Elections 2010 Pengo: Msiwachague wanaogawa khanga na fulana


Nimependa haya maneno kwa kuwa yana maana kubwa sana ndani yake maana siku ya mwisho ukiwa umesimama mbele ya haki utaulizwa yote uliyoyafanya
 
Sasa Huyu Ndio ASKOFU Maneno yake yamekaa kibusara zaidi!! huwezi ukamfananisha na KAKOBE ambaye ameweka kisasi mbele sababu TANESCO!


Njiwa umepigwa falsafa baba.

Askofu hapo anamaanisha Kikwete na genge lake ni watu hatari, wezi, walafi, wanafiki, waongo wasichaguliwe tena.
 


Naomba nikupongeze kwa maelezo yako - ambayo kwa upande wangu naona ni KWELI KABISA. Hata hivyo naomba usiwalaumu sana viongozi wa Dini kwani sio wote WANAJUA KWA UNDANI VITU VINAVYOENDELEA - MIKATABA FEKI INAYOFANYIKA; RUSHWA ZINAZOTOLEWA NYINGINE KWA SIRI ETC. NA KAMA KAWAIDA WAKIJUA NI LAZIMA WAWE NA USHAHIDI PIA; NA PIA SIO WOTE WANA UJASIRI WA KUONGEA AU WALIO NA MAHALI SAHIHI PA KUONGELEA - KUMBUKA DR. SLAA ALIONGELEA BUNGENI KWA VILE ALIKUWA NA CHANCE YA KUFANYA HIVYO . NAKUUNGA MKONO NA NAMPONGEZA DR. SLAA KWA UJASIRI WAKE WA KUWEKA MAMBO WAZI NA KAMA MUNGU ANGEMPA NAFASI YA KUWA RAIS - NAAMINI TAIFA LETU LINGEBADILIKA NA UMASKINI UKATUTOKA - MUNGU MBARIKI DR. SLAA NA KUMLINDA - AMEN!!
 
Sasa Huyu Ndio ASKOFU Maneno yake yamekaa kibusara zaidi!! huwezi ukamfananisha na KAKOBE ambaye ameweka kisasi mbele sababu TANESCO!
njiwa bwana mbona kakobe kafuta ibada tarehe 31 watu wakapige kura?nae ni askofu hakuna mtu ambaye ni PERFECT.HUMAN BY NATURE NI SELFISH alikuwa anavutia kwake.
 
ujumbe huu umewafikia watu wangapi? au ndo waliokuwa ibadani na wana jamii forum tu ambao wengi wenu mnauwezo wa kulipia huduma hii ya internet na kupata taarifa kama hizi?mh kazi ipo kwani najua wapewa kanga na tshirt walikuwa wachache ibadani hapo anapoongoza askofu huyu,pili na kama ni magazeti wapewa tshit na khanga wachache wananunua magazeti kujua ujumbe uliotolewa na askofu.

 
Amefanya vizuri kwakumbusha wananchi nadhani wengi sasa wamepata ufahamu ni swala la wakati tuu
 
We dada angu Joyce unamjua Pengo au unamsikia kuna prominent figures hata akisemea chumbani na mwandishi mmoja tu habari zinashambaa kama moto wa nyika sembuse yeye kasemea hadharani.
 
"Si kuambiwa na mwenyekiti wa jumuiya, kasekista (Mwalimu wa dini), kadinali au padre kuwa mchague fulani, hakuna atakayesimama kwa dhamira yako, anayefaa ni yule anayejiepusha na matendo ya rushwa," alisema Kadinali.

Ya kweli haya! :confused2:
 
alimaaanisha msimchague mtu kwa sababu ya vitu anavyokupa, inaweza kuwa ni pesa pia na hata chadema inaweza kutoa

ila Chadema haijawahi kutoa, hivyo kwa kua CCM imeashathibitika kua inatoa rushwa ya hela, Kanga na Kofia basi, inyimwe kura
 
Wewe mpiga kuar, Pengo amekupa nafasi ya kutumia utashi wako na uelewa ulijaaliwa na Mungu kutambua jema na baya.

Alichofanya ni kukupa dondoo tu, achana na kofia, fulana na khanga. CHagua mtu sahihi... halafu piga kura. Humu sisi kwa habari tunazojua wanotoa kofia, fulana nk, ni wale wale mashati ya kijani. Kubali usikubali
 
Hapa hajatajwa mtu, kwanini watu wanajihisi?...Je ni vibaya mtu akitoa darasa hilo kwa jamii?...Tusiogope vivuli vyetu!...Naona wale waliotumwa hapa JF kwa kazi maalum tayari wamekuja juu, maana wanaona wazi nafasi ya BWANA wao inahojiwa!
The truth is...TUNAHITAJI MABADILIKO ili kutoa nafasi kwa mawazo mbadala!!
 
Ushauri wa busara sana wenye akili timamu wataelewa mazuzu watalalama daima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…