SoC02 Pendekezo; Mfumo mbadala wa kudhibiti moshi unaotokana na viwanda ili kutunza mazingira

SoC02 Pendekezo; Mfumo mbadala wa kudhibiti moshi unaotokana na viwanda ili kutunza mazingira

Stories of Change - 2022 Competition
Joined
Aug 2, 2022
Posts
60
Reaction score
75
1. UTANGULIZI
Viwanda ni moja kati ya shughuli ya kiuchumi ambayo muhimu katika ukuaji wa uchumi wa nchi kwa sababu viwanda husababisha kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa na huduma zinazopatikana kwa watu kwa bei nafuu, hupunguza utegemezi kwa nchi zingine na inaboresha uchumi, hupelekea kupanda kwa kiwango cha maisha na kuongeza nafasi mpya za ajira. Kwa upande mwingine viwanda pia vina hasara zake hususani katika uchafuzi wa mazingira. Kwamfano moshi unaotoka viwandani unaposambaa katika hewa unaweza kuwa na adhari kwa binadamu, wanyama na mimea. Kwa sasa viwanda vingi vimewekwa mabomba maalum yanayoelekeza moshi kwenda katika anga lakini bado mfumo huo una athari ndani yake ambazo nitaziorodhesha hapa, na kupendekeza mfumo mpya na faida zake.

2. MFUMO UNAOTUMIKA KWA SASA
Idadi kubwa ya viwanda duniani vimesimikwa mabomba maalum kwa juu yanayoelekeza moshi kuelekea juu katika anga ambapo moshi viwandani umeelekezwa kwenda juu kwa kutumia mabomba maalum.

2.1. ATHARI ZA MFUMO UNAOTUMIKA KWA SASA
Mfumo huu unaathari mbalimbali ikiwemo kuharibika kwa tabaka la ozoni kwa sababu mfumo umeelekeza moshi wa viwandani kwenda kwenye anga. matokeo ya kuharibika kwa Tabaka la Ozoni ni kuruhusu mionzi ya jua (sun radiation) kufikia uso wa ardhi hivyo kutishia afya ya viumbe hai katika ikolojia mbalimbali. Mionzi ya jua ukifika katika uso wa dunia husababisha kuongezeka kwa magonjwa ya kansa ya ngozi, uharibifu wa macho kama vile mtoto wa jicho unaosababisha upofu, upungufu wa uwezo wa mwili kujikinga na maradhi na kujikunja kwa ngozi, hivyo mtu aweza kuonekana mzee kuliko umri wake. Pia idadi kubwa ya watoto wapo katika hatari zaidi ya kupata madhara haya. Madhara mengine ni pamoja na kuathiri ukuwaji wa aina mbalimbali za mimea.

2.2. NJIA YA KUZIKABILI ATHARI
Njia ya kuzikabili athari za mfumo huu ni kubadili maelekezo wa mabomba ya moshi ambapo mabomba hayo yanapaswa yatokee kiwandani kuelekea chini ya ardhi ambapo kutakuwa na chemba maalum iliyotengenezwa kwa ajili ya kuuhifadhia moshi badala ya kuuelekeza mabomba ya moshi katika anga. Baada ya muda moshi huo unaweza weza kuvunwa kutoka katika ardhi na unaweza kutumia kama malighafi ya kutengenezea bidhaa mbalimbali kama rangi nyeusi ya kiatu (kiwi). Najua wengi mtajiuliza moshi unaweza vipi kuwa malighafi lakini ukienda katika bomba la kutolea moshi la gari au pikipiki ukichunguza utakutana na nta ya masinzi meusi yaliyotengenezwa na moshi kisha utakuwa umepata majibu ya swali uliokuwa unajiuliza.

