SEASON 2
SEHEMU YA 23
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ jamani kila kitu kinakwenda vizuri.Sasa ni muda wa kujiandaa kwa ajili ya kuelekea huko.Akasema Mathew na kuwachukua Elibariki na Anitha hadi katika chumba ambacho huhifadhi silaha .Akafungua kabati na kutoa fulana nne zisizopenya risasi akawapatia Elibariki na Anitha na moja ikawa kwa ajili ya yule jamaa mwingine watakayemtumia
“ Eli,unaweza kutumia silaha ? Akauliza Mathew
“ Ndiyo ninaweza Mathew , nimewahi kupitia mafunzo katika jeshi la kujenga taifa kwa hiyo ninafahamu kutumia silaha ingawa sijawahi kuingia katika mapambano.” Akasema jaji Elibariki.Mathew akampatia bastora.
“ Ihifadhi hiyo silaha pengine tunaweza kuihitaji” akasema Mathew halafu akaelekea katika chumba alimo Yule jamaa na kumpatia fula moja isiyopenya risasi .
Walipokuwa tayari wakaingia katika gari na kuanza safari wakitanguliwa na Yule jamaa akiwa katika Toyota Carina
ENDELEA…………….
“ Anna jiandae kuna sehemu tunakwenda” Flaviana akamwambia mdogo wake Anna
“ usiku huu? Anna akashangaa
“ Ndiyo kuna sehemu nataka kwenda usiku huu” akasema Flaviana
“Kuna jambo gani la muhimu kiasi cha kutoweza kusubiri hadi asubuhi ? Akauliza Anna ambaye alionekana wazi kwamba hakuwa tayari kuondoka usiku ule.Flaviana akamsogelea na kwa sauti ndogo akasema
“ Elibariki kanipigia simu usiku huu”
“ What ?! Elibariki? Yuko wapi ? Anna akajikuta akiuliza maswali mfululizo
“ Hata mimi sifahamu yuko wapi lakini amenihakikishiwa kwamba yuko sehemu salama” akasema Flaviana
“ Ouh Thank you Lord” akasema Anna
“Umekwishamfahamisha baba kama umeongea na Elibariki? Hata yeye atafurahi sana kusikia kwamba Elibariki yuko mzima .Atafanya mpango wa kwenda kumchukua mahala aliko” akasema Anna
“ Baba nimeongea naye lakini sijamfahamisha chochote kuhusiana na jambo hili na ninaomba usimweleze chochote.Elibariki hataki mtu mwingine yeyote afahamu kuhusiana na jambo hili kwa ajili ya usalama wake .Baada ya Elibariki kunusurika kuuawa sasa nimeanza kuamini yale maneno yake aliyokuwa akisisitiza kwamba kuna kitu kibaya kinachoendelea .” akasema Flaviana
“ Hata mimi shambulio lile limenipa wasi wasi sana .Ninaweza kukubaliana nawe kuhusu jambo hili kwamba kuna kitu kinaendelea chini kwa chini.Unadhani nani anaweza kuwa amefanya shambulio lile?
“ Ni vigumu kufahamu ni nani lakini ninachoweza kuhisi kwa haraka haraka kuna kitu kinachoendela hapa na kama ukikumbuka kuna kitu mama alitaka kutuambia lakini hakuweza kwani alifariki ghafla mchana wa siku ile ambayo alitutaka tuonane naye .Ninahisi kuna jambo kubwa ambalo alitaka kutueleza na kuna hisia zinakuja kwamba huenda jambo hilo alilotaka kutuambia ndilo lillomgharimu uhai wake.Mama alifariki ghafla sana na wewe mwenyewe ulishuhudia sintofahamu iliyokuwepo kuhusiana na sababu ya kifo chake. Elibariki alituambia kwamba wamegundua mama alifariki kwa kuchomwa sindano ya sumu lakini taarifa ile ya madaktari bingwa ambayo baba anaiamini inasema kwamba mama hakufariki kwa sumu.Ukichunguza kwa undani sana masuala haya utagundua kwamba kuna kitu hapa si bure nadhani ndiyo sababu Elibariki hakati tamaa katika jambo hili.Mara ya mwisho nilipooongea naye aliniahidi kwamba hatalala usingizi hadi ukwe liwa jambohili ujulikane na ninahisi hiki ndichokilichotaka kumtoa uhai.Amenitaka nikaonane naye usiku huu kuna jambo anataka kuniambia na nijitahidi niipate ile taarifa ya madaktari bingwa.” Akasema Flaviana
“ Anaitaka ile taarifa? Anataka kuifanyia nini? Akauliza Anna
“ Sifahamu anaitaka kwa ajili gani lakini amesisitiza sana kwamba anaihitaji usiku huu.”
