Pendekezo: Jangwani paboreshwe Wamachinga wa Kariakoo wahamishiwe hapo

Pendekezo: Jangwani paboreshwe Wamachinga wa Kariakoo wahamishiwe hapo

Championship

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2019
Posts
5,500
Reaction score
10,616
Wanabodi,

Ni dhahiri kwamba ipo changamoto kubwa sana ya wafanyabiashara hawa wadogo pale Kariakoo. Wamekuwa wengi mno na kusababisha adha kubwa sana kwa wenye maduka na wateja waendapo kupata huduma.

Ninapendekeza eneo lote la jangwani painuliwe, pajengwe vizuri na kuwekewa vibanda modern ambapo machinga wa pale kariakoo wapangishwe kwa malipo nafuu ili waweze kuendelea na kujikimu kimaisha.

Lile eneo ni zuri kwasababu lipo katikati ya mji, ni karibu na mahali watakapopata bidhaa (yaani maduka ya Kariakoo) na ni rahisi kwa wateja kuweza kuwafikia.

Ujenzi wa pale jangwani wala hauwezi kuwa complicated ikiwa ile mito mitatu itachimbwa na kujengewa vizuri ili ipitishe maji.

Muhimu tu ile mito ijengwe vizuri kwa plan ya kuwa njia ya usafirishaji kwa miaka ijayo. Ule mto unaweza kuchimbwa kutoka pale selander mpaka mbezi na kuvuta maji ya bahari ili kuwe na boti za abiria na utalii. Hii teknolojia ipo, nimeiona pale Dubai na Thailand.

Nawasilisha.
 
Ukweli ni kwamba umachinga ni tatizo na unatakiwa kuisha kabisa. Watu wawe na maduka na walipe kodi badala ya huu utaratibu wa kuwa na vibanda nje ya maduka na hawalipi kodi. Huu sio utaratibu mzuri wa kutoa ajira na kiukweli wanao nufaika ni waingizaji wa vitu wasiolipa kodi sio hawa vijana. Viwanda, Uvuvi, ufugaji na Kilimo ndiyo suluhisho la vijana.

Vyuo vya veta vitumike kutoa elimu ya hivi vitu. Wamachinga wanachangia uchafuzi mkubwa wa mazingira, kuharibu mipangilio ya miji na kuongoza kwa kuuza vitu fake.

Jangwani ni sehemu yenye mafuriko na mikondo ya maji inatakiwa kutengenezwa kama sehemu ya kupumzika wamachinga wataishia kupafanya jalala pale na mvua ikija uchafu wote utaishia kwenye mkondo wa maji na mito.
 
Yeah naunga mkono hoja

Kariakoo imebanana sana

Halafu ni rahisi kupajenga pale unajenga kama flyover watu wanakaa juu inakuwa shopping mail!!

Dubai waamisha bahari na kujenga project mpaka gorofa 60+

Sisi tunashindwa kujenga juu ya mkondo wa maji?

Tena bonde lote kuanzia mkwajuni mpaka karume palitakiwa ndio liwe Machinga shopping mail.!
 
Ukweli ni kwamba umachinga ni tatizo na unatakiwa kuisha kabisa. Watu wawe na maduka na walipe kodi badala ya huu utaratibu wa kuwa na vibanda nje ya maduka na hawalipi kodi. Huu sio utaratibu mzuri wa kutoa ajira na kiukweli wanao nufaika ni waingizaji wa vitu wasiolipa kodi sio hawa vijana. Viwanda, Uvuvi, ufugaji na Kilimo ndiyo suluhisho la vijana.

Vyuo vya veta vitumike kutoa elimu ya hivi vitu. Wamachinga wanachangia uchafuzi mkubwa wa mazingira, kuharibu mipangilio ya miji na kuongoza kwa kuuza vitu fake.

Jangwani ni sehemu yenye mafuriko na mikondo ya maji inatakiwa kutengenezwa kama sehemu ya kupumzika wamachinga wataishia kupafanya jalala pale na mvua ikija uchafu wote utaishia kwenye mkondo wa maji na mito.
Mkuu hii unaongelea plan ya muda mrefu ambayo itaendana na ukuaji wa uchumi wa nchi ambao unategemea sana sera na mipango. Hapa mimi nazungumzia mpango utakaookoa jahazi kwa sasa.

