Pendekezo laletwa wabunge wa Afrika Mashariki wachaguliwe sawa na wabunge wa Jamhuri Dodoma

Pendekezo laletwa wabunge wa Afrika Mashariki wachaguliwe sawa na wabunge wa Jamhuri Dodoma

Cicero

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2016
Posts
2,924
Reaction score
3,074
Habari zenu wadau.
  • Kwa wale mnaofuatilia shughuli za Jumuiya ya Afrika Mashariki mtagundua kwamba Bunge la Afrika Mashariki limeshindwa kufanya kikao hata kimoja tangu kuchaguliwa kwa wabunge wapya, sababu kuu ikiwa ni Kenya na South Sudan kushindwa kuchagua wawakilishi wao kwenye bunge hilo. Kenya wanasingizia eti wako busy na uchaguzi wao mkuu na South Sudan walikosea kufuata procedure za kuchagua wabunge wa Afrika Mashariki kama ilivyo kwenye mkataba (wanawake hawakutimia idadi stahiki).
  • Sheria na kanuni za bunge hilo zinasema kwamba akidi itatimia pale ambapo kutakuwa na wawakilishi walau watatu kutoka katika kila nchi mwanachama (I stand to be corrected on this).
  • Hivyo basi kuna pendekezo limeletwa na wadau kwamba ili kuepuka deadlock kama hii inayosababishwa na system iliyopo ya uchaguzi, wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wawe wanachaguliwa na wananchi moja kwa moja sawa na wabunge wenzao wa kitaifa yaani kwenye uchaguzi mkuu unakuwa unamchagua Rais, mbunge wa Afrika Mashariki na mbunge wa Jamhuri kama ilivyo kwenye Umoja wa Ulaya na ECOWAS.
  • Hili limekaaje? Ni zipi faida na hasara za hili pendekezo hususan kuelekea hatua ya mwisho ya mtangamano ambayo ni kuundwa kwa Serikali ya Shirikisho la Afrika Mashariki? Mimi kila siku I always say mnaopinga kuundwa kwa serikali ya EAC mmechelewa sana mtakuja shtuka kitu tayari kishasimama. Serikali haiundwi mara moja ila ni gradual process. Sasa hivi imeanzishwa passport ya pamoja ya EAC....mara inakuja sarafu moja ya Afrika Mashariki, bunge nalo ndo hilo liko mbioni kupewa more power and legitimacy. Yote haya ndio serikali ya EAC inavyoumbwa kama mtoto tumboni mwa mama yake!
SOURCE: EAC to consider direct voting for EALA members | NTV
 
Nipendekezo zuri lakin hapo gharama za uendeshwaji wa bunge naona kama vile itakuwa kubwa sana
 
Hili naliunga mkono kwa dhati, hata kwetu tumezinguana sana watu wanateuliwa kwa kutumia vigezo vya ovyo.
 
Back
Top Bottom