3. MFUMO MPYA NINAOUPENDEKEZA KUZUIA ATHARI ZA MOSHI WA VIWANDANI

Mfumo mpya ninaoupendekeza utakuwa kama ifuatavyo;

(a) Bomba la moshi lililoelekezwa kwenda chini ya ardhi ambapo kutakuwa na chemba maalumu ya kuhifadhia moshi. Ambapo itakuwa tofuati na mfumo wa awali ambao mabomba ya moshi kutoka viwandani yalikuwa yameelekezwa juu ili moshi uelekee angani.

(b) Uwepo wa chemba maalum ya kuhifadhia moshi iliyotengenezwa chini ya ardhi ambayo itakuwa inatumika kupokea moshi katika mabomba maalum yaliyoelekezwa chini ya ardhi na kuhifadhia moshi. Chemba ya kuhifadhia moshi inatakiwa iwe imesiribwa au kuwekwa saruji katika kuta zake ili kuzuia sumu au kemikali iliyopo kwenye moshi isiingie katika udongo na kuathiri viumbe vinavyoishi chini ya ardhi pamoja na mimea.

(c) Uwepo wa mlango maalum katika chemba utakaokuwa unatumika kupakua malighafi itokanayo na moshi ili ikatumie kutengenezea bidhaa mbalimbali kama rangi nyeusi inayopakwa katika kiatu alimaarufu kama (KIWI).

3.1. FAIDA ZA MFUMO MPYA
Mfumo mpya wa kuelekeza mabomba ya moshi chini ya ardhi ambapo kutakuwa na chemba ya kuhifadhia moshi iliyotengenezwa chini ya ardhi unafaida zifuatazo;

(a) Husaidia kutunza mazingira kwa kuzuia uchafuzi wa hali ya hewa kwani moshi ukitapakaa katika anga hupelekea hali ya hewa kuchafuka.

(b) Kuzuia kuaribika kwa tabaka la ozoni kwa sababu moshi unatoka kiwandani unakuwa umeelekezwa chini ya ardhi katika chemba maalum na sio angani. Kama tabaka la ozoni halitoaribiwa mionzi mikali ya jua itakuwa haifiki kirahisi katika uso wa dunia na hupelekea usalama wa afya ya viumbe hai wa ainambalimbali. Pia huzuia kuongezeka kwa magonjwa ya kansa ya ngozi, uharibifu wa macho kama vile mtoto wa jicho unaosababisha upofu, upungufu wa uwezo wa mwili kujikinga na maradhi na kujikunja kwa ngozi.

(c) Hurahisisha upatikanaji wa malighafi ambayo inaweza kutumika kutengenezea bidhaa mbalimbali kama rangi nyeusi inayotumika kung'arisha bidhaa nyeusi za ngozi kama viatu.

4. HITIMISHO
Mwisho ninapendekeza mfumo huu wa kuelekeza mabomba ya kusafirisha moshi chini ya ardhi katika chemba maalumu utumike katika viwanda ili kuhakikishiwa na usafi wa mazingira kwa kuthibiti moshi unaotoka katika viwanda usisambae katika anga na kusababisha uchafuzi wa hali ya hewa au uharibifu wa tabaka la ozoni ili kuepukana na athari mbalimbali zinazoweza kutokea baada ya kuaribika kwa tabaka la ozoni kama magonjwa ya kansa ya ngozi, uharibifu wa macho kama vile mtoto wa jicho unaosababisha upofu, upungufu wa uwezo wa mwili kujikinga na maradhi na kujikunja kwa ngozi. Athari hizo zitaepukika kwa sababu kama tabaka la ozoni litakuwa halijaharibika na mionzi mikali ya jua ambayo inaathari haiwezi kufika katika uso wa dunia kiurahisi.

Maana ya maneno yaliyotumika:
Tabaka la ozoni: hili ni tabaka la hewa ambalo liko katika anga la juu la pili lifahamikalo kitaalamu kama stratosphere ambalo linaweka aina ya tabaka ama tambara angani ambalo linazuia mionzi mikali ya jua inayoweza kuleta athari katika afya za binadamu na viumbe hai kuja moja kwa moja duniani.

