Kenyan
JF-Expert Member
- Jun 7, 2012
- 414
- 314
Raia wengi wa Kenya hasa wanaofanya kazi kati kati ya Jiji la Nairobi hawajafika mjini kutokana na woga wa vurumai za waandamanaji na mabomu ya machozi.
Maafisa wa polisi wameshika doria katika Barabara nyingi za kati kati ya Jiji. Ikumbukwe Rais William Ruto anatarajia wageni kadhaa wiki hii, wa kwanza akiwa ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Antonio Guterres ambaye atarajiwa kuwasili Nairobi Leo.
Aidha pia Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida anatarajiwa kuwasili Nairobi baadae.
Kiongozi mwengine anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini Kenya wiki hii ni Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.
Hatahivyo Kiongozi wa Upinzani Raila Odinga amesisitiza kuwa maandamano yataendelea kama kawaida akiwataka wafuasi wake kuandamana mpaka Ikulu.
Tayari maandamano yameanza katika Barabara ya Ngong ambapo basi la usafiri wa umma limeteketezwa na waandamanaji.
Wataalam wengi wa masuala ya kiusalama wamesema kuwa Jeshi la Polisi litatumia mbinu zile zile walizotumia mwezi Jana, ambapo lengo kuu lilikuwa ni kumzuia Odinga dhidi ya kuingia kati kati ya Jiji.
Maafisa wa polisi wameshika doria katika Barabara nyingi za kati kati ya Jiji. Ikumbukwe Rais William Ruto anatarajia wageni kadhaa wiki hii, wa kwanza akiwa ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Antonio Guterres ambaye atarajiwa kuwasili Nairobi Leo.
Aidha pia Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida anatarajiwa kuwasili Nairobi baadae.
Kiongozi mwengine anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini Kenya wiki hii ni Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.
Hatahivyo Kiongozi wa Upinzani Raila Odinga amesisitiza kuwa maandamano yataendelea kama kawaida akiwataka wafuasi wake kuandamana mpaka Ikulu.
Tayari maandamano yameanza katika Barabara ya Ngong ambapo basi la usafiri wa umma limeteketezwa na waandamanaji.
Wataalam wengi wa masuala ya kiusalama wamesema kuwa Jeshi la Polisi litatumia mbinu zile zile walizotumia mwezi Jana, ambapo lengo kuu lilikuwa ni kumzuia Odinga dhidi ya kuingia kati kati ya Jiji.