Peacock hotels na unyanyasaji wa kijinsia

Mkuu ndah ni kweli kabisa,ila watu wamejaa tamaa za uzinzi muno muno kuna kipindi waheshimiwa fulan mawaziri walikuwa wakija pale afikasana kweney moja ya baa ya mbunge mmoja walikuwa kama wanacheza draft leo asha m nachukua saleli
 
hapo nadhani inakuwa mnakubaliana kabisa, huwezi kukubali mpaka unabeba mimba na hujui cha kumpatia mwanao kisa unalinda kazi ambayo bado unajua ni ya mshahara mdogo huwezi kujikimu wewe na mwanao, wadada smtymz tunarubunika na vitu vidogo sana jamani...hapo mlirubuniwa mkarubunika., kwa hayo mengine pole sana.
 

Haloo; umeelewa ujumbe au ndion ushabiki kabla ya chai kijana?

my points were clear kwamba jambo lazima lifuatiliwe hata kama aliyepost ni nani kwani kajitolea mno kusema yaliyo ndani sana [kwa maana nyingine action point ndiyo hiyo]

Kweli; ushabiki mgumu sana
 
Hapo kimatare umelenga.

Tunapozungumzia swala la uzalendo tuwe tunamaanisha, kwani kuwa mzalendo haina maana kama unalihujumu taifa lako mwenyewe.


...Unajua mwanamke mara nyingi hawezi kuzungumza matusi yote kwa mumewe,Atabaki kusema tuu kazi mahali pale ni ngumu.Sasa ujue mtu mzima akisema hivyo.............(.....)

Kweli inapofika usiku unamtaka mkeo halafu anakuwa amechoka na kusema kazi ni ngumu mhhhh.... Tujiulize jamani.


Turudisheni uzalendo kama Timor, tuwe na uchungu na mali za umma, hata nguvu zetu binafsi tusikubali ziishe bure tuu eti kwa sababu tunafanya kazi kwa mtanzania mwenzetu.



Mambo ya kubabaika na wageni tuyaacheni, tukubali kuwa sisi tunaweza, ukimlipa mtanzania vizuri naye atafanya kazi yako vizuri.

Hili la ukwepaji wa kodi linajulikana hata ndani ya TRA, Kiongozi mmoja wa TRA alikuwa akija kwa huyu Bwana kuchukua bahasha kila mara. DAWASCO je? TANESCO je!? Billi hizo hazilipi ipasavyo zaidi zaidi hutoa bahasha tuu.

Mimi huwa nashangaa kuona Tanesco wanapambana na wenye viduka kuhusu mambo ya bill wakati mtu hatumii hata 150KWh kwa mwezi na kuachana na mtu ambaye ameweka substation katika jengo lake.

Na dawasco wanapambana na mtu anayetumia lita 1,200 kwa mwezi na kumuacha anayetumia lita 1,200,000 kwa wiki. Shame upon you who are after bahasha.

Yupo Waziri mmoja katika awamu ya nne alikuwa Mali Asili na Utalii jina sitamtaja alikuwa na chumba chake ghorofa ya 7 kwa ajili ya ufuska tuu,hapewi bill huyu....

Duuhh huyo waziri nadhani alikuwa na tabia ya kupenda mikutano ya mikoani ili apate nafasi ya kukimbia nyumbani wakati yupo hapa dar... hiyo kali wazee
 
Yupo Waziri mmoja katika awamu ya nne alikuwa Mali Asili na Utalii jina sitamtaja alikuwa na chumba chake ghorofa ya 7 kwa ajili ya ufuska tuu....

Wewe nawe, yaani umeamua kumtaja halafu unasema hautamtaja!!
 
Hapa ndiko uzandiki wote nilioueleza siku mbili zilizopita unakofanyika.Nimesoma maoni yote ya wadau,Lakini mpaka leo hii hakuna hata mmoja aliyejaribu kunitafuta nimpatie vithibitisho halisi.

Njooni wote ,TRA,DAWASCO,TANESCO,PCCCB,TISS Ikulu na Wana-JF niwape data tena tangu ianze hii hotel.Mikataba feki iliyotumika kukodishiwa LAPF Millenium Tower,Ukiukwaji wa uingizaji bidhaa mbali na vifaa vinavyotumika hapa hotelini.


