Petition: Tanzania should host CAN 2020!

Guys! Open ur eyes, dont u c what we will benefit 4m staging such a tournament?
Hahahahaha...

Simple!

We will qualify automatically! We wont have to sweat to qualify 4 th thing we have been fighting 4 a decade or two.
Plus we will talk to referees pembeni to favor us to @ least the semi-final stage.

U get ma point, pple?!
 
Let us decide between CAN 2020 na kujenga shule badala ya shule ya namna hii

au kuwa na hospitali ya namna hii


 
Asante Zed...saa ingine nadhani watu huwaga wanasahau jinsi tulivyo na matatizo hususan wakiwa ughaibuni na vi laptop vyao.
 
Let us decide between CAN 2020 na kujenga shule badala ya shule ya namna hii

au kuwa na hospitali ya namna hii



Mkuu huu mfano mzuri sana lakini kama Tanzania itaandaa hiyo CAN 2020 itasaidia kupunguza hayo kwa kuepuka Aibu
kwani priority kwa muda mrefu ilikuwa kununua 4 wheel kama solution ya barabara mbovu
Baada ya mashindano hata hivy vitanda vitaongezwa kwenye mahospitali kwani market after competition will not sustain same capacity
Hii nadhani ni cleaver twist kwa viongozi wetu kufanya kazi kuepuka aibu
 
I am suprised kuwa Kiranga na OPP and even Mzee Mwanakijiji to some extent bado wanatumaini na mipango ya Mkukuta kuwa tutajenga shule na kuchonga madawati ili watoto wasikalie vitofa!

Labda niulize, kwa kumchunguza kwenu Mtanzania, leo simba na Yanga wakicheza, hata kiingilio kikiwekwa kuwa Shilingi Laki Moja, Uwanja utajaa, watu watachacharika kuitafuta hiyo Laki Moja na kwenda kuangalia mpira.

Leo akishuka Kofi Olomide au Beyonce kufanya onyesho na kiingilio kikawa Shilingi laki Mbili, watu watachacharika na kuzitafut hizo shilingi laki mbili, watabeba zege, kuzoa mavi na mengine mengi alimradi wapate nafasi ya kwenda kuburudika.

Leo hii ukiwaambia tusafishe mitaa na kujenga upya sehemu ili Denzel Washington au Wayne Rooney waje kukaa mwezi mmoja, tutajikusanya kwa dhati kuimarisha nguvu na kufanya kazi kwa bidii na ufanisi wa hali ya juu ili kutoa mandhari mazuri ya kuwa wakarimu!

Jiulizeni inakuwaje ni rahisi kwa watu kuchangia Harusi, Ubatizo, Kipaimara, Jando, Unyago, Mkole lakini inapofika kuchangia kununua madawati, tunakuwa wagumu na wakali kuchangia?

Nikirudi kwenye hoja na kumjibu Mzee Mwanakijiji kwenye swali lake la Walilotuashia Wakoloni, naamini kuwa Tanzania ya sasa tunakwenda kwa mabadiliko. Kama agenda ya mwaka huu kwetu ni change, basi hata michezo ikiisha na tukaachiwa reli, umeme na miundombinu yetu, tutaweza kuamka upya na kuendeleza nchi kwa kutumia miundo mbinu tuliyojijengea ili kufanikisha michezo hii ambayo kwa mipango ya kawaida tumekuwa tukifanya kigugumizi kuifanikisha!
 
Tyuti,

Hakutakuwa na Tanzania wakati huo, kwa vile itakuwa kijijimbo cha Jamhuri ya EAC.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…