Anna akafikiri kidogo na kusema
“ taarifa yenyewe utaipata vipi wakati anayo baba? Sina hakika kama baba anaweza akakubali Elibariki aipate taarifa ile.”
“ tayari ninayo.Baba amenipatia usiku huu” akasema Flaviana
Anna ambaye tayari alikuwa kitandani akaamka na kujiandaa kisha wakaongozana hadi katika gari la Flaviana wakaondoka.
“ Flaviana unadhani Elibariki alikuwa sahihi kwamba mama aliuawa kwa sumu? Akauliza Anna
“ Siwezi kuwa na uhakika huo Anna lakini ukiangalia namna mambo yalivyotokea unaweza ukakubaliana na jambo hilo kwamba kifo cha mama hakikuwa cha kawaida.Nimekuwa nikilitafakari sana jambo hili .Hebu angalia mama alifariki ghafla na halafu ikatolewa taarifa kwamba usifanyike uchunguzi wowote wa kuhusiana na kifo chake .Hili jambo linashangaza sana kwa sababu haiingii akilini eti mwli wa mke wa rais usifanyiwe uchunguzi kubaini kilichosababisha kifo chake cha ghafla.Hii ni sababu iliyonifanya nimuombe Elibariki anisaidie kufanya uchunguzi ili tuweze kubaini kile kilichosababisha kifo cha mama. Katika uchunguzi uliofanyw ana watu wa Elibariki waligundua kwamba mama alichomwa sindano yenye sumu lakini baadae ikaja tena taarifa nyingine ikisema kwamba mama alikufa kwa shinikizo la damu na hakukuwa na dalili zozote za kuwepo kwa sumu katika mwili wake.Jambo hili linanipa mashaka sana na ninalazimika kuamini kwamba huenda kifo cha mama ni kweli kina mkonowa mtu na kikubwa zaidi kinachonifanya niamini hivyo ni baada ya Elibariki kunusurika kuuawa..Ninajiuliza sana kwa nini Elibariki atake kuuawa sasa hivi? Ni kitu cha kawaida majaji kuwa na maadui wengi na ndiyo sababu wamekuwa wakipatiwa ulinzi lakini kwa niniwatake kumuua sasa hivi? Ukijiuliza swali hili utagundua kwamba lazima kuna kitu kinachohusiana na kifo cha mama.Ninamfahamu Elibariki vizuri akilifuatilia jambo kwa nguvu namna hii lazima kuna sababu maalum.” Akasema Flaviana
“Hata mimi nimekuwa na mawazo kama yako na kilichonifanya niwe na mawazo hayo ni kuhusiana na shambulio la Elibariki.Kitu kingine kinachonipa maswali mengi ni kwamba kwa nini baba amekuwa kimya sana kuhusiana na masuala haya? Kwa masikio yangu nilimsikia Dr Kigomba akitoa amri kwamba watu waliokuwa wakifanya uchunguzi kubaini kilichomuua mama wakamatwe na kudhibitiwa lakini tulipomueleza baba kuhusiana na suala hili amekuwa mzito sana kutuamini na badala yake akadiriki kusema kwamba Dr Kigomba hahusiki kwa namna yoyote ile na suala lolote kuhusiana na kifo cha mama.”akasema Anna
“ Anna unahisi kwamba baba anaweza akawa anafahamu kinachoendelea ? Akauliza Flaviana
