Plantain/mzuzu/mkono wa tembo

Plantain/mzuzu/mkono wa tembo

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1100160


1100197


Ni kaka wa ndizi, hupikwa zikiwa mbichi au zimeiva.

Zina kiwango cha potassium mara mbili zaidi ya ndizi za kawaida

Jinsi ya kupika mzuzu wa nazi
1100383


Mahitaji
Ndizi 6
Nazi
Iliki
Safron
Unga wa mchele vijiko 3 vya chakula
Ghee kijiko kimoja cha chakula
Chumvi na sukari kiasi unachopenda

Upishi
Menya ndizi zitoe moyo na ukate size unayopenda
Loweka kwenye safron
Kuna nazi, weka tui la pili jikoni na ndizi, piga tui lisikatike,
Twanga iliki weka iliki ndani
Koroga unga wa mchele kwenye kijombe cha maji, hakikisha hauna mabonge weka kwenye ndizi endelea kupiga tui lisilete mabonge.
Weka tui bubu
Weka ghee (kama unapenda) hasa kama huna wasiwasi wa unene
Weka chumvi na sukari kama ndizi hazina sukari ya kutosha.
Tui likiiva okoa sufuria jikoni.
 
Hizo ndizi zikiwa zimeiva zikachomwa vizuri au kuchesha ndo chakula changu Cha kwanza nachopenda Sana..

Zikiwa mbichi sitaki hata kuona sura yake


Hapa ninazo kama 10 hazikozagi hizo
 
Hizo ndizi zikiwa zimeiva zikachomwa vizuri au kuchesha ndo chakula changu Cha kwanza nachopenda Sana..

Zikiwa mbichi sitaki hata kuona sura yake


Hapa ninazo kama 10 hazikozagi hizo
Zikiwa mbichi kula moja tu ya kuchemsha ikiwa bado ya moto na supu. Ni shibe kamili ya siku.
 
Zikiwa mbichi kula moja tu ya kuchemsha ikiwa bado ya moto na supu. Ni shibe kamili ya siku.
Yaani hizo mbichi pika upikavyo sitaki hata kuziona...

Zikiiva au kuiva kupitiliza km zinataka kuoza pale ndo hatari [emoji91]
 
Yaani hizo mbichi pika upikavyo sitaki hata kuziona...

Zikiiva au kuiva kupitiliza km zinataka kuoza pale ndo hatari [emoji91]
Zinakuawna sukari balaa mimi zikiiva sana ninachanganya na zinazoanza kuiva ili kubalance sukari
 
😂😂😂😂😂😂😂 futari tayari hapo Mkuu ila hauko pekee yako mie baada ya kuona uzi huu uko jukwaa lipi ndiyo nikatoka huko ullpowaza wewe.

Aisee, nina uhakika kuna watakao waza nilicho waza.
 
😂😂😂😂😂😂😂 futari tayari hapo Mkuu ila hauko pekee yako mie baada ya kuona uzi huu uko jukwaa lipi ndiyo nikatoka huko ullpowaza wewe.

Mwanzo aliweka ndizi tu bila msosi, naona thread imekuwa edited.

Itabidi niifute hiyo post.
 
😂😂😂😂😂😂😂 futari tayari hapo Mkuu ila hauko pekee yako mie baada ya kuona uzi huu uko jukwaa lipi ndiyo nikatoka huko ullpowaza wewe.
Nimecheka kwa nguvu
Baada ya kuona ni Sky Eclat nikajua ni mamulomulo
 
Mbwembwe zote za nini? Wewe menya, tia kwenye mkaa...choma, kula...shushia na K Vant kalale. Kwisha.
Gadeim... mi hapo nimeona kinywaji tu basi. Ndizi kitu gani bhana, hata mbuzi anakula ndizi kudadadeki!
 
Back
Top Bottom