Pishi: Jinsi ya kutengeneza Kalimati ya maharage

Pishi: Jinsi ya kutengeneza Kalimati ya maharage

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Jinsi ya kutengeneza Kalimati ya maharage:
Maharage yanatumika katika mapishi aina nyingi sana, Leo tutapika kalimati kwa kutumia maharage!. Kaimati hii ni nzuri sana kwani ina maharage yenye protini nyingi.

Maandalizi na Mahitaji

Ingredients
  • Maharage yaliyopikwa na kuiva 1/2 kikombe.
  • Maziwa safi 1/4 kikombe.
  • unga wa ngano Kikombe kimoja.
  • Mafuta ya kupikia.
  • Chumvi kiasi.
  • Yai 1.
  • Baking powder 1/2 kijiko cha chai (ukipenda).
Utayarishaji
Jinsi ya kutengeneza Kalimati hatua kwa hatua
  1. Chemsha maharage hadi yalainike na kukauka maji.
  2. Maharage yakipoa songa hadi yalainike vizuri.
  3. Chukua Una wa ngano changanya na barking powder kisha chekecha na tia chumvi.
  4. Changanya unga na maharage katika bakuli kubwa safi
  5. Koroga yai.
  6. Tia yai katika mchanganyiko huo, changanya vizuri
  7. Tia maziwa kwenye mchanganyiko huo, hakikisha unakuwa mzito wa kutosha unaokatika ukimimina.
  8. Chemsha mafuta katika kikaangio chako.
  9. Chota na kijiko cha chakula weka kwenye mafuta yanayochemka.
  10. Choma mpaka ziwe za kahawia. Tayari kitafunwa.
 
Hii kichwani nikipiga picha najikuta inanijia picha ya bajia za dengu...kwenye mlo inaruhusiwa kuliwa na chatne?
 
Back
Top Bottom