Pete Hegseth, Waziri wa Ulinzi mteule Marekani asema anaunga mkono Israel kuwaangamiza na kuwaua kila mwanachama wa Hamas aliyesalia hai

Jamaa ameongea kama mlevi, Afghanistan wamekaa almost 20yrs lakini wameondoka na Taliban wamerudi wanaendelea kuendesha maisha yao. Sasa wamefaidika na kipi?
Kwamba wamalize migogoro ya mashariki ya kati wahamie China.... China wataiweza?
Na ni mlevi balaa😀
 
Maneno mengi huwa ni kama ule upepo usio dhuru 😄 🤣 mwenzenu Shetanyahu kakubali masharti ya Hamas we baki na huyo kichaa wako kasema kasema.

⭕️ Hii hapa ni rasimu ya makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza kulingana na vyombo mbalimbali vya habari:

Awamu ya 1 (siku 42):

1. Kusimamishwa kwa muda kwa shughuli za kijeshi na kujiondoa kwa Israeli kutoka kwa maeneo yote yenye wakazi.

2. Kusimamishwa kwa muda kwa shughuli za hewa kwa saa kumi kila siku.

3. Kurudishwa kwa watu waliohamishwa kwenye maeneo yao ya makazi.

Siku ya 7: Waisraeli wanajiondoa kutoka Mtaa wa Al-Rasheed hadi Mtaa wa Salah Al-Din, kubomolewa kwa mitambo ya Israeli na kuwarudisha watu waliohamishwa makazi yao.

Siku ya 28: Waisraeli wajiondoe kutoka Gaza ya kati, kuruhusu watu kusafiri bila malipo.

• Uwasilishaji wa vifaa vya msaada, mafuta na kuondoa vifusi, sambamba na kufunguliwa kwa hospitali na mikate kote Gaza.

* 4. Kubadilishana mateka:

Awamu ya 1: Hamas itawaachilia mateka 33, huku Israel ikiachilia wanawake na watoto wa Kipalestina 30 kwa kila mateka aliyeachiliwa huru, ili wazuiliwe.

• Hamas kisha itawaachilia wanajeshi wote wa kike wa Israel walio hai, huku Israel ikiwaachilia wafungwa 50 wa Kipalestina kwa kila mmoja.

5. Ratiba ya kubadilishana wafungwa:

Siku ya 1: Hamas inawaachilia mateka watatu wa raia.

Siku ya 7: Hamas huwaachilia mateka wanne raia, wakifuatiwa na mateka watatu wa Israeli kila wiki.

Wiki ya 6: Hamas inawaachilia wafungwa wote waliosalia wa Israel walio chini ya awamu hii kwa kubadilishana na wafungwa wa Kipalestina kulingana na orodha iliyoandaliwa na Hamas.

• Israel itawaachilia wafungwa 47 waliozuiliwa baada ya makubaliano ya Shalit na raia wote walio chini ya umri wa miaka 19 waliokamatwa huko Gaza baada ya Oktoba 7.

• Wafungwa wa Kipalestina wataachiliwa bila masharti, na hakuna kukamatwa tena siku zijazo.

6. Awamu ya kwanza ya kubadilishana mateka ni tofauti na awamu ya pili.

7. Mazungumzo ya awamu ya pili yataanza kabla ya Siku ya 16.

8. Umoja wa Mataifa utaendelea kutoa misaada.

9. Miundombinu
ukarabati utaanza.

10. Angalau nyumba 60,000 na mahema 200,000 yatatolewa kwa wale waliopoteza makazi yao.

11. Kuongeza idadi ya watu waliojeruhiwa wanaosafirishwa kwa matibabu kwa njia ya kivuko cha Rafah na kuruhusu harakati za biashara.

12. Ujenzi mpya na fidia kwa raia utaanza chini ya usimamizi wa mashirika na nchi, zikiwemo Misri na Qatar.

13. Katika awamu hii, uondoaji na usitishaji wa shughuli za kijeshi utaendelea, pamoja na mazungumzo ya awamu ya pili.

14. Usitishaji wa kudumu wa mapigano utatangazwa, na Israel itajiondoa kikamilifu kutoka Gaza.

Awamu ya 2 (siku 42):

15. Kubadilishana miili baada ya kuwatambua marehemu.

16. Kujengwa upya kwa Gaza (miaka 3-5) chini ya usimamizi wa kimataifa na Umoja wa Mataifa, ikiwa ni pamoja na Qatar na Misri.

17. Ufunguzi wa vivuko kwa watu binafsi na bidhaa.

Wadhamini wa makubaliano hayo ni Qatar, Misri na Marekani.
 
Huwawei ilikufa chini ya Trump. Tutegemeee mengi kwa muhuni wetu Trump kwa kipindi hiki cha miaka 4 mingine
Hivi unaelewa ulichoandika?
Unafikiri Huawei ni kampuni ya kutengeneza simu pekee, huawei wapo kwenye telecom, cloud technology, AI, magari, wanatengeneza computers n.k, wanafanya mambo mengi sana, so usifikiri kuzuiliwa playstore na sanctions baadhi itawazuia kusonga mbele kwenye mambo mengine...

