Mkuu kwani kwenye ligi toka 2019 hadi sasa yanga kaifunga simba mara ngapi? Naona umeandika libarua lireeeeefu kisa kukandwa na kibu denga
Ha ha ha!
Yaani Mkuu umesahau tumewakanda mno hadi jezi mkazifanya tambala la deki mkawa mnaona aibu kuzivaa mitaani!
Ngoja nikutajie mechi tulizowakanda ninazokumbuka
1. Morisson aliwatungua Makolo goli moja la uchungu la Faulo nje ya 18 hadi Manula akapiga makofi mkasema kahongwa!
2. Zawadi Mauya aliwatungua Makolo goli moja tu likawauma mno shuti kali la kuua kipa dkk 12 tu mkapambana na goli halikurudi.
3. Mayele aliwapiga Taifa goli 2 safi baada ya kudai Bwana misifa wenu Inonga eti anatosha! Changanya Inonga, Onyango na Tshabalala wote Mayele anawaweka mfukoni siku akimka vyema anaitwa Goal Scoring Machine (GSM)
4. Feisal aliwapasua Kirumba goli la karne shuti Kali hakuna Dunia nzima, lile goli Bado hamjalilipa linawauma hadi Leo mlivyo mbumbumbu mkaamua kumrubuni na kuua kipaji chake Yuko Zenji tu anakula urojo!
5. Saidoo alipiga kiufundi penati ya mwisho kule Zenji tukawakanda na kubeba Mapinduzi cup.
6. Mechi ya karibuni mkidhani mmeshinda Aziz Ki Mzee wa kuwapiga matobo kina Tshabalala akapiga Faulo kama Yuko Madrid!!
Mbumbumbu jengeni basi sanamu la Rage maana hata mkandwe vipi mnakunja ngumi tu! Uwezo hamna, kocha Mzee, wachezaji wazee, mashabiki wazee, kombe hata moja hamna zimebaki kelele tu mara ooh tumechukua kombe la kufa kiume!
Leo Simba mnakandwa Tena na Azam jamaa wanapenda sifa hao, kuifunga Simba ndo Raha yao! mtakoma! Mi nimekaa paleeee kibanda umiza Buza kwa Mpalanger, Mkishakandwa mje kushtaki maana last time niliwaambia mkitoka Wydad Morocco mje kushtaki hamkuja, nimemaindi kinoma, mi Huwa sipendi dharau!