Mawaiba
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 417
- 151
Habari za week end wana jamvi...
Tafadhali naomba maelezo ya kina toka kwa mtu yeyote mwenye utambuzi wa kitaalamu kuhusu tatizo la kiafya linalojulikana kitaalamu kama Foot Drop. Nimefikia uamuzi wa kuuliza toka kwenu kwa sababu itokanayo namaelezo yafuatayo:-
Kijana wangu wakiume, umri wake ni miaka 24, alipata ajali ya kuanguka na pikipiki yapata wiki nne zilizopita. Ingawa hakupata mjeraha yaliyopelekea kutokwa na damu sehemu yoyote ya mwili wake, lakini baada ya kukutana nae jana niligundua kwamba hali aliyonayo ilikuwa inahitaji msaada wa kitaalamu.
Kifupi ni kwamba alipopata hiyo ajali alikuwa anaishi eneo ambalo hakuna madaktari waliokuwa na uwezo wa kung'amua tatizo alilolipata kutokana na tukio hilo. Baada ya kurudi nyumbani, na mimi kugundua kwamba ana tatizo lisilo la kawaida niliandaa mazingira ya kumkutanisha na daktari ambaye baada ya kupata maelezo ya mgonjwa aliniambia kijana wangu ana tatizo linalojulikana kama foot drop, ambapo baada ya kufanyia matibabu ya viungo kwa hatua ya awali na kumpa maelekezo ya jinsi anavyotakiwa uendelea na matibabu hayo kwa siku za baadae pia alimuandikia atumie dawa ili atumie.
Baada ya kuambiwa kwamba kijana wangu ana tatizo hilo la foot drop, nilitaji kutafuta taarifa za ziada kuhusu tatizo hili, na baada ya kwenda kwenye Google nikakutana na maelezo yaliyokuwa ni kisayansi zaidi kiasi kwamba nilishindwa kupata majibu juu ya kile nilichotaka kukijua, ambayo ni haya;-
1)Kwamba Foot Drop inaweza kuwa permanent au temporary. Kwahiyo nikataka kujua kama hili tatizo la kijana wangu lipo katika category gani?
2)Kwamba kutokana na upeo wangu mdogo wa kibaiolojia nilikuwa najua kwamba nerve damage huwa haiwezi kuwa recovered.
Kwa maana hii wana Jf, ninaimani hili nijukwaa la wataalamu, naomba mnijuze khs hatma ya mguu wa kijana wangu kwamba je, ni ulemavu wa kudumu au anaweza kurudi katika hali yake ya kawaida?
Tafadhali naomba maelezo ya kina toka kwa mtu yeyote mwenye utambuzi wa kitaalamu kuhusu tatizo la kiafya linalojulikana kitaalamu kama Foot Drop. Nimefikia uamuzi wa kuuliza toka kwenu kwa sababu itokanayo namaelezo yafuatayo:-
Kijana wangu wakiume, umri wake ni miaka 24, alipata ajali ya kuanguka na pikipiki yapata wiki nne zilizopita. Ingawa hakupata mjeraha yaliyopelekea kutokwa na damu sehemu yoyote ya mwili wake, lakini baada ya kukutana nae jana niligundua kwamba hali aliyonayo ilikuwa inahitaji msaada wa kitaalamu.
Kifupi ni kwamba alipopata hiyo ajali alikuwa anaishi eneo ambalo hakuna madaktari waliokuwa na uwezo wa kung'amua tatizo alilolipata kutokana na tukio hilo. Baada ya kurudi nyumbani, na mimi kugundua kwamba ana tatizo lisilo la kawaida niliandaa mazingira ya kumkutanisha na daktari ambaye baada ya kupata maelezo ya mgonjwa aliniambia kijana wangu ana tatizo linalojulikana kama foot drop, ambapo baada ya kufanyia matibabu ya viungo kwa hatua ya awali na kumpa maelekezo ya jinsi anavyotakiwa uendelea na matibabu hayo kwa siku za baadae pia alimuandikia atumie dawa ili atumie.
Baada ya kuambiwa kwamba kijana wangu ana tatizo hilo la foot drop, nilitaji kutafuta taarifa za ziada kuhusu tatizo hili, na baada ya kwenda kwenye Google nikakutana na maelezo yaliyokuwa ni kisayansi zaidi kiasi kwamba nilishindwa kupata majibu juu ya kile nilichotaka kukijua, ambayo ni haya;-
1)Kwamba Foot Drop inaweza kuwa permanent au temporary. Kwahiyo nikataka kujua kama hili tatizo la kijana wangu lipo katika category gani?
2)Kwamba kutokana na upeo wangu mdogo wa kibaiolojia nilikuwa najua kwamba nerve damage huwa haiwezi kuwa recovered.
Kwa maana hii wana Jf, ninaimani hili nijukwaa la wataalamu, naomba mnijuze khs hatma ya mguu wa kijana wangu kwamba je, ni ulemavu wa kudumu au anaweza kurudi katika hali yake ya kawaida?