PISHI: Chipsi za ndizi mzuzu

PISHI: Chipsi za ndizi mzuzu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
IMG_2576.jpg


Maandalizi; dakika 5
Muda wa kupika; dakika 10
Muda jumla; dakika 15


Mahitaji
1. Ndizi mzuzu tatu kubwa
2. Vijiko 4 vya chakula chenga za mkate
3. Mafuta ya kutosha ya kukaangia
4. Chumvi au viungo vingine

Maelekezo


1. Menya na kukatakata ndizi umbo la chispi kubwa kubwa kiasi; nyunyizia chumvi na pilipili manga uchanganye vizuri

IMG_2545.jpg


2. Kwenye kikaangio kikubwa moto wa juu kiasi, weka mafuta ya kupikia acha yachemke vizuri. Wakati mafuta yanachemka, chovya vipande vya ndizi kwenye chenga za mkate hadi zifunikwe vizuri, kandamiza na mkono chenga zishike kwenye ndizi vizuri.

3. Kaanga kwa dakika mbili upande wa kwanza, geuza kwa dakika moja upande wa pili, au mpaka ziive ziwe na rangi ya kahawia.

4. Ipua kutoka kwenye mafuta, ziweke kwenye sahani yenye tissues zichuje mafuta.


Jikoni na jane


 
Back
Top Bottom