“ Siwezi kusema kwamba anahusika moja kwa moja lakini kwa namna alivyolishughulikia jambo hili inanipa mashaka kidogo kuaminikwambahawezi kufahamu kinachoendelea .Inaonekana wazi kabisa kwamba hakulipa ule uzito unaostahili.Aliyefariki ni mke wake na alipaswa kulipa uzito mkubwa sana sana suala hili lakini naona imekuwa tofauti kabisa.Haonekanikujali.haonekani kuumizwana kifocha mama.” Akasema Anna
“ Anna unaweza ukawa sahihi katika hili.Hata mimi japokuwa nilikuwa upande wake kuhusiana na ile taarifa ya madaktari bingwa lakini nilishangazwa zaidi na namna alivyolichukulia suala hili kwa wepesi na kukubali kirahisi maelezo ya Dr Kigomba.Halafu kuna jambo lingine ambalo kwangu mimi naliona kama si la kawaida ,Elibarikiamekuwa akihudhuria katika kila kikao tunachokifanya cha kifamilia.yeye ni sehemu ya familia yetu na ndiyo sababu siku ile nilimuita aje katika kikao kile ili kwa pamoja tuisikie taarifa ya uchunguzi wa kifo cha mama toka kwa madaktari bingwa.Kitu cha kushangaza baba hakuonyesha kufurahi kumuona Elibariki katika kikao kile na ndiyo maana akamtolea maneno yale makali.Kama utakumbuka baada ya kikao aliniita nje na akanifokea sana kwa nini nimemuita Elibariki katika kikao kile .Inaonyesha wazi kwamba hakutaka Elibariki afahamu chochote kuhusiana na taarifa ile.Swali kubwa la kujiuliza hapa ni kwamba kwa nini baba hakutaka Elibariki afahamu chochote kuhusiana na taarifa ile ya kifo cha mama? Binafsi yangu naona kama jambo hili linahitaji kufanyiwa uchunguzi ” akasema Flaviana
“ Tutalichunguzaze Flaviana? Akauliza Anna
“ Hata mimi sielewi lakini kuna haja ya kufanya uchunguzi.Ngoja tukionana na Elibariki usiku huu nitaongea naye kuhusu jambo hili.Yeye anaweza kuwa naushaurimzuri zaidi ” Akasema Flaviana
Waliendelea na safari yao hadi walipofika Simbona hoteli mahala alipoelekezwanaElibariki wakutane ,akapunguza mwendo na kusimamisha gari katika kituo cha basi.Kulikuwa na taksichache eneo lile
“ Hapa ndipo mlipangamkutane?akauliza Anna
“ Ndiyo ! tulipanga tukutane hapa” akasema Flaviana huku akiangaza macho kulitafuta lile gari aliloelekezwa na mara akaliona
“ Anna nitashuka na kuingia katika lile gari la bluu pale mbele.Mle ndimo alimo Elibariki.Utanisubiri hapa hapa,sintakawia sana” akasema Flaviana na kufungua mlango akashuka garini na kuelekea moja kw amoja katika lile gari la bluu akataka kuufungua mlango na kuingia akasita akenda kugonga katika kioo cha dereva.Kioo kikashushwa halafu mtu yule aliyekuwamo ndani ya ile gari akamuamuru afungue mlango wa nyuma na aingie ndaniya gari.Huku akiwa na uoga mwingi,Flaviana akafungua mlango wa nyuma akaingia.Elibariki hakuwamo ndani ya gari
“ Elibariki yuko wapi? Akauliza Flaviana
“ Funga mlango” akaamuru yule jamaa.
