Polisi afariki dunia kwa kugongwa na lori akiwa kwenye pikipiki

Polisi afariki dunia kwa kugongwa na lori akiwa kwenye pikipiki

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Askari polisi wa Kituo cha Kibaya wilayani Kiteto Mkoa wa Manyara, Geogre Mwakambonjo (40) amefariki dunia baada ya kugongwa na lori alipokuwa amepanda kwenye pikipiki.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ahmed Makarani amesema tukio hilo limetokea leo Jumanne Desemba 24 mwaka 2024.

Kamanda Makarani ameeleza kuwa askari polisi huyo amefariki dunia baada ya kugongwa na lori akiwa amepakizwa kwenye pikipiki.

Ameeleza kuwa, askari polisi huyo, amepata ajali hiyo eneo la Msasani, Kata ya Maisaka mjini Babati kwenye barabara kuu ya Arusha - Dodoma.

Kamanda Makarani amesema chanzo cha kifo cha askari huyo ni uzembe wa dereva aliyekuwa anaendesha lori kwa kutokuwa makini.
IMG_1988.jpeg
 
Uyo pichani hana miaka 40.
kwanini asiwe na 40 amezidisha au amepunguza..inamaana ww unabishana na waajiri wake ambao wana cheti chake cha kuzaliwa,vyeti vya O'leve au chuo pia hata NIDA yake..kuna watu wana umri mkubwa lakini wanaonekana wadogo kimtizamo wanang'aa hii kutokana labda wana maisha mazuri kwao hawana njaa ila wengine kuonekana wakubwa kiumri na wamekomaa hawana nuru yote sababu ya dhiki na umaskini
 
kwanini asiwe na 40 amezidisha au amepunguza..inamaana ww unabishana na waajiri wake ambao wana cheti chake cha kuzaliwa,vyeti vya O'leve au chuo pia hata NIDA yake..kuna watu wana umri mkubwa lakini wanaonekana wadogo kimtizamo wanang'aa hii kutokana labda wana maisha mazuri kwao hawana njaa ila wengine kuonekana wakubwa kiumri na wamekomaa hawana nuru yote sababu ya dhiki na umaskini
I don't speak for the dead.. Nenda kamzike askari mwenzio acha povu.
 
I don't speak for the dead.. Nenda kamzike askari mwenzio acha povu.
ww ndio uwache povu hao waliotaja umri wake ndio wenye access na taarifa zake..sio ww eti unabana pua kabisa ooh huyo hana 40 utadhani ulimzaa ww kwa ujuaji wako wa kishamba..kajambe mbele kule..
 
Back
Top Bottom