Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 144
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wamewataka wazanzibari kulaani kwa nguvu zote matamshi yaliotolewa jana na Waziri Mkuu Mizengo Peter Pinda ya kutaka kuifuta Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ)na kubakia serikali moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Matamshi hayo yametolewa na wajumbe hao wakati wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Fedha na Uchumi katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea Maisara Mjini Unguja.
Wawakilishi hao walisema Waziri Mkuu Pinda ni Kiongozi asiyeitakia mema Zanzibar kutokana na kauli zake za mara kwa mara za kuidharau na kuikejeli serikali ya mapinduzi ambapo walisema wanalaani matamshi hayo lakini pia wamewataka wanzanziri wote kulaani vikali matamshi yake aliyoyatoa juzi bungeni.
Mwakilishi wa Jimbo la Tumbatu (CCM) Haji Omar Kheri amemtaka Waziri Mkuu Pinda aanze kujizuia kutoa matamshi yake yanayoiweka Zanzibar katika wakati mgumu na wasiwasi wa utatanishi.
Kheri ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Chama Cha Mapinduzi (CCM) alisema kutokana na Zanzibar kuwa na nia njema na Muungano ilisamehe na kukubali kupoteza hata Utaifa na utambulisho wake kwa kuungana na Tanganyika mwaka 1964, jambo ambalo alisema halionekani kuthamininwa na Watanganyika hivi sasa.
Alisema kama kuna mtu anabeza hoja ya mafuta na gesi asilia kuondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano basi huyo ndiye adui anayetaka kuuvunja muungano uliopo kwa miaka 45 na sio wazanzibari amabo wanadai haki zao katika muungano uliopo amabo hautendi haki sawa kwa pande mbili hizo.
Mwakilishi huyo alisema hakuna haja ya wabunge kuwaona wawaklilishi hawana mamlaka ya kujadili mustakabali wa Zanzibar na badala yake kinachotakiwa ni kuheshimiana na kuthanminiana katika pande zote mbili ambazo kila moja ina mamlaka yake na katiba ya kuendesha nchi.
"Uchumi wa Zanzibar haulingani na Tanzania Bara,bajeti ya Zanzibar ni 400 bilioni wakati wenzetu wanagota katika Trilioni 35,mafuta ni kichocheo cha SMZ kujinasua kiuchumi na kukuza maendeleo ya jamii lakini naona hivi sasa kila siku kunazuka jambo jengine" alisema Kheri ambaye pia ni Mnadhimu wa Baraza la wawakilishi kwa upande wa CCM.
Mnadhimu huyo alisema hoja ya mafuta na gesi asilia kubakishwa katika orodha ya mambo ya muungano sio ya Rais wa Zanzibar na Mweyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Aman Karume na Waziri wa Maji Ujenzi Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid bali ni msimamo wa Baraza la Wawakilishi na ndio uamuzi wa wananchi wote wa visiwa vya Unguja na Pemba.
"Suala la mafuta ni gumu na halitekelezeki katika mfumo wa Muungano, litashindikana kama suala la Bandari linavyoleta utata ambalo ni la Muungano, lakini likisimamiwa na kila upande chini ya chombo chake husika yaani PTA na ZPC" Alisema Kheri.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo la Chonga (CUF) Abdallah Juma Abdallah alisema kauli ya Waziri Mkuu Pinda si kauli ya kiungwana na haipaswi kuzungumzwa na mtu mzito kama yeye.
Alisema kauli yake hailengi kuimarisha Muungano bali inalenga kuvunja Muungano na hakutarajia kabisa kama mtu mzima kama yeye anaweza kufikiria kuifuta SMZ wakati huu ambao Muungano umedumu kwa miongo kadhaa.
"Kwa Kweli Mheshimiwa Spika nilikuwa natizama TV na niliposikia kauli ile ya Pinda alipoitoa bado kidogo tu niivunje TV yangu mwenyewe…niliitukana na kukereka jinsi alivyokuwa akitoa matamshi yale,sisi ni watu wazima hakuna sababu ya kutishana kama ni Muungano wa kutishana mimi simo kabisa nasema kwa uhakika kabisa" alisema Mwakilishi huyo.
