Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Mapenzi yanatakiwa yakupe furaha ya kimwili, akili na kiuchumi.
Sasa utakuta mtu ameingia kwenye mahusiano, ghafla uchumi unayumba; fedha hazipatikani tena, madeni yamekuwa mengi, kila kona ukipita unadaiwa.
Mara kurukwa na akili na kujikuta unaongea mwenyewe mwenyewe barabarani, ukiwa kwenye kikao unashinda kuongea pointi kutokana na changamoto ya magonjwa ya akili.
wakati mwingine unavaa mavazi yaliyochakaa, mkanda umepauka, viatu vimepauka, soli ya kiatu inaenda upande; mipango ya kimaendeleo ya kufungua biashara ujenzi n.k yote imekufa.
Na haya yote, unakuta yameanza ukiwa kwenye mahusiano; kabla ya mahusiano hayakuwepo.
Sasa, kwanini ubaki kwenye mahusiano ya namna hiyo, yanayokutesa?
Piga chini na usonge mbele.
Sasa utakuta mtu ameingia kwenye mahusiano, ghafla uchumi unayumba; fedha hazipatikani tena, madeni yamekuwa mengi, kila kona ukipita unadaiwa.
Mara kurukwa na akili na kujikuta unaongea mwenyewe mwenyewe barabarani, ukiwa kwenye kikao unashinda kuongea pointi kutokana na changamoto ya magonjwa ya akili.
wakati mwingine unavaa mavazi yaliyochakaa, mkanda umepauka, viatu vimepauka, soli ya kiatu inaenda upande; mipango ya kimaendeleo ya kufungua biashara ujenzi n.k yote imekufa.
Na haya yote, unakuta yameanza ukiwa kwenye mahusiano; kabla ya mahusiano hayakuwepo.
Sasa, kwanini ubaki kwenye mahusiano ya namna hiyo, yanayokutesa?
Piga chini na usonge mbele.