Hao machinga watalipia hivyo vibanda hivyo serikali itapata mapato.
 
Ukweli ni kwamba umachinga ni tatizo na unatakiwa kuisha kabisa. Watu wawe na maduka na walipe kodi badala ya huu utaratibu wa kuwa na vibanda nje ya maduka na hawalipi kodi. Huu sio utaratibu mzuri wa kutoa ajira na kiukweli wanao nufaika ni waingizaji wa vitu wasiolipa kodi sio hawa vijana. Viwanda, Uvuvi, ufugaji na Kilimo ndiyo suluhisho la vijana.

Vyuo vya veta vitumike kutoa elimu ya hivi vitu. Wamachinga wanachangia uchafuzi mkubwa wa mazingira, kuharibu mipangilio ya miji na kuongoza kwa kuuza vitu fake.

Jangwani ni sehemu yenye mafuriko na mikondo ya maji inatakiwa kutengenezwa kama sehemu ya kupumzika wamachinga wataishia kupafanya jalala pale na mvua ikija uchafu wote utaishia kwenye mkondo wa maji na mito.
Umetoa hoja mfu tupu.

1. Elimu sio hitaji la kila mtu.

2. Kuto kulipa kodi ni ujinga wa serikali kutokutengeneza mifumo mizuri ya kuwafanya walipe kodi.

3. Vitu fake, sio kila mtu anauwezo wa ku afford original. Vilevile hatuwezi kusema ni fake kwasababu ni approved na TBS. Kama ni fake maana yake TBS taasisi ya serikali imeshindwa kudhibiti hivyo wanayoiongoza wameshindwa kazi.

4. Katika maisha lazima kuwe na makundi (wenye nacho na wasio nacho) hivyo hawa machinga ni kimbilio la wasio nacho, ukisema wapewe frame hawataweza kuafford.

Solution aliyotoa mtoa mada ni nzuri lakini alivyosema wajenge mifereji ambayo inaweza kupitisha boat ameiongezea serikali mzigo ambao walishindwa kuubeba tangu enzi na enzi.
 
Hao sio wasitaarabu,huo mto utakuwa wakijani ndio utaziba kabisa
Mkuu hapa ni rahisi tu kuweka usimamizi mzuri. Pale moshi wameweza kushinda uchafu ingawa kuna machinga wengi sana.
 
Ninapendekeza eneo lote la jangwani painuliwe, pajengwe vizuri na kuwekewa vibanda modern ambapo machinga wa pale kariakoo wapangishwe kwa malipo nafuu ili waweze kuendelea na kujikimu kimaisha.
Hivi "Machinga Complex" machinga wapo siku hizi?

Huko Jangwani ndiko hawaendi kabisa kwa sababu watakosa biashara. Watu wapo Kariakoo, Jangwani wakafanye nini!

Swala na Machinga linahitaji akili kubwa kulishughulikia kuliko ilivyo sasa.

Kumbuka pia, sio swala la Dar es Salaam peke yake, na hata Dar yenyewe, tatizo halipo Kariakoo peke yake, limeenea kila mahali.
 
Umetoa hoja mfu tupu.

1. Elimu sio hitaji la kila mtu.

2. Kuto kulipa kodi ni ujinga wa serikali kutokutengeneza mifumo mizuri ya kuwafanya walipe kodi.

3. Vitu fake, sio kila mtu anauwezo wa ku afford original. Vilevile hatuwezi kusema ni fake kwasababu ni approved na TBS. Kama ni fake maana yake TBS taasisi ya serikali imeshindwa kudhibiti hivyo wanayoiongoza wameshindwa kazi.

4. Katika maisha lazima kuwe na makundi (wenye nacho na wasio nacho) hivyo hawa machinga ni kimbilio la wasio nacho, ukisema wapewe frame hawataweza kuafford.