Mwakilishi huyo mbali ya kulaani kauli ya Waziri Mkuu alisema matamshi hayo ni kama ni mwendelezo na dhamira ya SMT kutaka kuifuta SMZ katika ramani ya dunia na kuongeza kwamba wazanzibari hawatakuwa tayari kuona kifo cha SMZ kwani hivi sasa inaonekana Tanganyika wameshoshwa na wazanzibari kutokana na kauli zao wanazozitoa ambazo zimekosa uvumilivu.
Mwakilishi wa Jimbo la Chake Chake (CUF), Omar Ali Shehe amewataka wawakilishi na wananchi wote wa Zanzibar kulaani vikali matamshi hayo ambayo yenye kutishia kuifuta Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Alisema lengo la Tanganyika hivi sasa ni kuifanya zanzibar ni mkoa mmoja wapo wa Tanzania jambo ambalo kabisa halitawezekana kwa kwa kuwa Zanzibar ina mamlaka yake kamili kama ilivyo Tanzania.
Mwakilishi huyo wa Chake Chake alisema kufa kwa SMZ hakutakubaliwa kabisa kwani wazee waliotangulia walipindua kwa kutumia mawe, mashoka na mapanga ambapo wengi wao walipoteza maisha yao hivyo sio rahisi leo hii ielezwe kuwa hakuna serikali ya Zanzibar.
Alisema bila ya kuwepo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar hakutakuwa na heshima ya mzanzibari hivyo alimtaka Waziri Mkuu Pinda na wenzake wenye ndoto ya kuizika Zanzibar na kuitoa katika ramani ya dunia wasahau jambo hilo kwani hakuna mzanzibari atakayekubali suala hilo hata siku moja.
"Mheshimiwa Spika tumekerwa sana na kauli ya Pinda na kwa umoja wetu tunasema kwamba tunayalaami matamshi haya ya mtoto wa mkulima (Pinda) na tunamwambia kama ameshindwa kazi aende akachuke jembe na kuendeleza kilimo na sisi tumeshaamua kuwa mafuta hayatakuwa ya Muungano wala hatubadilishi kauli zetu huo ni msimamo wa wazanzibari" . Alisisitiza mwakilishi huyo ambaye ni mdogo kiumri
Shehe alisema kwamba Zanzibar haiwezi kabisa kusaga meno ikiwa nje ya muungano kwani rasilimali zilizoko Zanzibar zinawatosha wazanzibari kwa uchache wao na hivyo hakuna haja ya kutishana na kudhalilishana.
Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani (CUF) Hija Hassan Hija alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imevumilia sana uonevu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuikandamiza na kuiburuza Zanzibar kwa muda mrefu katika uchumi.
Amesema wakati umefika hivi sasa uonevu huo hautakubalika tena na kuwataka wananchi wasikubali kabisa kuyakubali maneno yanayoendelea kutolewa na viongozi wa seriakli ya jamhuri hasa yale yenye nia ya kuivuruga Zanzibar na kuipoteza katika ramani ya dunia.
Wananchi mbali mbali jana walionekana kujikusanya wakitafakari juu ya kauli ya waziri Mkuu Pinda aliyoitoa bungeni ambapo wengi wao walisema hivi sasa inaonekana watanzania hasa viongozi wamechoshwa na uvumilivu na wanataka Muungano uliopo kati ya Zanzibar na Tanzania Bara uvunjike.
"Hata siku moja maneno ya pinda hayawezi kuchukuliwa kama ni sahihi tanznaia bara ina mikoa mingapi? Ikiwa wanashindwa kuihudumia mikoa yao kuwa watu wanakaa na njaa wataweza kuifanya serikali moja halafu waweze kuihudumia huyu hana…akili zao sio timamu akapimwe kwanza Zanzibar ni nchi huru Pinda hata aende kuzikiri uchi Zanzibar haiwezi kufanywa nchi moja alaaa" alisema kwa hasira mkaazi mmoja wa Said Sudi Mkaazi wa Michenzani.
Juzi Waziri Mkuu Pinda wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo Bungeni Mjini Dodoma alisema kwamba kelele kuhusu mafuta na gesi asilia zitakwisha kwa kuwa na nchi moja yenye serikali moja kuliko serikali mbili.
Waziri Mkuu Pinda alisema hayo kufuatia swali aliloulizwa na Mbunge wa Jimbo la Ziwani (CUF) Ali Said Salim kuhusu mambo yasiokuwa ya Muungano yanaongozwa kupitia serikali gani kwa upande wa Tanzaania Bara wakati Zanzibar imesimamiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG.
