balozi SDG 10
Member
- Apr 17, 2024
- 8
- 8
Mbinguni kuna hukumu,amewaita manani
Malaika walo zamu,aridhi na samawini
Idadi wameshatimu,walo watu na majini
Umeonewa shetani?
Mikao ni kwa kaumu,watu wa zama fulani
mitume yao hashimu,ilotumwa duniani
Wamekaa kwa nidhamu,kikao kiso amani
Umeonewa shetani?
Mkuu wa mahakimu,aliyeketi enzini
Baada ya kusalimu,akaanza na shetani
Huyu bwana mdhalimu,aloleta tafarani
Umeonewa shetani?
Bwana shetwani rajimu,mkazi wa duniani
Upelekwe jahanamu,miaka ya sulemani
Kwa kosa la kuhujumu,kutia watu dhambini
Umeonewa shetani?
Machozi kwikwi za pumu,akigaa gaa chini
Imemzidi hukumu,anaomba afueni
Kulea ana jukumu,mama watoto nyumbani
Umeonewa shetani?
Utungo nime ukimu,jambo nawaelezeni
Yatawakuta magumu,mkijitia dhambini
Tuishini kwa nidhamu,haki usawa na dini
Umeonewa shetani?
#Mwl.Bakari
#Muungwana
Malaika walo zamu,aridhi na samawini
Idadi wameshatimu,walo watu na majini
Umeonewa shetani?
Mikao ni kwa kaumu,watu wa zama fulani
mitume yao hashimu,ilotumwa duniani
Wamekaa kwa nidhamu,kikao kiso amani
Umeonewa shetani?
Mkuu wa mahakimu,aliyeketi enzini
Baada ya kusalimu,akaanza na shetani
Huyu bwana mdhalimu,aloleta tafarani
Umeonewa shetani?
Bwana shetwani rajimu,mkazi wa duniani
Upelekwe jahanamu,miaka ya sulemani
Kwa kosa la kuhujumu,kutia watu dhambini
Umeonewa shetani?
Machozi kwikwi za pumu,akigaa gaa chini
Imemzidi hukumu,anaomba afueni
Kulea ana jukumu,mama watoto nyumbani
Umeonewa shetani?
Utungo nime ukimu,jambo nawaelezeni
Yatawakuta magumu,mkijitia dhambini
Tuishini kwa nidhamu,haki usawa na dini
Umeonewa shetani?
#Mwl.Bakari
#Muungwana