Uso wa dunia: Maana yake ni ardhi.

MICHORO YA PICHA HAPO CHINI INAONESHA MFUMO UNAOTUMIKA KWA SASA NA PICHA NYINGINE INAONESHA MFUMO NINAOUPENDEKEZA KUZUIA ATHARI ZA MOSHI WA VIWANDANI.

20220804_063037.jpg
20220804_134115.jpg
 
Upvote 6
Nime kuuliza moshi ni nini ? Mbona ujanijibu ?

Unajua nimeshangaa unataka ufungie moshi ambayo ni gesi kwenye chemba hii sayansi yako umesomea wapi ?

hili suala la kuweka mahandaki yani chemba ambazo zitaifadhi moshi ambapo ni gesi, tukisema tuzifungie zinaweza kulipuka kwasababu kila zitakavyo zidi kujibana sehemu moja zitapelekea mlipuko ambao baadae moshi utapanda tena kuelekea kwenye anga hewa.


Kama tukisema zitoke kwenye mlango wa chemba, zitasababisha kuondoa hewa ya oxygen kwenye Tabaka la biosphere, ambalo ndiyo tupo Mimi na wewe, hakuna kiumbe kitakacho baki hai wala miti na mimea tena vyote vitakufa kabisa kwa sababu oxygen itakuwa haipo.

Kutakuwa na mimoshi ya carbon gas ambazo ni sumu ambayo itaondoa hewa yote ya oxygen, ambayo ndiyo inatufanya sisi tuishi na imechukua asilimia 21 tu ambazo ni ndogo sana.!!!!!


Nimeona kunakipengele unazungumzia uchafuzi wa anga hewa kwa moshi unaotoka viwandani.

nikwambie moshi unaotoka viwandani hauwezi kuchafua anga hewa kwa kiasi ambacho kita haribu Tabaka la hewa. Kwasababu asilimia kubwa ya uwepo wa Tabaka ni gravity itokayo kwenye core ya dunia.


Kwahiyo ili tuharibu tabaka la anga hewa itabidi tupate nuclear bomb bomu la nyuklia litaweza kusababisha zile lava volcano zilizo banana kwenye kiini cha dunia kulipuka na kuanza kuja kwenye shape yajuu ambayo tupo mimi na wewe.

Alafu hapo ndipo ile gravity ya dunia itakufa hapo itapelekea lile puto ambalo ni atmosphere tabaka la anga hewa kuharibika hapo ndipo ile mionzi ya jua itachoma dunia yetu na kuunguza kila kitu. Kwahiyo vimoshi vidogo kutoka kwenye viwanda haviwezi kukinzana na gravity ya dunia lazima tupate kitu kizito sana.

Inahitajika nguvu kubwa ya moshi ili kuharibu Tabaka la anga hewa Ila sharti ni moja tu, lazima hiyo nguvu iweze kubalance gravity ya dunia kitu ambacho ni kigumu kufanywa na vimoshi vya viwandani.

Na hapo bado sijakuelezea kwamba dunia yetu inavutwa na jua inamaana gravity ikifa na tabaka likiharibika basi dunia yetu itaanguka moja kwa moja kwenye USO wa jua.


Nimeona kuna kioengele unaelezea tabaka likiharibika basi binadamu watapata kansa kutokana na mionzi ya jua.

Tabaka likiharibika hakuna hata kirusi kitakacho baki kila kitu kitaungua kama uonavyo moto wa jiko ukiunguza karatasi basi ndivyo itakavyo tokea kwenye dunia yetu.

Hakuna elimu ngumu kama ya sayansi ya anga kwahiyo kwenye chapisho lako umekosea kwa sababu hiyo mada yako wanasayansi na mainjinia walisha ikalia kikao tayari. Tatizo lengine jaribu kuwa mchunguzi wa mambo kabla ujaandika chochote kuhusu sayansi.

