Picha mbili tofauti za waasisi wa TANU 1954

Picha mbili tofauti za waasisi wa TANU 1954

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
PICHA MBILI ZA WAASISI 17 WA TANU MWAKA WA 1954

Kuna picha mbili za waasisi 17 wa chama cha TANU tarehe 17 Julai 1954.

Picha ya kwanza ambao hawaonekani katika picha ni ni Ally Sykes, Tewa Said Tewa na Joseph Kasella Bantu.

Ukitazama picha hiyo ya kwanza hapo chini utaona kuwa kuna maelezo kuwa wazalendo hao hawapo kwenye picha.

Kwa nini hawapo katika picha ni kwa sababu hawa walikuwa watumishi wa serikali na wangetiwa matatani hata kupelekea kufukuzwa kazi endapo serikali ingekuwa na ushahidi kuwa wamehusika katika kuasisisi chama cha siasa.

Kuna picha ya pili ambayo kuna sura ya Kasella Bantu imeingizwa katikati ya Abdulwahid Sykes na Dossa Aziz.

Kazi hii ilifanywa na Idara ya Picha ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Sijui nini sababu na makusudio ya kufanya hivi kwa kuingiza picha ya Kasella Bantu kwenye picha hii halisi wala sijui kwa nini hawakuweka na picha ya Ally Sykes na Tewa Said Tewa ikiwa palikuwa na haja ya kuweka waasisi wote wa TANU katika picha hii ya kwanza.

Hiki ni kitendawili ambacho bado hakijateguliwa sasa mwaka wa 66 toka TANU iundwe.

Picha hii halisi yaani ''original,'' nimeipiga kutoka kitabu cha Saadan Abdu Kandoro, ''Mwito wa Uhuru,'' (1961).
20200614_055833.jpg
 

Attachments

  • WAASISI WA TANU 1.jpg
    WAASISI WA TANU 1.jpg
    7.3 KB · Views: 7
PICHA MBILI ZA WAASISI 17 WA TANU MWAKA WA 1954

Kuna picha mbili za waasisi 17 wa chama cha TANU tarehe 17 Julai 1954.

Picha ya kwanza ambao hawaonekani katika picha ni ni Ally Sykes, Tewa Said Tewa na Joseph Kasella Bantu.

Ukitazama picha hiyo ya kwanza hapo chini utaona kuwa kuna maelezo kuwa wazalendo hao hawapo kwenye picha.

Kwa nini hawapo katika picha ni kwa sababu hawa walikuwa watumishi wa serikali na wangetiwa matatani hata kupelekea kufukuzwa kazi endapo serikali ingekuwa na ushahidi kuwa wamehusika katika kuasisisi chama cha siasa.

Kuna picha ya pili ambayo kuna sura ya Kasella Bantu imeingizwa katikati ya Abdulwahid Sykes na Dossa Aziz.

Kazi hii ilifanywa na Idara ya Picha ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Sijui nini sababu na makusudio ya kufanya hivi kwa kuingiza picha ya Kasella Bantu kwenye picha hii halisi wala sijui kwa nini hawakuweka na picha ya Ally Sykes na Tewa Said Tewa ikiwa palikuwa na haja ya kuweka waasisi wote wa TANU katika picha hii ya kwanza.

Hiki ni kitendawili ambacho bado hakijateguliwa sasa mwaka wa 66 toka TANU iundwe.

Picha hii halisi yaani ''original,'' nimeipiga kutoka kitabu cha Saadan Abdu Kandoro, ''Mwito wa Uhuru,'' (1961).View attachment 1477867
historia ya nchi kiuhalisia ina kona kona nyingi kiasi kwamba inahitajika kuandikwa upya na baadhi ya wapigania uhuru kuwaomba radhi kwa kusaulika, ama kimakosa au kwa maksudi...
 
historia ya nchi kiuhalisia ina kona kona nyingi kiasi kwamba inahitajika kuandikwa upya na baadhi ya wapigania uhuru kuwaomba radhi kwa kusaulika, ama kimakosa au kwa maksudi...
Mambo ya kisiasa wale wenye malengo yenye utata wana tabia ya kuvuta muda badala ya kuwa waadilifu na kutenda haki ili wale watetezi waondoke halafu walete visingizio vingine.Mfano wa visingizio hivyo ni "vijana wote waliopo sasa wala hawaoni haja ya kufanya hivyo na kwamba watu wote sasa wamekuwa hivi na vile".
Kwa hili sheikh Mohammed Said endelea na kazi zako bila kuchoka.Hata hao wenye kupuuza ukweli hatimae wataondoka na Mwenyezi Mungu ataurudisha ukweli kila mtu ashangae nani aliyejuwa hayo.Na kwa sababu historia ni kwa ajili ya kulinda haki na kufichua ukweli basi hata hivyo vizazi vya wanaoficha ukweli hatimae wataelewa na kulaumu mababu zao.
 
historia ya nchi kiuhalisia ina kona kona nyingi kiasi kwamba inahitajika kuandikwa upya na baadhi ya wapigania uhuru kuwaomba radhi kwa kusaulika, ama kimakosa au kwa maksudi...
No future in the past,
Hata ikiandikwa upya,wale walioumizwa wakatambuliwa,majina yao,yakawekwa hata kwenye pesa,sasa itasaidia vipi,nchi,nchi ni maskini,huduma za afya hovyo,ajira hakuna,ufisadi wa kidola umejaa,
Kilimo kipo duni,
 
No future in the past,
Hata ikiandikwa upya,wale walioumizwa wakatambuliwa,majina yao,yakawekwa hata kwenye pesa,sasa itasaidia vipi,nchi,nchi ni maskini,huduma za afya hovyo,ajira hakuna,ufisadi wa kidola umejaa,
Kilimo kipo duni,
Juan...
Kila kitu kina mahali pake.

Mimi naheshimu msimamo wako kuwa haya hayana umuhimu.
Sawa wala si tatizo.

Historia hii haina umuhimu kwako lakini kwa wengine ni muhimu na ndiyo maana wakaweka picha ya Kasella Bantu katika picha ambayo hakuwepo.

Kwangu historia hii ina umuhimu mkubwa sana kwani ni historia ya wazee wangu walivyounda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Sawa bw JUAN MANUEL lakn history ni muhim ili vizazi vyetu vije vijifunze.
No future in the past,
Hata ikiandikwa upya,wale walioumizwa wakatambuliwa,majina yao,yakawekwa hata kwenye pesa,sasa itasaidia vipi,nchi,nchi ni maskini,huduma za afya hovyo,ajira hakuna,ufisadi wa kidola umejaa,
Kilimo kipo duni,
 
Back
Top Bottom