Solution aliyotoa mtoa mada ni nzuri lakini alivyosema wajenge mifereji ambayo inaweza kupitisha boat ameiongezea serikali mzigo ambao walishindwa kuubeba tangu enzi na enzi.
Asante sana mkuu kwa mchango wako wenye tija. Ila mkuu wangu nilipofika Dubai na Thailand niliwaonea wivu sana jinsi walivyojenga ule mto na ambavyo serikali yao inapata mapato makubwa sana kwa utalii wa boti na zile boti zinavyorahisisha usafiri usiokuwa na foleni. Sioni kama ni mzigo, ni fursa kubwa sana.
 
Asante sana mkuu kwa mchango wako wenye tija. Ila mkuu wangu nilipofika Dubai na Thailand niliwaonea wivu sana jinsi walivyojenga ule mto na ambavyo serikali yao inapata mapato makubwa sana kwa utalii wa boti na zile boti zinavyorahisisha usafiri usiokuwa na foleni. Sioni kama ni mzigo, ni fursa kubwa sana.
Ndio ni fursa kubwa sana ila je changamoto za jangwani huzijui, je umeanza kuzisikia lini na ni hatua gani ambazo zimechukuliwa kudhibiti kabla ya mwaka 2015.
 
Hivi "Machinga Complex" machinga wapo siku hizi?

Huko Jangwani ndiko hawaendi kabisa kwa sababu watakosa biashara. Watu wapo Kariakoo, Jangwani wakafanye nini!

Swala na Machinga linahitaji akili kubwa kulishughulikia kuliko ilivyo sasa.

Kumbuka pia, sio swala la Dar es Salaam peke yake, na hata Dar yenyewe, tatizo halipo Kariakoo peke yake, limeenea kila mahali.
Nakubaliana nawe kwamba hili ni tatizo kubwa na lipo maeneo mengi. Mimi hapa nimeangalia suluhisho kwa ajili ya kariakoo ambapo kwakweli pana hali mbaya sana.

Machinga complex imefeli kwasababu ya namna ilivyojengwa. Machinga hawahitaji complex structures, vibanda modern ambavyo vinakuwa chini vitatosha.

Pale jangwani pakiwa rasmi na wote wakiondolewa kariakoo basi wateja watawafuata bila tatizo.
 
Umetoa hoja mfu tupu.

1. Elimu sio hitaji la kila mtu.

2. Kuto kulipa kodi ni ujinga wa serikali kutokutengeneza mifumo mizuri ya kuwafanya walipe kodi.

3. Vitu fake, sio kila mtu anauwezo wa ku afford original. Vilevile hatuwezi kusema ni fake kwasababu ni approved na TBS. Kama ni fake maana yake TBS taasisi ya serikali imeshindwa kudhibiti hivyo wanayoiongoza wameshindwa kazi.

4. Katika maisha lazima kuwe na makundi (wenye nacho na wasio nacho) hivyo hawa machinga ni kimbilio la wasio nacho, ukisema wapewe frame hawataweza kuafford.

Solution aliyotoa mtoa mada ni nzuri lakini alivyosema wajenge mifereji ambayo inaweza kupitisha boat ameiongezea serikali mzigo ambao walishindwa kuubeba tangu enzi na enzi.
Kuna hoja "mfu" zaidi ya hii uliyotoa hapa?

Hapana, nadhani hii ni hoja ya kiwenda wazimu.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kusema "Elimu sio hitaji" kwa mtu yeyote; ni kichaa tu ndiye anayeweza kuwaza hivyo.

Halafu wewe hujali kuwepo kwa 'vitu feki'?

Keshokutwa tukakuweke kwenye gari lenye spea feki likakupondeponde huko unakoishi wewe, usiwatakie na wengine yawakute.

Katika watu wenye mawazo mgando, wewe utakuwa unashika namba moja.
 
Ndio ni fursa kubwa sana ila je changamoto za jangwani huzijui, je umeanza kuzisikia lini na ni hatua gani ambazo zimechukuliwa kudhibiti kabla ya mwaka 2015.
Pale jangwani hakuna changamoto serious sana kama wataalamu wakifanya proper design ya ile mito na kuinua kidogo ile ardhi.

Kabla ya 2016 pale palikuwa safi kabisa, mikutano ilikuwa inafanyika mingi sana. Walipojenga ile stendi ya mwendokasi na kuwaondoa wale vijana waliokuwa wanauza mchanga ndipo tatizo likaanza.

