nyumba kubwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 10,309
- 8,379
Hii kitu picha imesababisha hofu kubwa sana kwa mke wa jamaa yangu. Mke wa jamaa yangu aliikuta picha ya mpenzi wa mumewe aliyepiga naye kabla hajamuowa, lakini kibaya zaidi huyo mpenzi wake mke wake anamfahamu na alifariki kwa ukimwi na mke wa jamaa yangu anajua hivyo, lakini sio kwamba alikuwa na ukimwi wakati wakiwa wapenzi na jamaa yangu. Sasa mke hakuamini kama wako salama, pamoja na kwamba wameishi miaka 20 ndani ya ndoa na wana watoto 2, ilibidi awajulishe wanandugu wote na ikaamuliwa wakapime afya, ndiyo mke wake aliporidhika baada ya kukuta wapo safi. Cha ajabu ni picha ya miaka 20 iliyopita.
Mshiki kama wewe ndo umemuacha? inakuwaje hapa? maana najua mwenye kuachwa ndo anakua na maumivu
Mimi nimeachana GF 3, lakini nguo, picha na baadhi ya vitu vyao ninazo! Siku nikikutana na mmoja wapo namkumbusha tu kuwa kuna mizigo yake aliiacha, basi anabaki anacheka/kulia tu. Wengine ndiyo hivyo tena anakuwa anataka turudiane.
Unasahau.
na wewe za kwako utapeleka wapi?hahahaa Meku, hapa sasa ataamua mwenyewe, akiziweka haya, akizichoma sawa, akizipandika kadamnasi namshitaki....lol
Ukiwa na mjengo wako utafanyaje, utauuza?ikitokea baby come back?
Aaaah wapi mi huwa siruhusu kitu kama hicho mkataba ukikatika basi nahama mpaka mtaa ili kupunguza bugudha
Kwenye mahusiano/ndoa watu hua wanapiga picha pamoja . . . kwaajili ya ukumbusho.
Kwa wale mlioko facebook mnajua siku hizi hizo picha haziishi kwenye album makabatini tu na ukutani ila mpaka mitandaoni unakuta mmoja ana picha kibao za mwenzake bila kusahau description za ohh huyu ndie. . baby wangu and so so.Nimeona mmoja kajaza kweli za girlfriend wake nikajikuta najiuliza kama siku wakiachana atazifutilia tu mbali au itakuaje.
Swali. . .je ikiwa mahusiano yatavunjika zile picha mlizopeana na kupiga pamoja zinatakiwa zifanyweje?Ni sahihi kuziweka tu?Zinatakiwa zitupwe/chanwe. . . kama jibu ni ndio je za harusi?Ni sahihi kweli kuharibu/tupa picha unayopenda kisa tu uliyeachana nae yumo?Na kama ukiweka kuna madhara?
Lizzy binafsi if we are done we are done.....
I want nothing to remind me of you, kwanza ili iweje?
wengine hizo picha wanapeleka kwa waganga wa kienyeji. anafifisha nyota yako hadi umkumbukee
Lini umekua? Si tumekucheza juzi tu wewe.
Imagine mtu umeishi naye mfano 10 years, mna watoto, do u think its easy?
Kongosha acheni kunitisha bana. . .
Semeni tu nikue niyaone manini???