Pendekezo: Kitengo cha Upelelezi kitolewe Polisi

Naunga mkono hoja, nafikiri hata China CID inajitegemea.
 
Anaweza asifanye upelelezi wa uhakika kwa sababu dpp kazi yake ina siasa kidogo.

Epelelezi unatakiwa ubakie kama taaluma na utalaam.
Siasa gani iliyopo kwenye ofisi ya DPP mkuu? Kile kitengo kimejaa wanasheria na sio wanasiasa!

Nimependa sana wazo hili na kiukweli Ni moja kati ya vitu adhimu kukutana navyo hapa JF wajuzi wa mambo ni wakati sasa kulisukuma Jambo hili mbele.
 
Point kubwa sana hii, Rais alipokuwa kusini wakati akimtumbua boss wa TAKUKURU alisema kuwa kuna wakati Polisi ndo wanaochezesha ramani na watu wanaotuhumiwa na kukwamisha upelelezi. Kwa kweli ni nchi zetu tu hizi ndo zinaunganisha Idara ya Upelelezi na Police Service. Ifike mahala Polisi ijitenge na Upelelezi kabisa, na waajiriwa wa Idara hii wawe hawatokani na jeshi la Polisi.
 
Kwa kweli mie navyoona ni nchi chache tena hasa za Africa ndo tumebaki na Ivestigation departments ndani ya Police... Nchi zingine unakuta idara za upelelezi hazihusiani kabisa na Police na huwa wanakuwa powerful kupenya popote, vitambulisho vyao ni vizito saaana mpaka Police wanawaogopa. Chukulia mfano India, Pakistan, FBI ya America au SFO ya UK ziko independent mpaka vibopa wanashtakiwa kama kawa
 
Siasa gani iliyopo kwenye ofisi ya DPP mkuu? Kile kitengo kimejaa wanasheria na sio wanasiasa!

Nimependa sana wazo hili na kiukweli Ni moja kati ya vitu adhimu kukutana navyo hapa JF wajuzi wa mambo ni wakati sasa kulisukuma Jambo hili mbele.
Thanks kwa kuunga mkono hoja.. ipo siku Tanzania itakua mahali pazuri pa kuishi
 
Bado zitakuwa taasisi mbili zinazofanya kazi moja! Old wine new bottle sijui kama kutakuwa na unafuu nadhani issue kuwa ni kutunga sheria zitakazosimamia taasisi hizo na muundo mbadala wa utendaji !
 
Tanzania Bureau of Investigation(TBI) ipo miaka mingi sana, ukienda ghorofa ya Saba wizara ya mambo ya ndani Dar utawakuta hapo wamejaaa na kazi wanapiga sanaaa.
Wa polisi ni ma CID, na wao wanafanya kazi nzuri sana.
 
Study your kantri kabla ya kutoa maoni ya marekebisho ya kimuundo (re-establishment). Lakini pia ni utafiti ulionyesha root-cause ya tatizo? Where to get the funds to run an independent bureau? Hujui kilio kikubwa cha kutoongezwa kwa mishahara ya watumishi wa umma na hata aho kwenye state apparatus ni kwa sababu tunatumi kila mwezi zaidi ya 5.5Bn kulipa mishahara tu? Na tunakusanya kwa wastani 1.3T. Tutabakiwa na nini kwa ajili ya JKN H.E.P. kule Rufiji? SGR? ATCL? ZAHANATI? HOSPITALI ZA WILAYA? ULINZI?
Namaanisha kuanzisha taasisi nyingine bila sababu iliokuwa ya nguvu ni kuiongeza matumizi ya fedha za umma na hivyo kuwa recurrent expenditure kubwa saaaaana kuliko development expenditure.
 
wapelelezi (polisi) ndio wapoteza ushahidi na wacheleweshaji kesi wakubwa
 
Tusijidanganye na tusijiumize. Kilio kikubwa kwenye establishments ni lack of enough funds to run the newly established offices. Hakuna mtu anapenda kazi nyingi au kutokuwepo kwa ufanisi. Ukiwa na sekta ya umma kubwa hasa upande wa utoaji huduma usiiingizia chochote kwenye mfuko mkuu wa hazina, ni maumivu makubwa kwa walipa kodi na kwa bajeti ya maendeleo. Kenya wamelemewa na miundo iliyosababishwa na katiba yao ya 2010, wanataka kubadilisha tena kupunguza mizigo.
 
Swala sio kuwa na ofisi nyingi swala ni namna gani serikali inajipanga kupata matokeo mazuri kwa resources chache.
 
kwenye state apparatus ni kwa sababu tunatumi kila mwezi zaidi ya 5.5Bn kulipa mishahara tu? Na tunakusanya kwa wastani 1.3T.
Kama makusanyo ni 1.3T na mishahara ni 5.5B, huoni mishahara ni 0.42% ya makusanyo? Au ulikusudia kuandika 550B?
 
Mkuu ni 550 B na sio 5.5 B[emoji28]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…