“ Wewe ni nani? Elibariki yuko wapi? Akauliza Flaviana kwa wasiw asi
“ Fuata maelekezo uliyopewa.Hukuambiwa uniulize maswali ,kazi yangu ni kukupelekea mahala aliko mtu wako.Kama uko tayari hatuna muda wa kupoteza funga mlango wa gari na nikupeleke huko unakotaka,kama hauko tayari shuka” akasema yule jamaa kwa sautiya ukali.Flaviana akafikiri kidogo halafu akaufunga mlango japokuwa mwili ulikuwa unamtetemeka.Gari likawashwa na kuondoka pale kituoni
******
Ni usiku ulionekena kuwa mgumu sana kwa Dr Joshua.Pamoja na uchovu aliokuwa nao baada ya kufanyishwa kazi nzito na Peniela usiku ule lakini hakuwa na dalilizozote za kupata usingizi.Bado suala la Elibariki liliendelea kukisumbua sana kichwa chake. Alikuwa ameketi sofani chumbani kwake akiwa nasimu yake pembani akisubiri kuwasiliana na Dr Kigomba kuhusiana na zoezi lialoendelea la kumfuatilia Flaviana ili kufahamu mahala alikojificha jaji Elibariki.
“ Toka nimeingia madarakani sijawahi kuwekwa katika wakati mgumu namna hii na mtu yeyote yule zaidi ya Elibariki.Nilikosea sana kumuacha hai mpaka leo .Kama ningejua mapema kwamba Elibariki ana sumu kali zaidi ya nyoka ningek…………….” Alikatishwa mawazoyake na muito wa simu.Haraka haraka akabonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow Kigomba.Mambo yanakwendaje huko?
“ mambo yanakwenda vizuri,hadimuda huu hakuna tulichokigundua bado.Flaviana ameshuka katika gari lake na ameingia katika gari lingine na likaondoka.Nahisi humo ndimo alimo Elibariki.Tunaendelea kulifuatilia na nitakufahamisha kila kitu baada ya muda mfupi” akasema dr Kigomba
“ Kigomba tafadhali jitahidi kwa kila uwezavyo ili jambo hili limalizike.Sitaki kusikia kosa lolote.Hii ni nafasi ya dhahabu tumeipata na tuitumie vizuri” akasema Dr Joshua
“ usihofu mzee.Mimi mwenyewe nimeamua kuingia kazini na vijana leo ili kuhakikisha kwamba hakuna kosa litakalofanyika.Nitakutaarifu tena baadae kidogo kinachoendela” akasema Dr Kigomba na kukata simu
“ Nina hakika safari hii Elibariki hataweza kuponyoka. “akawaza Dr Joshua baada ya kumaliza kuongea na Dr Kigomba.Akamimina whysky katika glasi na kunywa funda kubwa. Mara akastuliwa na mlio wa simu.Zilikuwa ni namba ngeni kabisa katika simu yake na akajiuliza mtu yule ni nani na amezipata wapi namba zake? .Alisita kidogo kuipokea ile simu.Ikaita kwa mara ya kwanza hakuipokea,ikaita kwa mara ya pili akaamua kuipokea
“ hallow “ akasema
“ hallow Dr Joshua” ikasema sauti ya upande wa pili.Dr Joshua akaitambua sauti ile
“ hallow Deus ! akasema Dr Joshua huku uso wake ukiwa na tabasamu
“ hahaha nilidhani hautaweza kuitambua sauti yangu” akasema Deus
“ Siwezi hata siku moja kuisahau sauti yako mtu ambaye uliniachia kijitii.Poel sana nilisikia kwamba ulikuwa unasumbuliwa na miguu na nimepanga kuja kukuona kwa siku za hivi karibuni.Vipi hali yako kwa sasa?
“ Kwa sasa hali yangu inaendelea vizuri sana.Tayari nimekwisha pata tiba naninaendelea vizuri.Nilianguka na kustua mguu wakati nikiwa shambani kufuatilia maendeleo ya mifugo yangu.”