Peacock Hotels-City Centre

Bibi Titi Mohamed Road,
P O Box 70270
Dar es Salaam,
Tanzania.


TEL: +255 22 2120334 /
+255 22 2114071

FAX: +255 22 2117962


E-MAIL: info@peacock-hotel.co.tz
reservation@peacock-hotel.co.tz


Website: Welcome to Peacock Hotel – City Center


Peacock Hotels Limited commenced operations in 1992 as a small city Hotel with only 27 rooms on 3 floors. The last decade has seen Peacock Hotel evolve from a small city Hotel to a medium sized city hotel. The hotel now has 24 standard rooms, 69 deluxe rooms, two bars and two restaurants.
 
timor angalia pm nimekupa no yangu nipe taarifa kamili nakuja hapo muda si mrefu
 
Ukweli kuendeshwa na mzawa sisi hatuna shida nalo, Ila mateso tunayoyapa, vitisho, masumango, Leo ukija hapa Hotelini hakuna mtu aliye radhi kukueleza yanayojiri ndani kwa kuhofia hatima yake.
Timor, sikuwa nimeiangalia hii topic tangu inaanza, nilichukulia simple tu... Do you need our input?

Naweza kutuma mwandishi ukutane nae. Wasiwasi wangu ni kama hutoficha ukweli pia. Hatokuwa biased kwako tu, atatakiwa kujua uongozi unatoa kauli gani dhidi ya shutuma hizi.

Kama uko tayari wasiliana nami kwa PM nami leo au kesho nitakutumia mtu ili kuweza kukata mzizi wa fitna.
 
Mi nawashangaa sana watu, huyu Timor amejitahidi kueleza kila kitu kinacho endelea huko kwenye hotel za Peackok...then watu wanakuja na micomment, oooh hao mabinti wanajirahisi kupata favour, oooh wanakubaliana ili watembee nao, ooh wametoa taarifa wapi, ooh kwa nini hawapeleki pilisi /mahakamani etc!

Mmeambiwa watu wenye elimu zao hapo hawakai...which means hawa wanao nyanyaswa hawakubahatika kwenda shule, so though kipato chao ni kodo hapo, hawana option nyingine bali ni kushikilia hicho walicho nacho! kama kuna mtu anaweza kuwasaidia kwa namna nyingine basi aseme sio kuleta masimango yasiyo na msingi...eleweni kwanza situation anayoielezea na watu wanaohusika ndio mtoe meneno ya kejeli!

Sasa ngoja na mimi nitoe ushuhuda kidogo hapa;kati ya mwaka 2007 na 2008 nilikuwa na rafiki yangu wa kike, yeye ni graduate(B.COM) wa UDSM alipata kibarua pale PEACKOK mnazi mmoja kama accountant, alikuwa analalamika sana kuhusu mambo ya fuatayo;

1) Maslahi ya wafanyakazi
Alikuwa anadai kuwa mmiliki wa hotel alikuwa na tabia kwanza ya kulipa mishahara midogo sana (yeye alikuwa nalipwa Tshs 250,000 pm) ukiacha hiyo, kwenye michango ya NSSF /PPF alikuwa nakwepa kwa kuchangia huko kidogo na pia automatically na TRA PAYE alikuwa anawakilisha kidogo, yaani ukiukaji wa sheria ulikuwa unfanywa hivi; kwa mfano huyu aliyekuwa anapata Tshs 250,000, mshahara huu aliugawa katika mafungu mawili, moja alilipa Tshs 100,000 kupitia PAYROLL na pili Tshs 150,000 alikuwa alipia pembeni, accordingly NSSF alichangia only 10% ya 100,000 na pia PAYE ilikatwa kwenye 100,000 tu!

2) Muda wa kazi

Huyu rafiki yangu alikuwa anaingia saa mbili asubuhi (8.00am) nakutoka kati ya saa kumi na mbili na nne usiku, hiyo ni kila siku (seven days a week).

3) Likizo

Kwa muda wa mwaka mmoja na kama miezi miwili aliyofanya kazi pale, huyu rafiki yangu hakupa hata ruhusa ya kwenda likizo, wakati sheria ya kazi inawataki waajiri kutoa walau siku 28 kwa mwaka kama likizo!