Matamshi hayo yametolewa na wajumbe hao wakati wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Fedha na Uchumi katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea Maisara Mjini Unguja.
Wawakilishi hao walisema Waziri Mkuu Pinda ni Kiongozi asiyeitakia mema Zanzibar kutokana na kauli zake za mara kwa mara za kuidharau na kuikejeli serikali ya mapinduzi ambapo walisema wanalaani matamshi hayo lakini pia wamewataka wanzanziri wote kulaani vikali matamshi yake aliyoyatoa juzi bungeni.
Mwakilishi wa Jimbo la Tumbatu (CCM) Haji Omar Kheri amemtaka Waziri Mkuu Pinda aanze kujizuia kutoa matamshi yake yanayoiweka Zanzibar katika wakati mgumu na wasiwasi wa utatanishi.
Kheri ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Chama Cha Mapinduzi (CCM) alisema kutokana na Zanzibar kuwa na nia njema na Muungano ilisamehe na kukubali kupoteza hata Utaifa na utambulisho wake kwa kuungana na Tanganyika mwaka 1964, jambo ambalo alisema halionekani kuthamininwa na Watanganyika hivi sasa.
Alisema kama kuna mtu anabeza hoja ya mafuta na gesi asilia kuondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano basi huyo ndiye adui anayetaka kuuvunja muungano uliopo kwa miaka 45 na sio wazanzibari amabo wanadai haki zao katika muungano uliopo amabo hautendi haki sawa kwa pande mbili hizo.
Mwakilishi huyo alisema hakuna haja ya wabunge kuwaona wawaklilishi hawana mamlaka ya kujadili mustakabali wa Zanzibar na badala yake kinachotakiwa ni kuheshimiana na kuthanminiana katika pande zote mbili ambazo kila moja ina mamlaka yake na katiba ya kuendesha nchi.
"Uchumi wa Zanzibar haulingani na Tanzania Bara,bajeti ya Zanzibar ni 400 bilioni wakati wenzetu wanagota katika Trilioni 35,mafuta ni kichocheo cha SMZ kujinasua kiuchumi na kukuza maendeleo ya jamii lakini naona hivi sasa kila siku kunazuka jambo jengine" alisema Kheri ambaye pia ni Mnadhimu wa Baraza la wawakilishi kwa upande wa CCM.
Mnadhimu huyo alisema hoja ya mafuta na gesi asilia kubakishwa katika orodha ya mambo ya muungano sio ya Rais wa Zanzibar na Mweyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Aman Karume na Waziri wa Maji Ujenzi Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid bali ni msimamo wa Baraza la Wawakilishi na ndio uamuzi wa wananchi wote wa visiwa vya Unguja na Pemba.
"Suala la mafuta ni gumu na halitekelezeki katika mfumo wa Muungano, litashindikana kama suala la Bandari linavyoleta utata ambalo ni la Muungano, lakini likisimamiwa na kila upande chini ya chombo chake husika yaani PTA na ZPC" Alisema Kheri.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo la Chonga (CUF) Abdallah Juma Abdallah alisema kauli ya Waziri Mkuu Pinda si kauli ya kiungwana na haipaswi kuzungumzwa na mtu mzito kama yeye.
Alisema kauli yake hailengi kuimarisha Muungano bali inalenga kuvunja Muungano na hakutarajia kabisa kama mtu mzima kama yeye anaweza kufikiria kuifuta SMZ wakati huu ambao Muungano umedumu kwa miongo kadhaa.
"Kwa Kweli Mheshimiwa Spika nilikuwa natizama TV na niliposikia kauli ile ya Pinda alipoitoa bado kidogo tu niivunje TV yangu mwenyewe…niliitukana na kukereka jinsi alivyokuwa akitoa matamshi yale,sisi ni watu wazima hakuna sababu ya kutishana kama ni Muungano wa kutishana mimi simo kabisa nasema kwa uhakika kabisa" alisema Mwakilishi huyo.
Mwakilishi huyo mbali ya kulaani kauli ya Waziri Mkuu alisema matamshi hayo ni kama ni mwendelezo na dhamira ya SMT kutaka kuifuta SMZ katika ramani ya dunia na kuongeza kwamba wazanzibari hawatakuwa tayari kuona kifo cha SMZ kwani hivi sasa inaonekana Tanganyika wameshoshwa na wazanzibari kutokana na kauli zao wanazozitoa ambazo zimekosa uvumilivu.
