zilizotumika kutoka kwenye gearbox za magari, mitambo, na mashine mbalimbali.
Hizi zipo kila kona ya miji, sehemu za kufanyia service ya vyombo vya moto na kwenye karakana mbali mbali za vyombo vya moto.

Zisizotambulika Sana
  • Tope toka kwenye matank makubwa ya kuhifadhia mafuta.
  • Mabaki ya mafuta toka kwenye meli zinazoleta mafuta.
  • Mabwawa ya kuhifadhia uchafu unaosafishwa (sledge) kutoka kwenye matank na hifadhi za mafuta.
  • Mafuta ghafi.
Zilizo Ngeni Kwa Wengi
  • B.O (Base Oil): Hii ni oil maalum inayotumika kwenye bahari kuu kufukuza maji kwenye mwamba wakati wa kuchoronga kwa ajili ya utafiti wa gesi asilia.
  • O.B.M (Oil Base Mud): Hii haina tofauti na B.O ila hii inakuwa imechanganyika na tope zaidi kuliko B.O.
  • Condensate: Haya ni mabaki ya gesi wakati wa kuchuja gesi asilia.
Aina zote hizo zinawekwa kwenye kundi moja la oil chafu, na zote zinawaka japo zinatofautiana ukali wa moto. Na kuna kati ya hizi aidha zinatumika moja kwa moja ama zinachujwa kwa njia mbalimbali na kupata kitu kinaitwa I.D.O (Industrial Diesel Oil).

Nitaendelea...
Asante Mshana Jr
 
Aisee hii ya maji iliwahi nitokea nilichokifanya nami nikapunguza oil nzuri nikaongeza maji nikawatimbia pale na mshikaji wangu pongo aisee walitetemeka ikabidi wanipe pure oil ni miaka minne imepita ila mtaan pale wanatoaga respect alafu mi niko cool
 
Matumizi yake bado yapo hidden, nauliza hasa kwa watu wakawaida

Matumizi yake bado yapo hidden, nauliza hasa kwa watu wakawaida
Watu wa kawaida matumizi hao ni kidogo sana
. Kuna wanaopima kwa lita na kuuza kwenye hardwares kama mbadala wa 'treated timbers'
. Kuna wanaotumia kama dawa ya kupunguza harufu kwenye mashimo ya vyoo hasa uswazi
.Kuna wanaotumia majumbani kama sumu kwenye mazalia ya wadudu waharibifu
.Ni kinga ya nyoka pia
 
Aisee hii ya maji iliwahi nitokea nilichokifanya nami nikapunguza oil nzuri nikaongeza maji nikawatimbia pale na mshikaji wangu pongo aisee walitetemeka ikabidi wanipe pure oil ni miaka minne imepita ila mtaan pale wanatoaga respect alafu mi niko cool
Hiyo ni ubwela ubaya😀😀😀
 
Hawa wakusanyaji wa mitaani ndio msingi wa oil chafu kwa wakusanyaji wa kati.. Hakuna uhuni wasioujua kwenye hii biashara.. Wengi hizi baiskeli sio zao ni za matajiri na wamepewq target kwa siku kiwango cha kukusanya.. Na wanapewa na mitaji pia
Kuna kiwango wakifikisha baiskeli zinakuwa zao moja kwa moja.. Na kwa baadhi huanza kuwauzia matajiti moja kwa moja bila kupewa mtaji
downloadfile-2.jpg
 
Biashara ya Oil Chafu

Biashara ya oil chafu ni biashara kubwa inayowaingizia watu mamilioni kwa mwezi, na vituo vikubwa viko maeneo yafuatayo:
  • Tabata Dampo
  • Temeke
  • Mbagala
  • Buza
  • Kigamboni
Kuna baadhi ya wafanyabiashara wanaosafirisha oil chafu mpaka nje ya nchi, hasa katika nchi za:
  • Zambia
  • Kenya
  • Uganda
Hii ni biashara isiyopenda utapeli, ghiliba, uongo wala udanganyifu. Kufanya hivyo ni kujitakia kifo cha mapema na cha fasta sana!

Udanganyifu ambao unavumilika uko kwa wakusanyaji na wasambaji wadogo, ambao huongeza maji na unga wa mfano ili kuongeza ujazo. Hawa kuna mbinu ya kuwabaini na kuwadhibiti.

Oil chafu rangi yake halisi ni nyeusi tii, inawaka haraka, na ina mlipuko mzuri.
Oil chafu iliyochakachuliwa inakuwa na weusi uliochakaa na haiwaki vizuri
Oil chafu iliyochakachuliwa ukiiwasha moto wake hupaparika hauna utulivu kabisa
Test nyingine ni kudondosha tone la oil kwenye karatasi nyeupe baada ya kuikoroga vizuri.. Kama ina maji basi kwenye lile tone kwenye karatasi kutakuwa na mduara wa unyevu.
Test ya mwisho ni kutumbukiza fimbo ndefu ndani ya tank na kuitoa.. Kama kuna maji utaona wazi mafuta yakijitenga na maji
Kwa kifupi hilo ndio faili zima la oil chafu.. Kama kuna niliyosahau ni madogo dogo
Una madini. Yani Mshana Jr ni sawa na mgodi tuu
 
Back
Top Bottom