Polisi Geita wachangia damu, kuadhimisha miaka 60

Polisi Geita wachangia damu, kuadhimisha miaka 60

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi hilo, wamechangia damu kwa ajili ya kuwasaidia wananchi pindi wanapopata Changamoto za uhitaji wa damu katika Wilaya ya Mbogwe Mkoa wa Geita.

Kamishna Msaidizi wa Polisi ACPMagai Chassa amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita limetumia maadhimisho hayo kuikumbuka benki ya damu salama ambapo wamechangia damu kwa ajili ya benki hiyo pia kufanya matembezi ya hiari kwa kushirikiana na Wananchi kwa lengo la kufikisha ujumbe kuhusiana na masuala ya uhalifu.
e0a3924c-5b30-424a-93da-7c322d2a9652.jpg

7c564c14-7a0e-4834-8c81-def4764f405b.jpg
ACP Chassa ameendelea kufafanua kuwa kilele cha maadhimisho hayo kitaifa kitakua Septemba 17 mwaka huu huko Mkoani Kilimanjaro ambapo kwa mkoa wa Geita walikutana na makundi mbalimbali ikiwemo wanafunzi, bodaboda, nyumba za ibada na vyombo vya habari kwa ajili ya kutoa elimu juu ya wananchi kujiepusha na vitendo vya uhalifu.

Maadhimisho hayo yanaenda na kauli mbiu ‘’Huduma Bora za Kipolisi kwa Umma zinapatikana kwa kubadilika kifikra, Usimamizi wa Sheria na Matumizi ya TEHEMA’.
00efcf58-e91c-40d3-8028-54660d36b6bc.jpg
 
Oooh! Kuchangia damu ni kitendo cha kiungwana sana ni sawa na kuokoa uhai wa mtu..

kukiwa na hamasa ya uchangiaji damu itasaidia kuondokana na gharama za kulipia damu wakati wa tatizo.

" Polisi acheni kutumika vibaya kisiasa mnatukosea wananchi"
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi hilo, wamechangia damu kwa ajili ya kuwasaidia wananchi pindi wanapopata Changamoto za uhitaji wa damu katika Wilaya ya Mbogwe Mkoa wa Geita.

Kamishna Msaidizi wa Polisi ACPMagai Chassa amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita limetumia maadhimisho hayo kuikumbuka benki ya damu salama ambapo wamechangia damu kwa ajili ya benki hiyo pia kufanya matembezi ya hiari kwa kushirikiana na Wananchi kwa lengo la kufikisha ujumbe kuhusiana na masuala ya uhalifu.
ACP Chassa ameendelea kufafanua kuwa kilele cha maadhimisho hayo kitaifa kitakua Septemba 17 mwaka huu huko Mkoani Kilimanjaro ambapo kwa mkoa wa Geita walikutana na makundi mbalimbali ikiwemo wanafunzi, bodaboda, nyumba za ibada na vyombo vya habari kwa ajili ya kutoa elimu juu ya wananchi kujiepusha na vitendo vya uhalifu.

Maadhimisho hayo yanaenda na kauli mbiu ‘’Huduma Bora za Kipolisi kwa Umma zinapatikana kwa kubadilika kifikra, Usimamizi wa Sheria na Matumizi ya TEHEMA’.
Waletwe Dar kuongeza nguvu ya kuwakabili CHADEMA tarehe 23/09/2024
 
Shida sasa,utakuta asilimia 70 ya damu iliyochangiwa inakuwa disposed.Hongereni
 
Back
Top Bottom