greater than
JF-Expert Member
- Sep 22, 2018
- 1,653
- 3,060
MAKALA YA 6
Karibuni tena katika Makala ya ujenzi. Leo tujifunze machache juu ya Udongo wa Mfinyanzi na Uhusiano wake katika Ujenzi1.Mfinyanzi ni moja kati aina kuu tatu za udongo.
-sifa aa Mfinyanzi
- Una Tanuka ukiwa na maji na kusinyaa ukikauka
- Una tunza maji(siyo rahisi maji kupenya)
- Una shika mana.
A.
-Chukua udongo wa kujaa kiganya
-Ulowanishe maji kidogo
-Tengeneza umbo la mpira (duara)
-Ukiona huo mpira umeshikamana bila hata kumong'onyoka ujue huo ni mfinyanzi
B.
-Chukua udongo kidogo
-ulowanishe maji
-Fikicha huo udongo kwenye vidole vyako
-Ukiona una nata nata ,basi huo ni mfinyanzi
C.
-Kama umefika kwenye eneo lako kipindi cha kiangazi,
-Ukaona kuna nyufa kwenye ardhi,ambapo hata kijiti kinapenya huo ni mfinyanzi
2.maeneo yenye udongo wa Mfinyanzi yapo ya aina mbili.
Maeneo yenye mfinyanzi mkali.
-udongo unakuwa una kiwango kikubwa cha Mfinyanzi.mfano
- Mbezi Juu na Makongo juu -wilaya ya Kinondoni
- MbeziLuis,Kimara,Goba,Kibamba,Kiluvya,Msigati -wilaya ya Ubungo
- Kinyerezi,Segerea - wilaya Ilaya
- Pugu Kajiungeni,Majohe,Buyuni,Msongola-Wilaya ya Ilala
- Bunju B ,Mabwe Pande - Wilaya ya Kinondoni.
- Chamazi,Mgeni Nani -wilaya ya Temeke
-Haumong'onyoki, hii ni kutokana na sifa ya punje sake kushikamana sana.
-Unazuia usambaaji wa mizizi ya miti karibu na jengo lako.
-Unatunza maji kwa mda mrefu,hii ni kutokana na sifa ya kutoruhusu maji kupenya
4.Hasara za Udongo wa mfinyanzi
-Ni ngumu kuchimba msingi au Shimo,kwahiyo mtu huingia gharama kubwa na mda mrefu kwenye kuchimba .
-Ngumu kuotesha mimea
-Haupo stable/imara kwenye kubeba msingi,hii ni kwakuwa unatanuka na kusinyaa.
5.Athari kubwa ya Ujenzi katika Udongo huu ni
Nyufa kwenye msingi na kuta
-Udongo karibia na msingi unapolowa maji kipindi cha mvua ,unatanuka
-Kuna upande Unatanuka sana kwenye kidogo.na kukandamiza msingi au kusukuma juu.
-kiangazi kikija,utasinyaa kwa viwango tofauti.
-Mabadiliko hayo hupelekea msingi kuvunja taratibu na kuweka nyufa au
-Kusukuma juu sehem ya jengo.
6.Athari nyinginee
Milango na madirisha kuwa migumu kufunga na kufungua
-sehemu moja ya jengo ipo juu,nyingine chino
Uwazi kuzunguka madirisha na Milango