“ usijali Mr Presidnet nitakuja kukutembelea siku za hivi karibuni.Unajua kuna mambo mengiya kujifunza toka kwako kwa kuwa na mimi ninakaribia kumaliza muda wangu wa uongozi kwa hiyo natakiwa kujifunza toka kwenu mlionitangulia namna ya kuishi maisha ya kawaida baada ya kumaliza kuitumikia nchi” akasema Dr Joshua
“ Karibu sana Dr Joshua muda wowote ukiwa na nafasi” akasema Deus ambaye ni rais mstaafu na ndiye aliyemkabidhi ofisi Dr Joshua.Kimya kifupi kikapita halafu Dr Joshua akasema
“ Deus umenistua kidogo kwa simu yako ya usiku huu.” Akasema Dr Joshua
“ usiogope Dr Joshua,nimekupigia muda huu kwanza kukupa pole nyingi sana kwa kifo cha mkeo Dr Flora.Ninamfahamu vizuri Dr \Flora alikuwa na mahusiano mazuri sana na mke wangu kwa hiyo hata sisi tumeondokewa na rafiki muhimu sana wa familia yetu.Sikuweza kufika kwenye msiba lakini mke wangu alikuwepo na aliniwakilisha” akasema Deus
“ Deus nashukuru sana na ninamshukuru Mungu kwa kila jambo.Yeye ndiye mwenye kupanga kila itu kitokee.Ni vigumu sana kuikabili hali hii lakini ninajitahidi” akasema Dr Joshua.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Deus akasema
“ jambo la pili ambalo nimekupigia simu usiku huu ni kutaka tuongee kuhusiana na Package E21.” Akasema Deus na kumstua sana Dr Joshua.Alihisi kama kuna kitu kizito kimempiga kichwani.Kwa sekunde kadhaa akawa ni kama mtu aliyepigwa na butwaa.
“Dr Joshua !!..akaita Deus
“ Hal..hallow deus” akasema Dr Joshua lakini kwa mbali sauti yake ilionekana kutetemeka.
“ Joshua mbona umestuka namna hiyo?akauliza Deus
“ Deus kwa nini unataka tuongelee jambo hilo? Kwa nini leo? Akauliza Dr Joshua
“ Is it safe? Bado iko salama? Akauliza Deus
Dr Joshua akavuta pumzi defu na kuuliza
“ Deus niambie kwa nini unauliza kuhusu jambo hili?
“ Usiogope Joshua,nahitaji tu kujua kama Package E21 iko salama” akasema Deus
“ Kwani kuna tatizo gani Deus ? Akauliza Dr Joshua.
“ Ninataka tu kufahamu kama bado ipo na iko salama” akasema Deus.Dr Joshua akakaa kimya kwa sekunde kadhaa na kusema
“ Deus naomba unieleze kwa nini umenipgia simu? Unataka nini?Ninakufahamu vizurilazima kuna sababu iliyokufanya ukanipigia simu “ Akasema Dr Joshua
“ Dr Joshua kuna ubaya gani kujua kama package iko salama? Mimi nilikabidhiwa na nikaitunza kwa miaka yangu yote kumi halafu nikakukabidhi wewe nikiaminikwamba itaendelea kuwa salama kwa hiyo ni jukumu langu kufahamu kama bado iko salama” akasema Deus na maneno yale yakaonekana kumchukiza Dr Joshua
“ Deus ninakuheshimu mno na ninataka nikueleze jambo moja,wakati wa uongozi wako hakuna aliyekuwa akikuingilia katika kila ulichokifanya.Kwa sasa umekwisha maliza uongozi wako na una pumzika kwa hiyo naomba uendelee kupumzika.Masuala ya Package E21 hayakuhusu tena.Hili ni jukumu langu kwa hiyo naomba usiingilie kazi zangu” akasemaDr Joshua
“ Dr Joshua,siwezi kuacha kufuatilia kuhusu kitumuhimu kama hiki.Wakati wa uongozi wangu niliilinda kama mboniya jicho langu tofauti na wewe unavyotaka kufanya” akasema deus na kumstua sana Dr Joshua.Uso wake ukakunja ndita.
“ Umesema nini Deus? Akauliza Dr Joshau kwa ukali
“ Joshua ninafahamu kila kitu unachotaka kukifanya”
“ Mbona sikuelewi unamaanisha nini? Akauliza Dr Joshua
“ Joshua ninafahamu kuhusu biashara unayotaka kuifanya “
“Biashara gani?