Siyo kwa ubaya Mimi Nime kupigia kura alafu nime kurekebisha kaka usiwe na wasiwasi.
 
FB_IMG_16597490924804059.jpg

FB_IMG_16597490823643762.jpg





FB_IMG_16597489636099259.jpg

( pichani ni nuclear bomb ) sasa kaka uje uniambie kati hivyo vimoshi vya viwanda vinawezaje kuharibu tabaka la anga hewa ? Unaambiwa pamoja na kwamba Bomu la nyuklia linaweza kiharibu atmosphere ya dunia tukiachana na nuclear bomb chengine kinacho weza kuharibu tabaka la anga hewa ni atomic bomb elimu za Tanzania zinapaswa kuboreshwa kwenye sayansi.
 
Nime kuuliza moshi ni nini ? Mbona ujanijibu ?

Unajua nimeshangaa unataka ufungie moshi ambayo ni gesi kwenye chemba hii sayansi yako umesomea wapi ?

hili suala la kuweka mahandaki yani chemba ambazo zitaifadhi moshi ambapo ni gesi, tukisema tuzifungie zinaweza kulipuka kwasababu kila zitakavyo zidi kujibana sehemu moja zitapelekea mlipuko ambao baadae moshi utapanda tena kuelekea kwenye anga hewa.


Kama tukisema zitoke kwenye mlango wa chemba, zitasababisha kuondoa hewa ya oxygen kwenye Tabaka la biosphere, ambalo ndiyo tupo Mimi na wewe, hakuna kiumbe kitakacho baki hai wala miti na mimea tena vyote vitakufa kabisa kwa sababu oxygen itakuwa haipo.

Kutakuwa na mimoshi ya carbon gas ambazo ni sumu ambayo itaondoa hewa yote ya oxygen, ambayo ndiyo inatufanya sisi tuishi na imechukua asilimia 21 tu ambazo ni ndogo sana.!!!!!


Nimeona kunakipengele unazungumzia uchafuzi wa anga hewa kwa moshi unaotoka viwandani.

nikwambie moshi unaotoka viwandani hauwezi kuchafua anga hewa kwa kiasi ambacho kita haribu Tabaka la hewa. Kwasababu asilimia kubwa ya uwepo wa Tabaka ni gravity itokayo kwenye core ya dunia.


Kwahiyo ili tuharibu tabaka la anga hewa itabidi tupate nuclear bomb bomu la nyuklia litaweza kusababisha zile lava volcano zilizo banana kwenye kiini cha dunia kulipuka na kuanza kuja kwenye shape yajuu ambayo tupo mimi na wewe.

Alafu hapo ndipo ile gravity ya dunia itakufa hapo itapelekea lile puto ambalo ni atmosphere tabaka la anga hewa kuharibika hapo ndipo ile mionzi ya jua itachoma dunia yetu na kuunguza kila kitu. Kwahiyo vimoshi vidogo kutoka kwenye viwanda haviwezi kukinzana na gravity ya dunia lazima tupate kitu kizito sana.

Inahitajika nguvu kubwa ya moshi ili kuharibu Tabaka la anga hewa Ila sharti ni moja tu, lazima hiyo nguvu iweze kubalance gravity ya dunia kitu ambacho ni kigumu kufanywa na vimoshi vya viwandani.

Na hapo bado sijakuelezea kwamba dunia yetu inavutwa na jua inamaana gravity ikifa na tabaka likiharibika basi dunia yetu itaanguka moja kwa moja kwenye USO wa jua.


Nimeona kuna kioengele unaelezea tabaka likiharibika basi binadamu watapata kansa kutokana na mionzi ya jua.

Tabaka likiharibika hakuna hata kirusi kitakacho baki kila kitu kitaungua kama uonavyo moto wa jiko ukiunguza karatasi basi ndivyo itakavyo tokea kwenye dunia yetu.

