1. Pole sana Mheshimiwa Mbowe kwa kukaa rumande kwa kipindi hicho chote. mambo mengi ya kifamilia, kiuchumi, kijamii na kisiasa yalikwama kwa sababu haukuwepo mtaani.
Sisi wafuasi na wapenda haki tuliumizwa sana kwa kuwa ilikuwa ni unyanyasaji wa wazi wa dola dhidi yako na wenzako bila hata chembe ya aibu.
Mungu atawalipa ktk hayo mliyopitia.
2. Hongera sana kwako na wenzako kwa kuwa mmeachiwa bila masharti na upande wenye dola umedhihirisha kuwa kesi yenu haikuwa na mashiko. Kwa maana nyingine wale wote waliojigamba na kukuchafua kabla hata ya kufika mahakamani wana deni kubwa la kulipa.
Kwa nchi zilizoendelea ktk mawanda ya demokrasia na uwajibikaji, leo hi viongozi kadhaa wangeachia nafasi zao.
3. Asante Mbowe na wenzako kwa kuwa kesi yenu imewafungua Watanzania wengi. Binafsi kila kesi iliposomwa nilikuwa nafuatilia kujua yaliyojiri.
Asanteni Mawakili Wasomi kwa kusimama kidete na kusimamia haki hata pale mlipooneshwa upendeleo wa waziwazi.
Zaidi ya yote Asante mhabaroshaji wetu uliyeweza kuandika neno baada ya neno kutoka mahakamani ukaweza kutuhabarisha sisi wananchi tuliotapakaa kila kona ya Dunia. Mungu atakulipa
Mwisho: Tuendelee kuchangia Chama kupitia ajenda ya Join the Chain, One Million Challange
Sisi wafuasi na wapenda haki tuliumizwa sana kwa kuwa ilikuwa ni unyanyasaji wa wazi wa dola dhidi yako na wenzako bila hata chembe ya aibu.
Mungu atawalipa ktk hayo mliyopitia.
2. Hongera sana kwako na wenzako kwa kuwa mmeachiwa bila masharti na upande wenye dola umedhihirisha kuwa kesi yenu haikuwa na mashiko. Kwa maana nyingine wale wote waliojigamba na kukuchafua kabla hata ya kufika mahakamani wana deni kubwa la kulipa.
Kwa nchi zilizoendelea ktk mawanda ya demokrasia na uwajibikaji, leo hi viongozi kadhaa wangeachia nafasi zao.
3. Asante Mbowe na wenzako kwa kuwa kesi yenu imewafungua Watanzania wengi. Binafsi kila kesi iliposomwa nilikuwa nafuatilia kujua yaliyojiri.
Asanteni Mawakili Wasomi kwa kusimama kidete na kusimamia haki hata pale mlipooneshwa upendeleo wa waziwazi.
Zaidi ya yote Asante mhabaroshaji wetu uliyeweza kuandika neno baada ya neno kutoka mahakamani ukaweza kutuhabarisha sisi wananchi tuliotapakaa kila kona ya Dunia. Mungu atakulipa
Mwisho: Tuendelee kuchangia Chama kupitia ajenda ya Join the Chain, One Million Challange