Mhe.Chana Apokelewa kwa Shangwe za Utamaduni na Sanaa
Na Shamimu Nyaki
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Februari 17, 2023 amewasili kwa mara ya kwanza wizarani hapo baada ya Kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hivi karibuni kuiongoza wizara hiyo.
Mara baada ya kupokelewa na Mtangulizi wake Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye sasa ni Waziri wa Maliasili na Utalii, amejionea burudani nzuri kabisa kutoka kwa watumishi wa wizara hiyo waliobobea katika Sekta za Utamaduni na Sanaa.
Watumishi walimpokea kwa ngoma, nyimbo utenzi na majigambo yaliyoongozwa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sanaa Dkt. Asha Salum
Mapokezi ya Mhe. Waziri yalipambwa pia kwa nyimbo zenye ujumbe wa ukaribisho ambazo ziliimbwa na Maafisa Utamaduni wa Wizara hiyo.
Na Shamimu Nyaki
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Februari 17, 2023 amewasili kwa mara ya kwanza wizarani hapo baada ya Kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan hivi karibuni kuiongoza wizara hiyo.
Mara baada ya kupokelewa na Mtangulizi wake Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye sasa ni Waziri wa Maliasili na Utalii, amejionea burudani nzuri kabisa kutoka kwa watumishi wa wizara hiyo waliobobea katika Sekta za Utamaduni na Sanaa.
Watumishi walimpokea kwa ngoma, nyimbo utenzi na majigambo yaliyoongozwa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sanaa Dkt. Asha Salum
Mapokezi ya Mhe. Waziri yalipambwa pia kwa nyimbo zenye ujumbe wa ukaribisho ambazo ziliimbwa na Maafisa Utamaduni wa Wizara hiyo.