Hakuna elimu ngumu kama ya sayansi ya anga kwahiyo kwenye chapisho lako umekosea kwa sababu hiyo mada yako wanasayansi na mainjinia walisha ikalia kikao tayari. Tatizo lengine jaribu kuwa mchunguzi wa mambo kabla ujaandika chochote kuhusu sayansi.

Siyo kwa ubaya Mimi Nime kupigia kura alafu nime kurekebisha kaka usiwe na wasiwasi.
Umefafanua vyema

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app
 
Nime kuuliza moshi ni nini ? Mbona ujanijibu ?

Unajua nimeshangaa unataka ufungie moshi ambayo ni gesi kwenye chemba hii sayansi yako umesomea wapi ?

hili suala la kuweka mahandaki yani chemba ambazo zitaifadhi moshi ambapo ni gesi, tukisema tuzifungie zinaweza kulipuka kwasababu kila zitakavyo zidi kujibana sehemu moja zitapelekea mlipuko ambao baadae moshi utapanda tena kuelekea kwenye anga hewa.


Kama tukisema zitoke kwenye mlango wa chemba, zitasababisha kuondoa hewa ya oxygen kwenye Tabaka la biosphere, ambalo ndiyo tupo Mimi na wewe, hakuna kiumbe kitakacho baki hai wala miti na mimea tena vyote vitakufa kabisa kwa sababu oxygen itakuwa haipo.

Kutakuwa na mimoshi ya carbon gas ambazo ni sumu ambayo itaondoa hewa yote ya oxygen, ambayo ndiyo inatufanya sisi tuishi na imechukua asilimia 21 tu ambazo ni ndogo sana.!!!!!


Nimeona kunakipengele unazungumzia uchafuzi wa anga hewa kwa moshi unaotoka viwandani.

nikwambie moshi unaotoka viwandani hauwezi kuchafua anga hewa kwa kiasi ambacho kita haribu Tabaka la hewa. Kwasababu asilimia kubwa ya uwepo wa Tabaka ni gravity itokayo kwenye core ya dunia.


Kwahiyo ili tuharibu tabaka la anga hewa itabidi tupate nuclear bomb bomu la nyuklia litaweza kusababisha zile lava volcano zilizo banana kwenye kiini cha dunia kulipuka na kuanza kuja kwenye shape yajuu ambayo tupo mimi na wewe.

Alafu hapo ndipo ile gravity ya dunia itakufa hapo itapelekea lile puto ambalo ni atmosphere tabaka la anga hewa kuharibika hapo ndipo ile mionzi ya jua itachoma dunia yetu na kuunguza kila kitu. Kwahiyo vimoshi vidogo kutoka kwenye viwanda haviwezi kukinzana na gravity ya dunia lazima tupate kitu kizito sana.

Inahitajika nguvu kubwa ya moshi ili kuharibu Tabaka la anga hewa Ila sharti ni moja tu, lazima hiyo nguvu iweze kubalance gravity ya dunia kitu ambacho ni kigumu kufanywa na vimoshi vya viwandani.

Na hapo bado sijakuelezea kwamba dunia yetu inavutwa na jua inamaana gravity ikifa na tabaka likiharibika basi dunia yetu itaanguka moja kwa moja kwenye USO wa jua.


Nimeona kuna kioengele unaelezea tabaka likiharibika basi binadamu watapata kansa kutokana na mionzi ya jua.

Tabaka likiharibika hakuna hata kirusi kitakacho baki kila kitu kitaungua kama uonavyo moto wa jiko ukiunguza karatasi basi ndivyo itakavyo tokea kwenye dunia yetu.

Hakuna elimu ngumu kama ya sayansi ya anga kwahiyo kwenye chapisho lako umekosea kwa sababu hiyo mada yako wanasayansi na mainjinia walisha ikalia kikao tayari. Tatizo lengine jaribu kuwa mchunguzi wa mambo kabla ujaandika chochote kuhusu sayansi.

