Pdidy wa Mwanza azua hofu kwa kudaiwa kubaka wanawake na wasichana kimiujiza

Joined
Nov 19, 2024
Posts
94
Reaction score
307
Mtu mmoja asiyefahamika ambaye amepachikwa jina la Pdidy anatafutwa kwa udi na uvumba kwa tuhuma za kubaka wanawake na watoto kimiujiza. Inadaiwa mbakaji huyo inapofika usiku kuanzia saa 7 usiku huingia kwenye nyumba mbalimbali ambapo hubaka wanawake, kujeruhi au kuiba mali. Mashuhuda wanadai kwamba anapoingia ndani huwezi kusikia milango ikifunguliwa, na anaweza kuwa chumba kingine akifanya uhalifu huku walio vyumba jirani wasisikie kinachoendelea.

RPC mkoa wa Mwanza, Kamanda Mutafungwa amesema taarifa wanazo za mtu huyo anayetenda uhalifu kimiujiza hivyo jeshi la polisi halifanyi kazi kimiujiza kwani litakakikisha linawakamata wote wanaotenda makosa.

Your browser is not able to display this video.
 
Kwa mara nyingine tena popobawa wa kingosha awapelekea moto kisawasawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…