Mpo hapo wadau, huyu ni GRADUATE how about std seven's?
 
Last edited:


Acha kudandia gari kwa mbele na wewe? Elelewa kwanza real situation kabla ya kutoa matusi kwa huyo dada! Unasema ni habari za uzushi, lete habari za ukweli sio unapinga tu wakati huna facts.....nahisi wewe utakuwa mmoja wapo ya vijana wa Mfugale au na wewe unatabia hiyo!

Umeshaambiwa wenye shule zao hawakai hapo, which means huyo dada ni mmoja wapo ya wenye shule.......bado umenga'ng'ania eti kama haridhiki akatafute kazi sehemu nyingine, sema wapi wanaajiri STD 7 kirahisi kivile?

Huyu dada hata kama hana elimu, huyu mwenye hotel hana haki ya kumnyanyasa hivyo, anatakiwa kuheshimu huduma anayoitoa hapo hotelini na kumcompansate accordingly. Ok amemzalisha mtoto basi amtunze mtoto huyo nalo haliwezekani tena? Huu ni ubandidu na uhuni....waache kutumia pesa zao kunyanyasa wanawake kijinsia!

Milo -----Watch out your words!
 
Dada mbona unadanganya ummah ??

Hutoi contacts zako tukueleweje

moderator naomba huyo member apewe ban mbona anachezea watu ??

Ametoa malalamiko yake anataka kusaidiwa anayayuka
 
Wewe unachekesha kweli!
Sasa kazi unataka miguu na hiyo kitu unavua mwenyewe kisha unapanua miguu wewe mwenyewe kwani unabakwa?Njaa zenu zitasababisha muambukizwe UKIMWI hivi hivi.
 
Wewe unachekesha kweli!
Sasa kazi unataka miguu na hiyo kitu unavua mwenyewe kisha unapanua miguu wewe mwenyewe kwani unabakwa?Njaa zenu zitasababisha muambukizwe UKIMWI hivi hivi.

Sio vizuri kumtusi mtu, kama huna msaada au ushauri kwake nyamaza. After all huyu dada ataisaidia sana TRA kama ataanika wizi uliofanyika, kama wazawa wenyewe wanaiibia nchi yao kwa nini wageni waogope kuiba? Charity begins at home.
 
Sio vizuri kumtusi mtu, kama huna msaada au ushauri kwake nyamaza. After all huyu dada ataisaidia sana TRA kama ataanika wizi uliofanyika, kama wazawa wenyewe wanaiibia nchi yao kwa nini wageni waogope kuiba? Charity begins at home.

Good comment!

Watu wengine ndugu yangu ni waajabu sana, just can't understand them! Nashukuru kwa kumjibu Fidel 80!
 
Hakuna sababu ya kumtusi mtu, pia mojawapo ya hatua ni pamoja na hii ya kutuhabarisha hapa ili kama kuna mwenye msaada basi asaidie.
 
Jamii kwanini timor anatoa badai halafu anakimbia imi nimemfuata chemba nikampa mpaka no yangu ya simu tuwasiliane nimpe mwanasheria toka lchp hajibu anakimbia maana yake nini ?
 
Jamii kwanini timor anatoa badai halafu anakimbia imi nimemfuata chemba nikampa mpaka no yangu ya simu tuwasiliane nimpe mwanasheria toka lchp hajibu anakimbia maana yake nini ?

.....tatizo ni leads alizotoa........na miadi mliompa..........zinamlengesha......she must be careful..........otherwise......usiwaamin sana hawa wafanyabiashara..........ni "MAFIAs"
 
Jamii kwanini timor anatoa badai halafu anakimbia imi nimemfuata chemba nikampa mpaka no yangu ya simu tuwasiliane nimpe mwanasheria toka lchp hajibu anakimbia maana yake nini ?

Sidhani kama ni sahihi kumtuhumu mtu kwa kutoa hoja yake, elewa huyu inawezekana hata hiyo net ni ya kulia timing.
 
Jamani Shy kila kitu nimekupa sijakimbia.Hujui kwamba mimi ni mwaajiriwa na hawa mafisadi.Internet yenyewe hadi kibandani Kisutu unadhani mchezo.Hebu fungua PM yako uaanze kazi basi mapema kesho asubuhi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…