Pitia uzi huu ujifunze umuhimu wa kukagua gari kama una watoto wadogo

Pitia uzi huu ujifunze umuhimu wa kukagua gari kama una watoto wadogo

Matanga

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2019
Posts
2,281
Reaction score
3,976
Juzi ijumaa nilirudi nyumbani mchana kwa lunch na kuona watoto. Baada ya lunch na kuwahudumia kidogo nikarudi kazini.

Baada ya nusu saa dada yao akanipigia kuwa Gerry (my first born) haonekani nyumbani. Nilikuwa kwenye mkutano muhimu sana kwangu.

Nikatoka na kumpigia dada yao amtafute mpaka kwenye makabati maana anapenda tabia ya kujificha.

Hapo nilikuwa nafanya taratibu za kuomba udhuru na kumuachia mtu majukumu yangu. Baada ya kupata ruhusa nikaelekea kwenye gari ili nikasaidie kumtafuta. Kufungua gari nilipiga yowe la taharuki.

Nilimkuta mtoto akiwa anatoka jasho sana, amechoka, kwa kifupi alikuwa hoi. Hii ni kutokana na kukosa hewa kwa muda. Alipatiwa huduma ya kwanza, muhimu ilikuwa ni kupata hewa safi. Niliogopa sana, nilipata mshtuko mkubwa. Mpaka leo nikikumbuka nahisi vibaya.

Baada ya yeye kupata nafuu nilimuomba aniambie ilikuwaje. Akaniambia alivyoona naenda kazini alitangulia kwenye gari akajificha siti ya nyuma chini. Then akapitiwa na usingizi. Aliamshwa na joto kali ikabidi achukue documents zangu achane ajifutie jasho. Then akawa anachoka. Alipita uncle alimuita ila hajasikia. Ndo anaishia kusema hivyo.

Wapendwa nime share na nyie ili tuwe makini na watoto wetu. Ni watundu sana. Tukague magari yetu ndani na chini kabla ya kuondoka.

Namshukuru sana Mungu kwa maana bado ametaka niwe na mtoto huyu hadi leo.

..it's a true story

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mwamwala iyunga,
Tatizo la kudekeza watoto kama mayai kuna siku utampoteza. Wewe tabia yake ya kijinga ya kujificha unaijua sasa kwa kuwa unamdekeza amekuzoea huwezi kuchukua hatua ndiuo maana alifanya ujinga huo. Simama kama mzazi ukizoeana sana na mtoto eti unaishi kizungu sijui mom!! dad!!! matokeo ndio hayo
 
mwamwala iyunga,
UKiwa unapaki gari, jenga tabia ya kuacha japo sehemu kidogo wazi ya vioo viwili. Hii itakusaidia pia kupunguza joto ndani ya gari lako.
 
Nawe ujifunze yafuatayo:

1. Ukipaki gari popote hata kama ni nyumbani hakikisha umelock milango yote.
2. Kabla ya kuanza safari kagua siti za nyuma kwanza.


BTW sina gari,bajaji,pikipiki wala baiskeli.

Unforgetable
 
Tahadhari ingine ni hii hakikisha unafunga ile child lock siku moja mtoto wangu alifungua mlango wa nyuma wakati gari linatembea ingelikua sinaangalia kioo cha pembeni kile cha dereva kijana angedondoka..na ningemkanyaga na tairi
 
Aseee watoto wamekuwa watundu afu na viakili vya kujiongeza sana sku izi yaan usipokuwa makini kweli ni changamoto
 
Hii ilimkuta Dada mmoja alikuja sokoni TX pale kinondoni A kaenda sokoni Ndani ya Gari aliwaacha Watoto ndani vioo vyote kapandisha juu... Ndani ya Gari kulikuwa na Watoto 3.

Inavyoelekea lock zilijifunga na joto lile kukosa hewa.... Kuna mtoto alikuwa analia
Nakumbuka sisi tulikuwa upande wa pale wanapouza pikipiki kubwa used tunaziangalia
Nkashtuka Kuna Hali fulani pale siyo

Nkamwambia mwenzangu wale Watoto Ndani wame kwamaa kusogeaaa wamejaa jashoo kuulizia mwenye Gari yuko wapi mpemba mmja akasema alimuona kama nusu saa iliyopita akishuka

Ahhh hpo ikabidi wanaume tutumie mbinu za uwizi kufungua Gari maana pale tunafahamika DK 3 nying mlango iko wazi. Wale watoto baada ya kupata hewa dah walipatwa na ahueni.

Mara yule mama akaja mbioooo alikuwa dad's mkenya wacha watu waanze kumlaumu kwa uzembe

Alitushukuru ila tulimpiga fine ya bia hapo hunters club

Unapokuwa na Watoto lazima mtu uwe makini

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom