Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia na kumhoji aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Uenyekiti katika mtaa wa Buswelu A kupitia CHADEMA, Pastory Apolinary Sililo anayedaiwa kuwa alitekwa na watu wasiojulikana.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa amesema mnano tarehe 26 mwezi huu, mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Victoria, Ezekia Wenje alionekana kwenye vyombo vya habari akitoa taarifa ya kutoweka kwa mgombea huyo, huku akidai alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na kwamba ametekwa na maisha yake yapo hatarini na kuliomba Jeshi la Polisi kumtafuta mgombea huyo.
Pia soma: LGE2024 - Mgombea CHADEMA adaiwa kutekwa Polisi kuingia mzigoni kuanza kufuatilia
Kamanda Mutafungwa amesema kabla Wenje hajatoa taarifa hiyo tayari tukio hilo lilikuwa limesharipotiwa katika kituo cha Polisi Buswelu kwamba mgombea huyo hajulikani alipo, na upelelezi ulianza mara moja kwa kuwahoji watu mbalimbali akiwemo mke wake.
Aidha, Kamanda Mutafungwa amesema walipomhoji afisa mtendaji wa mtaa wa Buswelu A, Godso Mkama alisema mgombea huyo hajatekwa ambapo alieleza kuwa mgombea huyo alimwambia kuwa hawezi kugombea tena na kwamba anajiondoa kwenye mchakato na kusema ataondoka kwenye mtaa huo hadi mchakato wa uchaguzi utakapokamilika ndipo akaenda kujificha mtaa wa Buhila A, wilayani Ilemela kwa ndugu yake aitwaye Zaituni Selemani Misonge anapodaiwa kujificha tangu Novemba 25 hadi alipokamatwa na Polisi.
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Kamanda Mutafungwa amesema baada ya kukamatwa amekanusha kutekwa na kusema alijificha ili kukwepa kugombea nafasi hiyo ya uenyekiti, mbali na mgombea huyo pia Jeshi la Polisi linawashikilia ndugu zake, Zaituni Selemani Misonge na Aneth Joshua Bumale.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia na kumhoji aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Uenyekiti katika mtaa wa Buswelu A kupitia CHADEMA, Pastory Apolinary Sililo anayedaiwa kuwa alitekwa na watu wasiojulikana.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa amesema mnano tarehe 26 mwezi huu, mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Victoria, Ezekia Wenje alionekana kwenye vyombo vya habari akitoa taarifa ya kutoweka kwa mgombea huyo, huku akidai alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na kwamba ametekwa na maisha yake yapo hatarini na kuliomba Jeshi la Polisi kumtafuta mgombea huyo.
Pia soma: LGE2024 - Mgombea CHADEMA adaiwa kutekwa Polisi kuingia mzigoni kuanza kufuatilia
Kamanda Mutafungwa amesema kabla Wenje hajatoa taarifa hiyo tayari tukio hilo lilikuwa limesharipotiwa katika kituo cha Polisi Buswelu kwamba mgombea huyo hajulikani alipo, na upelelezi ulianza mara moja kwa kuwahoji watu mbalimbali akiwemo mke wake.
Aidha, Kamanda Mutafungwa amesema walipomhoji afisa mtendaji wa mtaa wa Buswelu A, Godso Mkama alisema mgombea huyo hajatekwa ambapo alieleza kuwa mgombea huyo alimwambia kuwa hawezi kugombea tena na kwamba anajiondoa kwenye mchakato na kusema ataondoka kwenye mtaa huo hadi mchakato wa uchaguzi utakapokamilika ndipo akaenda kujificha mtaa wa Buhila A, wilayani Ilemela kwa ndugu yake aitwaye Zaituni Selemani Misonge anapodaiwa kujificha tangu Novemba 25 hadi alipokamatwa na Polisi.
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Kamanda Mutafungwa amesema baada ya kukamatwa amekanusha kutekwa na kusema alijificha ili kukwepa kugombea nafasi hiyo ya uenyekiti, mbali na mgombea huyo pia Jeshi la Polisi linawashikilia ndugu zake, Zaituni Selemani Misonge na Aneth Joshua Bumale.