Siyo kwa ubaya Mimi Nime kupigia kura alafu nime kurekebisha kaka usiwe na wasiwasi.
ulisoma Geographia kaka
 
ulisoma Geographia kaka
Mimi ni mwanasayansi wa anga, elimu ya geographia nazani inatakiwa ifanyiwe marekebisho kwa sababu inahusiana na sayansi kwahiyo mtu anapo zungumzia matabaka ya anga heti yakiaribika sijui kutakua na kansa sijui kutakuwa na joto MTU huyo anakuwa anaelimu ndogo ya shule ya msingi


Kama na wewe unaamini moshi Wa viwanda unaweza kuharibu Tanaka la anga hewa hivi unajua dunia ilishawai kupigwa na steroids kubwa Kama mwezi hivi unajua dunia ilishawai kupigwa atomic bomb hivi unajua kule Ukraine mabomu ya supersonic yamesababisha moshi pia unajua nikisema nitoke nje ya Tanaka la anga news nitakuwa outer space sasa nikisema niangalie hata kaeneo katakacho onesha jengo la kiwanda sitaweza kuona kwasababu kiwanda kimechukua Kama kapunje kwa atom kwenye dunia likubwa kwahiyo vimoshi haviwezi kuathiri atmosphere ya dunia ili atmosphere iharibike lazima ipatikane kitu chenye nguvu angalau Mara mbili ya mwezi wetu huu sayansi ni pana Sana nazani umenielewa


Kwahiyo masomo ya kuharibika kwa atmosphere kwa kutumia moshi Wa viwanda ni elimu mbovu na atmosphere ikiharibika zile gesi zilizo tunzwa ndani ya atmosphere zitapotea kwahiyo hakuna cha kansa Ila nikwamba hakuta KKuwa na yoyote atakaye baki hai hata virusi vitateketea.
 
Mimi ni mwanasayansi wa anga, elimu ya geographia nazani inatakiwa ifanyiwe marekebisho kwa sababu inahusiana na sayansi kwahiyo mtu anapo zungumzia matabaka ya anga heti yakiaribika sijui kutakua na kansa sijui kutakuwa na joto MTU huyo anakuwa anaelimu ndogo ya shule ya msingi


Kama na wewe unaamini moshi Wa viwanda unaweza kuharibu Tanaka la anga hewa hivi unajua dunia ilishawai kupigwa na steroids kubwa Kama mwezi hivi unajua dunia ilishawai kupigwa atomic bomb hivi unajua kule Ukraine mabomu ya supersonic yamesababisha moshi pia unajua nikisema nitoke nje ya Tanaka la anga news nitakuwa outer space sasa nikisema niangalie hata kaeneo katakacho onesha jengo la kiwanda sitaweza kuona kwasababu kiwanda kimechukua Kama kapunje kwa atom kwenye dunia likubwa kwahiyo vimoshi haviwezi kuathiri atmosphere ya dunia ili atmosphere iharibike lazima ipatikane kitu chenye nguvu angalau Mara mbili ya mwezi wetu huu sayansi ni pana Sana nazani umenielewa


Kwahiyo masomo ya kuharibika kwa atmosphere kwa kutumia moshi Wa viwanda ni elimu mbovu na atmosphere ikiharibika zile gesi zilizo tunzwa ndani ya atmosphere zitapotea kwahiyo hakuna cha kansa Ila nikwamba hakuta KKuwa na yoyote atakaye baki hai hata virusi vitateketea.
Kwahiyo boss sayansi yako inataka kutuambia moshi wa viwandani hauna athari zozote..? Maana unaudharau sana mwanasayansi wetu. Then so umesema Geographia ifanyiwe marekebisho mana inahusiana na sayansi kwahiyo unataka kutuambia ulisoma Biology, Chemistry, na Physics bila Geographia ukawa mwanasayansi wa anga.
 
Back
Top Bottom