Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Chama cha Demokrasia na Maendelea kimefanya uchaguzi wa kumpata Mwenyekiti wa Chama Taifa, licha ya chaguzi zingine kufanyika ndani ya Chama ila mafahari hawa wawili walitikisa anga la Siasa ndani na nje ya Tanzania kutokana na uswawishi wao mkubwa Kisiasa.
Soma, Pia: Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA 2025: Tundu Lissu ashinda nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa kwa Kura 513 sawa na 51.5%
Mnyukano wao kwenye mitandao ya kijamii na hata kwenye mahojiano na vyombo mbalimbali vya habari ilizua hisia kwamba huwenda hata wakikutana uso kwa uso basi wangezichapa ama kutoongea kabisa ila mambo hayakuwa hivyo na kuonesha somo kubwa la demokrasia.
Hapa nimekukusanyia baadhi ya matukio ya picha za kukumbukwa katika uchaguzi huu wa kihistoria katika chama chao;
1. Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwa mara ya kwanza kwenye Kikao cha Kamati Kuu Chadema, makuu ya chama hicho, Mikocheni Dar es Salaam, Ijumaa, Januari 10, 2025.
2. Tundu Lissu na Freeman Mbowe, wakicheza pamoja kwa bashasha wimbo wa "Tuvushe Mbowe Tuvusheee" kwenye Mkutano Mkuu Bawacha Taifa
3. Tundu Lissu na Freeman Mbowe kwenye foleni ya zoezi la kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Mwenyekiti
4. Tundu Lissu na Freeman Mbowe wakifurahia pamoja baada ya kupiga Kura
Soma, Pia:
Soma, Pia: Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA 2025: Tundu Lissu ashinda nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa kwa Kura 513 sawa na 51.5%
Mnyukano wao kwenye mitandao ya kijamii na hata kwenye mahojiano na vyombo mbalimbali vya habari ilizua hisia kwamba huwenda hata wakikutana uso kwa uso basi wangezichapa ama kutoongea kabisa ila mambo hayakuwa hivyo na kuonesha somo kubwa la demokrasia.
Hapa nimekukusanyia baadhi ya matukio ya picha za kukumbukwa katika uchaguzi huu wa kihistoria katika chama chao;
1. Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwa mara ya kwanza kwenye Kikao cha Kamati Kuu Chadema, makuu ya chama hicho, Mikocheni Dar es Salaam, Ijumaa, Januari 10, 2025.