Huyu jamaa anaishi kawaida kabisa japokuwa ndie tajiri namba moja Africa. Hebu ktk hiyo picha tazama
1,Kalamu
2,Mapete vidoleni (hana)
3,Simu ya kawaida kabisa
Sisi ukipata hela za mkopo tu utavaa Mapete vidole vyote,utaning'iniza funguo za kavits ka mkopo hadi za mageti yote ya nyumbani kwako,utajifanya kuzungusha round wakati hela yenyewe ndio hiyohiyo, nk nk Tunaishi kimaigizo sana.
Tuna kiburi,jeuri,tu wavivu wengi wetu,hatuheshimu kazi,tunapenda sana siasa kuliko uchumi,si ajabu tutasalia hivihivi.
Tubadilike watanzania wenzangu.
FREEMAXENCE.
N'yadikwa
hela zilikosea kwenda kwa huyo
ukiwa na hela inabidi wanaokuchukia wanune kwa matusi yako ya kihela hela
kama mtaani hakuna lami exhaust unaigeuzia chini ukipita vumbi tu mpaka wakikuona wajizibe pua na midomo
kwa mtu kama dangote lengo lake ni kuwa tajiri na sio kuonekana tajiri, ila kwa sisi watu wa kawaida, hatuna pesa sio matajiri kwanini tusivae vizuri tukaonekana kidogo, au mkuu unajua gharama ya hiyo kanzu, ni mshahara wa mtu huo