“ Usijifanye haufahamu Joshua.Usisahahu kwamba hata mimi nilikuwa katika nafasi kama yako na ninauwezo wa kufahamu kila kinachoendelea katika uongozi wako.I have lots of connections Joshua” akasema Deus.Dr Joshua akahisi joto kali na kijasho kikaanza kumchuruzika.Alihisi kusikia kizungu zungu.
“ Joshua are you there? Akauliza Deus baada ua Dr Joshua kuwa kimya
“ Unasemaje Deus?
“ Joshua ninarudiaa tena kukukumbusha kwamba ninaifahamu biashara unayoifanya na ninafahamu unataka kuwauzia akina nani.”akasema Deus
“ Kwa hiyo baada ya kugundua hivyo ni kitu gani unakihitaji? Akauliza Dr Joshua kwa ukali
“ I want you to stop that business as soon as possible.” Akasema Deus kwa ukali
“ Dr Joshua sikuwahi kufikiria kwamba mtu kama wewe unaweza ukafanya kitu hatari kama hiki kwa taifa.Nilikukabidhi package ile nikiamini kwamba utaitunza na kuilinda kama mboniya jicho lako lakini umeingiwa na tamaa ya fedha na unataka kuhatarisha usalama wa taifa.Joshua please don’t do it.Usifanye kabisa jambo hatari kama hilo.Usiitoe ile package mahala ilipo.Pale iko sehemu salama na itaendelea kukaa pale kwa miaka yote.Ni kwa sababu ya unyeti wake ndiyo maana inahifadhiwa ikulu sehemu ambayo anayefahamu ilipo ni rais wa nchi pekee kwa hiyo Joshua narudia tena kukusisitiza kwamba usifanye hicho kitu unachotaka kukifanya.” Akasema Deus kwa ukali
“ who are you Deus to give me orders? Wewe huna mamlaka yoyote kwa sasa ya kuniamuru mimi jambo lolote!!akafoka Dr Joshua
“ Joshua naomba usisahau kwamba I’m a president too..”akasema Deus
“ Ex president. !! akasema kwa ukali Dr Joshua.
“ hauko tena katika uongozi kwa hiyo kwa sasa huna nguvu yoyote ya kuweza kuniamuru chochote” akaendelea kusema kwa ukali Dr Joshua
“ Kitu gani kinakufanya uwe na uhakika huo kwamba siwezi kukuamuru kitu? Umesahau kwamba mimi ndiye niliyekuteua na kukupigania hadi ukashika nafasi hiyo? Kama nilikuwa na nguvu ya kukuweka hapo ulipo ,unadhani sintakuwa na nguvu ya kukuondoa hapo ulipo ? Akauliza Deus
“ Usinitishe huna lolote Deus.I am a president of United republic of Tanzania and you are just a normal citizen so don’t you ever try to interfere anything in my administration ! Wananchi ndio walioniweka hapa na wala si wewe kwa hiyo usinitshe na huwezi kunifanya chochote na tena ninakuonya kwamba usithubutu tena kunipigia simu na kunitolea vitisho. Mimi ni rais na nina uhuru wa kufanya jambo lolote .Package hii haihusiani na raia yeyote wan nchi hii na kuiuza sijavunja sheria wala katiba ya nchi” akasema Dr Joshua kwa ukali huku jasho likimtiririka.
“ Joshua unapata kila kitu unachokihitaji katika maisha yako,na ukimaliza muda wako wa kulitumikia taifa utaishi kwa raha mustarehe na kwa heshima nyingi.Umekwisha fanya mambo mengi mazuri katika nchi hii na watanzania wataendelea kukukumbuka kwa miaka mingi ijayo kwa mambo uliyowafanyia.Tafadhali usiingiwe na tamaa na ukaharibu yale mazuri yote uliyoyafanya kwa sababu tu ya hayo mabilioni ya fedha unayotarajia kuvuna baada ya kuiuza Package E21.” Akasema Deus
“ Deus naomba usitafute ugomvi kati yangu na wewe kwa sababu unaelewa kwamba huwezi kunishinda hata kidogo.” Akasema Dr Joshua
“ Joshua hii ninakupa amri nasi ombi.Nikisikia kwamba unaendelea na biashara hii unayotaka kuifanya basi jiandae kuondoka katika hicho kiti.Siko tayari kuona ukihatarisha usalama wa nchi yetu kwa tamaa zako.Siko tayari kuona maisha ya mamilioni ya watu yakiwa hatarini kwa tamaa zako.Nitakudhibiti kabla hujafanya unavyotaka kufanya and I will take you down Joshua.Kwa heri kwa sasa” akasema Deus na kukata simu.Zilipita kama dakika mbili Dr Joshua bado alikuwa amesimama akiwa na simu yake mkononi.