Ile mito ijengwe vizuri na tatizo halitakuwepo tena.
 
Kuna hoja "mfu" zaidi ya hii uliyotoa hapa?

Hapana, nadhani hii ni hoja ya kiwenda wazimu.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kusema "Elimu sio hitaji" kwa mtu yeyote; ni kichaa tu ndiye anayeweza kuwaza hivyo.

Halafu wewe hujali kuwepo kwa 'vitu feki'?

Keshokutwa tukakuweke kwenye gari lenye spea feki likakupondeponde huko unakoishi wewe, usiwatakie na wengine yawakute.

Katika watu wenye mawazo mgando, wewe utakuwa unashika namba moja.
Kazi ya vyombo vilivyoanzishwa kisheria kudhibiti na kukagua uingizwaji na uuzaji wa bidhaa fake wanao ongoza vyombo hivi wasipo fuatilia nao vitawamaliza kama wewe nae ni miongoni hufanyi kazi yako kwa umakini vitu unavyoita fake vitakumaliza.

Elimu si hitaji la kila mtu, kama unazungumzia ya darasani.

Lakini elewa maana pana ya elimu kwanza na sijui wewe ulizungumzia elimu ipi?

Iliyo rasmi au isiyo rasmi?
 
Nakubaliana nawe kwamba hili ni tatizo kubwa na lipo maeneo mengi. Mimi hapa nimeangalia suluhisho kwa ajili ya kariakoo ambapo kwakweli pana hali mbaya sana.

Machinga complex imefeli kwasababu ya namna ilivyojengwa. Machinga hawahitaji complex structures, vibanda modern ambavyo vinakuwa chini vitatosha.

Pale jangwani pakiwa rasmi na wote wakiondolewa kariakoo basi wateja watawafuata bila tatizo.
Mkuu, natafuta mifano ya kukuunga mkono.

Bado naona ni vigumu kwa mtu kutoka nyumbani kwenda kuwatafuta Machinga walipo Jangwani, na asiende Kariakoo madukani.

Hivi Manzese inaweza kuwa mfano? Buguruni na kwingineko?

Sehemu zote walipo Machinga ni sehemu za barabara kuu karibu na makazi ya watu au sokoni wanakopitia watu wengi wakisaka mahitaji yao.

Ukimweka Machinga Jangwani, labda uweke na stendi kubwa ya Daladala zikipitia na kutokea hapo toka sehemu mbalimbali za mji.
 
Pale jangwani hakuna changamoto serious sana kama wataalamu wakifanya proper design ya ile mito na kuinua kidogo ile ardhi.

Kabla ya 2016 pale palikuwa safi kabisa, mikutano ilikuwa inafanyika mingi sana. Walipojenga ile stendi ya mwendokasi na kuwaondoa wale vijana waliokuwa wanauza mchanga ndipo tatizo likaanza.

Ile mito ijengwe vizuri na tatizo halitakuwepo tena.
Ok ushauri mzuri ufanyiwe kazi ila sina hakika kama wataufanyia kwani mafile wanayo mezani ya mapendekezo mengi tu lakini hawajafanyia kazi to date.
 
Kazi ya vyombo vilivyoanzishwa kisheria kudhibiti na kukagua uingizwaji na uuzaji wa bidhaa fake wanao ongoza vyombo hivi wasipo fuatilia nao vitawamaliza kama wewe nae ni miongoni hufanyi kazi yako kwa umakini vitu unavyoita fake vitakumaliza.

Elimu si hitaji la kila mtu, kama unazungumzia ya darasani.

Lakini elewa maana pana ya elimu kwanza na sijui wewe ulizungumzia elimu ipi?

Iliyo rasmi au isiyo rasmi?
Hii ni tofauti na wewe unayoyashabikia, kwamba vitu feki vinawasaidia maskini. Hii ni dhana potofu kabisa ambayo madhara yake kwa nchi ni makubwa.

Hivi vitu feki itabidi vishindane na vitu halali vinavyozalishwa kihalali na viwanda vya hapa, bado wewe unavililia vitu hivyo hata kama serikali itakosa kodi na vijana wako watanufaika kuuza vitu hivyo kuliko kuzalisha vya halali na vyenye viwango?

