Braza fanya research kwa utulivu na umakini wa hali ya juu
Kama mdau aliyesema hapo juu, kampuni nyingi zinawekeza matangazo ya online kuliko mabango, vipeperushi n.k. Teknolojia imebadilika
Pili, hao akina Outdoor wameweka mabango yao sio kwa interval...wameweka sehemu maalum kama njiapanda, sehem zenye foleni, sehem zenye mikusanyiko ya watu wengi kama masoko n.k.
Tatu, kampuni nyingi zenye uwezo wa kulipia tangazo hutaka coverage kubwa thats why unaona hao jamaa wako barabara kuu tu
Nne, kwa milioni 60 haitakidhi, hapa itabidi uongeze. Kama utataka kuinstall frem kubwa kama hao competitors wako...maana frem moja tu hapo ni million kadhaa, mafundi, material, before kodi, kulipia eneo....
Nitaendelea...