“ Huyu shetani katokea wapi tena? Aggghhh!!.. kabla hili halijaisha linaibuka hili.” Akajiuliza Dr Joshua na kumimina mvinyo katika glasi akaugugumia wote .
“ Deus amefahamuje kuhusu mpango huu? Akaendelea kujiuliza akamimina tena mvinyo katika glasi
“ Tunaojua kuhusu siri hii ni watu watatu ,mimi,Kigomba na Amos ,ni nani basi kati yetu ambaye atakuwa amempa taarifa Deus? Lazima ni mmoja kati yetu .Nina ni kati ya Kigomba na Amos? Akajiuliza
“ Akili yangu inanituma kwa Amos.Imani inaanza kunitoka kwake.Nahisi ni yeye ambaye anaweza kuwa akitoa habari zetu.Dr Kigomba sina shida naye ni mtu ambaye nimekwisha fanya naye mambo mengi makubwa na ya hatari na hakuna hata siku moja nimewahi kusikia jambo lolote nililofanya naye limevuja.Baada ya kumshirikisha captain Amos mambo ndiyo yameanza kwenda kombo.Nitamfanyia uchunguzi wa kina Amos na kuzifahamu nyendo zake.Nitaweka vijana wa kumfuatilia katika kila jambo analolifanya na ukweli utajulikana tu.Nikifahamu kwamba ni yeye ndiye anayetoa habari zetu basi sintakuwa na huruma naye,nitamzimisha kimya kimya “ akawaza Dr Joshua
“ Deus Amasile Mkozumi ..” akatamka Dr Joshua kwa sauti ndogo
“ Deus ni mtu ninayemuheshimu sana .Ni mtu ambaye wakati wa uongozi wake alifanya mamabo mengi makubwa kwa nchi hii na heshima yake ni kubwa sana .Kwa msaada wake nilifanikiwa kukipata kiti hiki cha urais.Pamoja na mambo yote aliyonifanyia lakini kwa hiki anachotaka kukifanya amepotea njia.Nitaweka kila kitu pembeni na nitapambana naye.Ninamfahamu vizuri Deus ni mtu ambaye akisema jambo hulitimiza.Kama ameahidi kunitoa katika kiti hiki basi atafanya hivyo.Ni mtu ambaye bado ana ushawishi mkubwa sana na anaweza akawashawishi wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani na rais na wakaniondoa madarakani.Ni mtu ambaye sipaswi kumpuuza hata kidogo.Nguvu yake katika siasa bado ni kubwa .Kwa maneno aliyoongea japokuwa nilikuwa nikibishana naye lakini yameniogopesha sana.Natakiwa kuchukua hatua haraka sana na kumaliza Deus kabla hajanimaliza.Mimi ni rais wa nchi na nina kila nyenzo ya kuweza kummaliza Deus na wale wote anaoshirikiana nao.Baada ya Elibariki nimepata adui wa pili.Lazima niwamalize wote haraka sana.Nimekaribia mwisho kabisa wa biashara hii kwa hiyo lazima nihakikishe kwamba ninawaondoa wote haraka iwezekanavyo.” Akawaza Dr Joshua na kuchukua simu yake akabonyeza namba Fulani halafu akaiweka simu sikioni
“ General Adam,tafadhali naomba nikuone hapa ikulu usiku huu.” Akasema Dr Joshua na kukata simu
“ I will destroy you Deus,I must destroy you!!! Akasema Dr Joshua kwa hasira na kunywa mvinyo kwa fujo.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………