Hukueleza ni elimu ipi uliielenga kwenye bandiko lako.

Hata hivyo, elimu ni elimu tu, iwe rasmi au isiwe rasmi sioni tofauti yake.
 
Mkuu, natafuta mifano ya kukuunga mkono.

Bado naona ni vigumu kwa mtu kutoka nyumbani kwenda kuwatafuta Machinga walipo Jangwani, na asiende Kariakoo madukani.

Hivi Manzese inaweza kuwa mfano? Buguruni na kwingineko?

Sehemu zote walipo Machinga ni sehemu za barabara kuu karibu na makazi ya watu au sokoni wanakopitia watu wengi wakisaka mahitaji yao.

Ukimweka Machinga Jangwani, labda uweke na stendi kubwa ya Daladala zikipitia na kutokea hapo toka sehemu mbalimbali za mji.
Mkuu unayafahamu yale masoko yanayotembea kwa zamu katika siku za wiki pale biafra, goba, kunduchi, tegeta etc? Wale ni machinga per se na wanavutia wateja ambao huwezi kuamini.

Masoko yapo mengi tu na bidhaa zipo lakini watu na v8 zao kutoka salasala na bahari beach wanaenda kujaza 'friji' kwa wale wamachinga.. unajua kwanini? Bei yao iko chini ya bei ya soko.

Mimi naona inawezekana watu wakawafuata pale maana barabara ipo na daladala nyingi sana zinapita pale ikiwemo mwendokasi.
 
Hii ni tofauti na wewe unayoyashabikia, kwamba vitu feki vinawasaidia maskini. Hii ni dhana potofu kabisa ambayo madhara yake kwa nchi ni makubwa.
Hivi vitu feki itabidi vishindane na vitu halali vinavyozalishwa kihalali na viwanda vya hapa, bado wewe unavililia vitu hivyo hata kama serikali itakosa kodi na vijana wako watanufaika kuuza vitu hivyo kuliko kuzalisha vya halali na vyenye viwango?

Hukueleza ni elimu ipi uliielenga kwenye bandiko lako.

Hata hivyo, elimu ni elimu tu, iwe rasmi au isiwe rasmi sioni tofauti yake.
Feki hapana aisee niambie ni less-quality ambao huletwa kulingana na hali za kiuchumi za wananchi zilivyo.

So sio kwamba machinga wanauza fake bali wametumia kigezo kwamba wananchi wengi hawapo vizuri kiuchumi lakini wanahitaji vitu vizuri hivyo wanawaletea kama hivyo vizuri ambavyo ni less-quality na watengenezaji au wazalishaji wa vitu vizuri wanajua sio wote wanaweza kuafford high end product hivyo wanatengeneza na less-quality (low end product) ili wasiwatenge hawa wasio vizuri kiuchumi wasio mudu vizuri.

Kwahiyo hamna fake kwakuwa vyote vipo regulated na mamlaka iliyopewa dhamana hiyo.

Usiku mwema chief.
 
Kuna hoja "mfu" zaidi ya hii uliyotoa hapa?

Hapana, nadhani hii ni hoja ya kiwenda wazimu.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kusema "Elimu sio hitaji" kwa mtu yeyote; ni kichaa tu ndiye anayeweza kuwaza hivyo.

Halafu wewe hujali kuwepo kwa 'vitu feki'?

Keshokutwa tukakuweke kwenye gari lenye spea feki likakupondeponde huko unakoishi wewe, usiwatakie na wengine yawakute.

Katika watu wenye mawazo mgando, wewe utakuwa unashika namba moja.
Mkuu nadhani hapa mnachanganya kidogo kwa kutumia neno 'fake'.. kimsingi hizi bidhaa nyingi zinazouzwa cheap sio fake.. ni bidhaa za grade iliyo chini ya ile grade ya juu.

Inapaswa serikali iweke clear guideline ili mnunuzi awe anajua wakati ananunua kama bidhaa ni highest quality, medium au low quality. Inataka tu usimamizi ili watu wapate huduma kulingana na level zao za kiuchumi.

Muhimu tu serikali iangalize yale maeneo sensitive sana wasiruhusu bidhaa ambazo ni medium au low quality.
 
Back
Top Bottom