Mwakilishi wa Jimbo la Chake Chake (CUF), Omar Ali Shehe amewataka wawakilishi na wananchi wote wa Zanzibar kulaani vikali matamshi hayo ambayo yenye kutishia kuifuta Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Alisema lengo la Tanganyika hivi sasa ni kuifanya zanzibar ni mkoa mmoja wapo wa Tanzania jambo ambalo kabisa halitawezekana kwa kwa kuwa Zanzibar ina mamlaka yake kamili kama ilivyo Tanzania.
Mwakilishi huyo wa Chake Chake alisema kufa kwa SMZ hakutakubaliwa kabisa kwani wazee waliotangulia walipindua kwa kutumia mawe, mashoka na mapanga ambapo wengi wao walipoteza maisha yao hivyo sio rahisi leo hii ielezwe kuwa hakuna serikali ya Zanzibar.
Alisema bila ya kuwepo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar hakutakuwa na heshima ya mzanzibari hivyo alimtaka Waziri Mkuu Pinda na wenzake wenye ndoto ya kuizika Zanzibar na kuitoa katika ramani ya dunia wasahau jambo hilo kwani hakuna mzanzibari atakayekubali suala hilo hata siku moja.
"Mheshimiwa Spika tumekerwa sana na kauli ya Pinda na kwa umoja wetu tunasema kwamba tunayalaami matamshi haya ya mtoto wa mkulima (Pinda) na tunamwambia kama ameshindwa kazi aende akachuke jembe na kuendeleza kilimo na sisi tumeshaamua kuwa mafuta hayatakuwa ya Muungano wala hatubadilishi kauli zetu huo ni msimamo wa wazanzibari" . Alisisitiza mwakilishi huyo ambaye ni mdogo kiumri
Shehe alisema kwamba Zanzibar haiwezi kabisa kusaga meno ikiwa nje ya muungano kwani rasilimali zilizoko Zanzibar zinawatosha wazanzibari kwa uchache wao na hivyo hakuna haja ya kutishana na kudhalilishana.
Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani (CUF) Hija Hassan Hija alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imevumilia sana uonevu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuikandamiza na kuiburuza Zanzibar kwa muda mrefu katika uchumi.
Amesema wakati umefika hivi sasa uonevu huo hautakubalika tena na kuwataka wananchi wasikubali kabisa kuyakubali maneno yanayoendelea kutolewa na viongozi wa seriakli ya jamhuri hasa yale yenye nia ya kuivuruga Zanzibar na kuipoteza katika ramani ya dunia.
Wananchi mbali mbali jana walionekana kujikusanya wakitafakari juu ya kauli ya waziri Mkuu Pinda aliyoitoa bungeni ambapo wengi wao walisema hivi sasa inaonekana watanzania hasa viongozi wamechoshwa na uvumilivu na wanataka Muungano uliopo kati ya Zanzibar na Tanzania Bara uvunjike.
"Hata siku moja maneno ya pinda hayawezi kuchukuliwa kama ni sahihi tanznaia bara ina mikoa mingapi? Ikiwa wanashindwa kuihudumia mikoa yao kuwa watu wanakaa na njaa wataweza kuifanya serikali moja halafu waweze kuihudumia huyu hana…akili zao sio timamu akapimwe kwanza Zanzibar ni nchi huru Pinda hata aende kuzikiri uchi Zanzibar haiwezi kufanywa nchi moja alaaa" alisema kwa hasira mkaazi mmoja wa Said Sudi Mkaazi wa Michenzani.
Juzi Waziri Mkuu Pinda wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo Bungeni Mjini Dodoma alisema kwamba kelele kuhusu mafuta na gesi asilia zitakwisha kwa kuwa na nchi moja yenye serikali moja kuliko serikali mbili.
Waziri Mkuu Pinda alisema hayo kufuatia swali aliloulizwa na Mbunge wa Jimbo la Ziwani (CUF) Ali Said Salim kuhusu mambo yasiokuwa ya Muungano yanaongozwa kupitia serikali gani kwa upande wa Tanzaania Bara wakati Zanzibar imesimamiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
SOURCE: ZANZIBAR YETU BLOG.
Last edited: