Pesa inataka nini?

Pesa inataka nini?

KENZY

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
32,529
Reaction score
76,691
Nimekuwa nikiamini ktk mafunzo ya aina mbili hapa duniani..
Moja ni kufunzwa na watu/mtu.
Na pili ni kufunzwa na dunia/mazingira.

Ni vyema kuutumia uwepo wetu wa ufahamu ktk kujifunza,kuelimika na kutenda.
Sio kwamba naifahamu pesa kiundani sana!,la hasha!.. ila nimeikuta lkn pia kuikuta haimaanishi nisiijue!.

Pesa tunaitafuta ili tutatue vinavyoweza kutatulika na pesa.
Lkn je, ulishawahi jiuliza pesa inataka nini?

Nimeshashuhudia watu wakiwa na pesa na tena kurudi chini Kama alivyokuwa jana!..
Hata wewe unaesoma hapa unaweza ukawa shuhuda wa wewe mwenyewe au mtu mwengine!.
Tunaweza kuteleza mara moja au mbili na tukainuka jumla ila sio wote wanaoweza kuinuka!..

Pesa inataka kile ambacho haukukijua wakati unaanguka!!.

Kuwa na pesa kunahitaji uwe na elimu juu ya pesa ili uweze kuimudu pesa hiyo!.. Ni sawa na kusema uwe na pikipiki wakati hujui kuiendesha hapo kaa ukijua utaanguka tu!!..
Pesa inahitaji elimu ambayo itakufanya ujue kwanini pesa..?
Kwanini utumie pesa..?
Kwanini utafute pesa..? Na swala la msingi zaidi ni kivipi utaitumiaje pesa kupata pesa..?
Hapa wengi tunaanguka!..
Labda nitoe mfano huu ili nieleweke vyema.. mtu unasomea ualimu but ukimaliza unakuta ajira huku mtaani hola!.

Unapambana unafanya vitu vyako unajichanga then unaanzisha biashara but huna elimu ya biashara!.. kaa ukijua huko ni sawa na kubeti na kwenye kubeti huwa kunamatokeo mawili.

Pesa inahitaji taarifa sahihi..
Ili uweze kuimudu pesa yako ktk kukuletea pesa ni lazima uwe na taarifa sahihi ilikusudi uweze kufanya maamuzi sahihi..

Ukitaka kufanya biashara kaa ukijua sio mtaji tu ndo utakuletea faida au mfanyakazi mzuri ama huduma nzuri n.k hayo sio pekee tu!.. taarifa ya nini kinahitajika,muda gani,mahali gani na kivipi huo ndio msingi wa kwanza utakaoweza kukuletea pesa kwenye pesa.

Pesa inahitaji nidhamu..
Ulishawahi kuona mtu fulani akipata fedha anabadilika..?
Huyo anaweza kuwa ni wewe au Yule ama Mimi!!
Ndio pesa hubadili tabia ya mtu hata kwa nusu saa tu!.. kutokuwa na nidhamu ya fedha ndipo hufanya kujiuliza kuwa pesa hii imeishaje??!
Pesa inahitaji nidhamu ya aina yake haswa kwenye utulivu wa akili,hupaswi kuwa mwenye pupa katika utumiaji wa fedha kwa maana fedha inahitaji swali kwanini kwa mtumiaji makini.. ila inahitaji upumbavu kidogo tu ili ikupeperuke!.
Ipo hivi Kama utaendelea kureact tabia zilezile za matumizi mabovu jua kamwe hautabadili chochote.

Pesa inahitaji uvumilivi..
Uvumilivi kwa maana nyengine ni muda.. na sio muda tu bali muda muafaka na sahihi!..
Wengi wao tumekuwa tukishindwa kuwa wavumilivu haswa pale tunapopata miburungutu.. sometimes pesa inahitaji kutunzwa tu ama kuwekezwa huku ikisubiri muda muafaka na sahihi ili ije iungane na taarifa sahihi zenye nidhamu, uvumilivi ili iweze kuja kuleta pesa nyenzake..

Naomba niishie hapo.. mengine tutaelewashana kadri mjadala unavyoenenda..
 
Masomo yote yanayohusu fedha yanayofundishwa mavyuoni na ukumbini na nyie MA motivation speakers ni fake. Kila tajiri ana siri yake ambayo hatamwambia mtu mpaka anaingia kaburini
Unaweza ukawa kweli lkn usiwe mkweli mwenye usahihi maana sometimes sio elimu ndo inakuwa pungufu bali mtu ndo anakuwa pungufu mbele ya elimu!.
 
Hivi hizo siri mnazosemea huwa mnamaanisha nini?
Dili chafu au shirki?
Yale anayoyasema tajiri mbele ya umma kumotivate watu ni unafiki tu. Siri anayo mfukoni.

Ni sawa na kiongozi aliyesoma kwa kuungaunga na kupiga chabo mpaka anamaliza University anapotembelea shuleni kwenu lazima atawaambia msome kwa bidii
 
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.

Mhubiri 9:11
 
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.

Mhubiri 9:11
Imebidi nirudi kwenye biblia kutizama huu mstarii...[emoji122][emoji122]
 
Imebidi nirudi kwenye biblia kutizama huu mstarii...[emoji122][emoji122]

Kuna toleo la kiingereza limeelezea vizuri zaidi, nilipenda maelezo yake.

NLT
I have observed something else under the sun. The fastest runner doesn’t always win the race, and the strongest warrior doesn’t always win the battle. The wise sometimes go hungry, and the skillful are not necessarily wealthy.

And those who are educated don’t always lead successful lives. It is all decided by chance, by being in the right place at the right time.
 
Yale anayoyasema tajiri mbele ya umma kumotivate watu ni unafiki tu. Siri anayo mfukoni.
Ni sawa na kiongozi aliyesoma kwa kuungaunga na kupiga chabo mpaka anamaliza University anapotembelea shuleni kwenu lazima atawaambia msome kwa bidii
Sawa...! Nadhan ni sawa mtoto anayeongoza darasani akae na mambumbu .lazima aact umbumbu..maana hata akisema someni watu watamwambia wewe kila siku unafaulu usituchoshe
 
Kuna toleo la kiingereza limeelezea vizuri zaidi, nilipenda maelezo yake.

NLT
I have observed something else under the sun. The fastest runner doesn’t always win the race, and the strongest warrior doesn’t always win the battle. The wise sometimes go hungry, and the skillful are not necessarily wealthy. And those who are educated don’t always lead successful lives. It is all decided by chance, by being in the right place at the right time.
Ni kweli maelezo yapo vizuri....Kiujumla mie nimependa huo mstari wa mhubiri.
 
Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.

Mhubiri 9:11

Dah kumbe ata kwenye bible ipo hii..... Better to be born lucky than gifted

Bora uzaliwe mwenye bahati kuliko mwenye kipaji
 
🤔🤔Kwamba mambo haya yanakwenda sambamba na bahati.?

Tatizo lugha rafiki lugha, sasa sie tuliekimbia umande changamoto zinakua maradufu.
Najaribu kutafakari
1. Being at the right place.
2. At the right time

Nikajikuta nakumbuka ule usemi unapishana na gari la mshahara.
Yaani kila ukisikia jambo unakuta limeshapita muda au halina umuhimu tena, wakati mwenzako anapata hizo taarifawakati muafaka na kuzifanyia kazi zinamnufaisha.

Hapa swali linakuja, nini kifanyike kukufanya uwe at the right place at the right time? Je, inaathiriwa na marafiki au watu wanaokuzunguka? Ratiba zako na unavyopangilia mambo yako vina mchango kwenye hilo? Ndio tunarudi pale pale kwenye usemi wako, au ni bahati tu?
 
Tatizo lugha rafiki lugha, sasa sie tuliekimbia umande changamoto zinakua maradufu.
Najaribu kutafakari
1. Being at the right place.
2. At the right time

Nikajikuta nakumbuka ule usemi unapishana na gari la mshahara.
Yaani kila ukisikia jambo unakuta limeshapita muda au halina umuhimu tena, wakati mwenzako anapata hizo taarifawakati muafaka na kuzifanyia kazi zinamnufaisha.

Hapa swali linakuja, nini kifanyike kukufanya uwe at the right place at the right time? Je, inaathiriwa na marafiki au watu wanaokuzunguka? Ratiba zako na unavyopangilia mambo yako vina mchango kwenye hilo? Ndio tunarudi pale pale kwenye usemi wako, au ni bahati tu?
Ni sahihi kabisa wanaotuzunguka na vile tunavyovifanya kila siku vina mchango mkubwa katika maisha huku vikichagizwa na juhudi binafsi za uitafutaji....lakini bahati nayo haichezi mbali
 
Hapo ulipo wakati huu unaona kama uko eneo muafaka kwa muda sahihi..?
Swali zuri mkuu, ndio maana Dr. Dispenza anasisitiza maisha ya present-future reality, the best way to predict our future is to create them and to live in present, hivyo tunaweza kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kubahatisha bahati zetu, otherwise tunaweza ishia kwenye rat race.
 
Back
Top Bottom