Trump hana jipya anatapatapa kama kuku inayotaka kuchinjwa...
 
🙏🙏🙏🙏👏👏👏👏👏🙏🙏🙏🙏
 
Ila hili suala linafikirisha sana, ina maana hao wafungwa katika kipindi cha muda wote walikuwa pale pale Gaza?
IDF na intel yake,technology, satellite na jeshi la ardhi na anga ,,msaada wa EU na US wa silaha na fedha na bado wakashindwa kufahamu walipo? aa walifahamu lakini wakashindwa kufika sababu ya mashambulizi?

Hao mateka kwa jinsi Gaza ilivyo ndogo, Gaza ni ndogo sana, Hamas waliwaficha wapi?

Hamas ni makomando na wana uwezo wa kupambana kuliko IDF, naweza kusema hivyo...
 
Leo Blinken kakiri Hamasi hakuna anaye weza kumshinda vita, afu vijana wa Heleluya wanaimba kwaya eti Israel kashinda vita, sikatai kashinda kwa kuvunja majumba na kauwa watoto na wanawake tu, sio wanamgambo wa Hamasi. Israel lazima atumie siasa ili kuishi salama na Hamasi sio vita.


View: https://youtu.be/BJZXp58djQs?si=bnegXYn1Inbhc3Jl
 
Tatizo bado mnazungumzia unipolarity jambo ambalo kwa sasa haliwezekani na US inajitahidi sana kurudi huko lakini haiwezekani..

Wakati wa USSR utambue ilikuwa ni bipolar, balance of power, huku US kule USSR, cha ajabu ni kwamba China leo inaizidi USSR at its peak, kama USSR ilikuwa superpower kipindi hiko basi tambua leo China ni superpower pia... USSR haikuwahi kufika ilipofikia China leo.

Bado sijaelewa lakini nchi kuwa superpower unaangalia vigezo gani...
 
Ni ukweli mchungu..
Kwa kweli inashangaza, kinachonishangaza uduni wa silaha walizonazo...
 
Bado sijaelewa lakini nchi kuwa superpower unaangalia vigezo gani...
Nchi kuitwa "superpower" ni kutokana na uwezo wake mkubwa wa kiuchumi, kijeshi, kisiasa, na kiutamaduni duniani. Vigezo muhimu vinavyozingatiwa ni:


1. Nguvu ya Kijeshi:


  • Uwepo wa jeshi lenye nguvu, teknolojia ya hali ya juu, na uwezo wa kuendesha operesheni za kijeshi duniani kote.
  • Uwepo wa silaha za nyuklia au uwezo wa kuzimiliki.
  • Uwezo wa kujilinda na kushiriki katika masuala ya kimataifa ya kiusalama.

2. Nguvu ya Kiuchumi:


  • Pato la Taifa (GDP) kubwa na soko thabiti la kifedha.
  • Ushawishi wa kiuchumi duniani, ikiwa ni pamoja na uwezo wa kudhibiti masoko ya kimataifa na biashara ya kimataifa.
  • Maendeleo ya kiteknolojia na uzalishaji wa viwanda vinavyoongoza kimataifa.

3. Nguvu ya Kisiasa:


  • Ushawishi mkubwa katika taasisi za kimataifa kama Umoja wa Mataifa, IMF, na WTO.
  • Uwezo wa kushawishi sera za kimataifa na kushiriki katika kutatua migogoro ya kidunia.

4. Nguvu ya Kiutamaduni:


  • Uenezaji wa lugha, tamaduni, na vyombo vya habari vinavyoathiri dunia nzima.
  • Ushawishi wa maadili, mitindo, burudani, na elimu katika mataifa mengine.

5. Uwezo wa Kiustadi na Kiteknolojia:


  • Uwezo wa kuendeleza na kutumia teknolojia za hali ya juu.
  • Nchi inayoongoza katika uvumbuzi wa kisayansi na utafiti.

Mfano wa nchi zinazotambulika kama "superpower" ni Marekani, huku China na Urusi zikionekana kuimarisha nafasi zao katika kuwania hadhi hiyo.

Chanzo : (Chatgpt)
 
Jamaa ameongea kama mlevi, Afghanistan wamekaa almost 20yrs lakini wameondoka na Taliban wamerudi wanaendelea kuendesha maisha yao. Sasa wamefaidika na kipi?
Kwamba wamalize migogoro ya mashariki ya kati wahamie China.... China wataiweza?
Taliban alifanya Mikataba na USA mzee
 
Kiongozi katika hayo yote uliyotaja, China kwenye utamaduni tu ndipo anatolewa kwingine kooote China yupo vizuri...
Kwa hilo CHina ni superpower...

Utamaduni wa magharibi wenyewe ndio huo kujumuisha na ushoga, kusagana na ushenzi mwingine.
Na huwezi kusema China si superpower kisa kazidiwa utamaduni, naelewa utamaduni wa magharibi unauza zaidi duniani... na si kuanza jana au juzi, hata USSR haukuwahi kuifikia US katika utamaduni lakini ilikuwa superpower...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…