Pls advice, tabia za mmewe zimemchosha...

yaani kuna vitu vyengine vidogo kweli watu wana complicate

utashindwaje ku deal na mumeo kwenye jambo dogo kama hilo?

utarudi kwenu utawaambia ambia vipi wazee? hamna sababu hata moja ya msingi

Hivi maana ya Gubu ni nini maana huyu dada kanambia kwa kifupi mme wangu ana gubu ..
 
FL1 naomba kukuuliza......Hapa tunatakiwa tumshauri nani? mwanamke? Sasa tukishamshauri utaenda kumwambia mwanamke tuliyomshauri? Sasa mwanaume aspobadili tabia, utakuja kutuomba tena tumshauri na yeye?:confused2::confused2:

Mnatakiwa mumpe mwanamke mbinu mbadala za kukaa na mmewe ...
 
huyu dada ni mpole sana, we ameshakuambia chakula chako si kitamu sasa kwann wajisumbua kupika?

Jamani, mwenzenu ndoa yake bado changa.. Akikataa kupika halafu akiachwa, mtasemaje?
 
Sioni kitu cha kumfanya aende nyumbani je angefumania:confused2:!ndoa ina mambo mengi jamani siyo smiling face muda wote,akae chini na mumewe kwa hekima aongee nae hayo mambo yanayomtatiza asikie response ya mumewe.Labda tu nikulize FL1,aliwahi kuongea nae chochote kuhusu hizo kero?pia amtoe housegal na akae bila msaidizi kwa muda unless kama ana mtoto mdogo.Swala la kukagua makabati sioni tatizo,amwache akague hata mara 3 kwa siku up to him.
 

Anadai alishaongea nae ila jamaa haelewi bado anapitia jikoni kukagua vitu na matabia yake mengine ndo maana akasema sijui mewe ana matatizo gani?
 
Anadai alishaongea nae ila jamaa haelewi bado anapitia jikoni kukagua vitu na matabia yake mengine ndo maana akasema sijui mewe ana matatizo gani?

Naona bado hajaongea nae inavyotakiwa hilo la kupekua jikoni linaweza kuwa sio ishu sana by the way huwa anaenda kupekua na HG akiwa yuko jikoni? FL1 mwambie wamuondee huyo HG kwanza nahisi hata hii tabia ya yeye kupekua huko jikoni itapungua maana inawezekana chanzo cha huo upekuzi ni huyo HG
 
Soma bold
Mwambie aongeze mshangao zaidi.
Asubiri siku aambayo wanakula tunda jamaa anamalizia huku akimtaja HG wao.

Endelea kushangaa mama wala usihofu
 

jamani tukumbuke kuwa hakuna formula ya maisha ambayo inafanana kwa watu wote, kila ndoa zina style yao ya maisha!kama huyo mwanaume anakagua makabati na kufanya vituko vingine hiyo ni style tu ya maisha!wapo wana ndoa wengine ambapo kazi ya nyumbani zimegawanywa sawa!mama akiwa anapika, baba anapiga deki na maisha yanasonga!
 

Bacha basi huko kupekua jikoni kwa huyo mwanaume kungekuwa kunaendana na yeye kuosha vyombo hapo ingekuwa poa ila nahisi huyu jamaa chanzo cha huo upekuzi ni huyo HG na ndio maana nikashauri aondolewe huyo HG tuone kama ataendelea kufanya hivyo hata kama mkewe akiwa jikoni kama akiacha basi chanzo ni huyo HG.
 

Mkuu FAINESTI.. HG ni kama mwanamke mwingine yeyote.. Cha muhimu, huyo mpekuaji huwa anapekuwa wakati HG yupo jikoni au? Maana sioni shida ya mtu kupekua nyumba yake, labda anatafuta PANYA au KOMBAMWIKO. Ila cha muhimu, Mke amuondoe HG haraka iwezekanavyo. Huwezi sifia chakula kinachopikwa na Beki tatu.. Hata kama ni kweli cha my wife wako ni kibaya..
 
Hivi maana ya Gubu ni nini maana huyu dada kanambia kwa kifupi mme wangu ana gubu ..

Gubu maana yake jamaa ana kero

Sasa hiyo kama nitabia yake kwa kweli kumbadilisha ni ngumu. Anachotakiwa kufanya ni ku-ignore mambo mengine. Kuingia jikoni kutizama chakula, ampuuze tu unless awe na wasi wasi na huyo msichana wa kazi.

kama ana wasi wasi huo, amuondoe tu, akae bila ya msaidizi kwa muda.
 

asante sana Gaijin hizi advice binti anzipata sambamba kabisa hapa
 
GUBU ni mapigo yatokanayo na maneno makali
unapigwa maneno mpaka unalia

Thanx Msanii najua maneno ni sumu kali unaweza kupewa neno moja ukawaza mpaka milenia tano zinaisha
 
Yaani kwa tatizo hili siku anakimbia anaweza kutana na mwenzake amsimulie ya kwake, then atarudi kwa mumewe fasta maana watu wana matatizo makubwa maar mia ya hilo na wapo kwa waume zao...
 
Thanx Msanii najua maneno ni sumu kali unaweza kupewa neno moja ukawaza mpaka milenia tano zinaisha
..Mke wangu ana gubu mpaka nduguze wanamhofia. ila mie nimezoea kucheza na nyoka wenye sumu naona burdani tu
 

Hapo na mimi ndio nataka kujua je ni wakati HG akiwa yuko jikoni au la? Maana nashindwa kuelewa ila nafikiri FL1 inabidi amuulize huyo rafiki yake hili swali.
 
Amtimue huoy housegal.....for starters....
 
Hapo na mimi ndio nataka kujua je ni wakati HG akiwa yuko jikoni au la? Maana nashindwa kuelewa ila nafikiri FL1 inabidi amuulize huyo rafiki yake hili swali.

Nitawakilisha
thanx
 
:lol::lol::lol::lol::lol::lol::lol::lol::lol::lol::lol::lol:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…