Polisi Iache Kujihusisha na Siasa..CCM Haitatawala Milele and so is CHADEMA and others

Polisi Iache Kujihusisha na Siasa..CCM Haitatawala Milele and so is CHADEMA and others

Elly B

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2011
Posts
1,194
Reaction score
906
Binafsi, kama ilivyo kwa wananchi wengi wa nchi hii, naendelea kusikitishwa na tabia ya Polisi kutumiwa na Serikali kwa maslahi ya CCM. Tabia hii siyo tu inawakosesha wengine haki, bali inafanya wananchi wakose Imani na uadilifu wa Polisi ilinayotakiwa kulinda usalama wa raia na mali zao (siyo chama na mali zake).

Siku za karibuni kumeibuka tabia ya ajabu ya watu kubambikiwa kesi kwa maslahi ya chama tawala au wakati mwingine kwa lengo la kuficha aibu ya kushindwa kazi yao.

Tumeona jinsi kesi ya utekaji wa Dr.Ulimboka ilivyokuwa na mafinyufinyu ya aina yake tangu kukamatwa kwa Mulundi kule Kawe. Kwa mtu wa kawaida kabisa ilikuwa ni ngumu kuanza kuamini acha kuelewa, kuwa mtu atatoka Kenya na kujua Mabwepande iko wapi, kwa Ulimboka ni wapi, anatumia namba gani na anatembela viwanja gani. Na hasa atoke kwao kuja kumteka Dr. Ulimboka kwa baya lipi alilowatendea Wakenya? Ni wazi kama nilivyowahi kusema siku za nyuma hii ilikuwa ni njia ya kuwapumbaza wananchi wa nchi hii, ambao wamezoeleka kwa kusahau haraka mara baada ya kuzuka jambo jipya. Kwa hiyo wana imani sasa wameshasahau kila kitu! Hata baada ya mahakama kuthibitisha kuwa Mulundi Joshua hana hatia bado Polisi haioni aibu kwa tabia yake ya ajabu! Ni vema ikakumbukwa kulikuwa na tume ya IGP ambayo mpaka leo haijatoa majibu kama ilivyoahidiwa. Mimi nadhani ni muda muafaka kwa polisi kuwaambia wananchi ni nani alimteka Dr.Ulimboka kama Mulundi hana hatia. Vinginevyo Wananchi hawataona ni uwongo kuwa serikali ina mkono katika zoezi lile. Vinginevyo ni kwa nini hiyo tume au hata CID wasimhoji Dr. Ulimboka mpaka leo?

Halafu kuna hili la Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri, Absalom Kibanda kutekwa na kuumizwa vibaya. Kuna ushahidi wa kuonyesha kuna mkono wa dola hata nyuma ya zoezi lile kwani Absalom alishapata kutahadharishwa mapema na alikuwa tayari kutoa ushirikiano. Mbona hatuoni maendeleo ya lolote? Ni kweli polisi ya Tanzania ni hopeless kiasi cha kushindwa kumpata hata mhalifu mmoja wa hayo matukio?

Siku za hivi karibuni kumekuja hili la Ugaidi! Ni ajabu kuwa kila anayekamatwa anatoka mahabusu na kulalamikia kuteswa huku akilazimishwa kukubali kuwa Mwenyekiti, Katibu au wengineo katika CHADEMA ni Waratibu wa mipango ya ugaidi. Wengine utasikia wanasema hadharani walikamatwa na makosa mengine na kuunganishwa na kesi za ugaidi eti kwa sababu una namba ya mtu wa CHADEMA! Kesi zote zikipelekwa mahakamani zinafutwa kwa kutokidhi vigezo vya Ugaidi. Hivi ni kweli ofisi ya DPP na DCI zimeshindwa kubaini ukweli wa mashtaka au kuna shinikizo nyuma ya hayo mahsitaka? Ni kweli DPP ameshindwa kuelewa sheria kiasi cha kushindwa kupambanua ni kesi ipi ni ya jinai na ipi ni ya Ugaidi? Siamini hilo. Ninachoona ni muendelezo tu wa tabia ya kubebeshana kesi feki.

Na kuna hii tabia ya aibu kabisa iliyozaliwa siku hizi ya polisi kumkamata mtuhumiwa, kumpiga mpaka kumwua na kutelekeza maiti bila hata kuwataarifu ndugu zake. Hivi ni nani aliyesema ukiwa polisi unakuwa siyo binadamu tena?
Labda ni kweli huyo ni mhalifu, lakini ni kwa nini asifikishwe mahakamani ahukumiwe kwa sheria kuliko kumpa hukumu bila kuzingatia uzito wa kosa wala sheria? kuna tofauti gani sasa kati ya polisi wanaoua watuhumiwa na raia wanaoua wahalifu bila kuwapeleka kwenye vyombo husika? Hii ni aibu kwa jeshi la polisi.

Ni wazi wanaobambikwa kesi ni wengi kuliko tunavyoweza kusikia kwani siyo wote wamepata nafasi ya kutoka mahabusu, Siyo wengi wanapata dhamana na ni wachache wanaoweza kushauriwa na mawakili.

Kinachonistua ni hii hali ninayoona ya kuwa wote walotekwa na wote walibambikwa kesi wana mwelekeo mmoja wa kukosoa seriakli aidha kwa magazeti yao na vyombo vya habari au kwenye majukwaa ya siasa, jambo ambalo linafanya niamini kuwa hakuna la ziada zaidi ya serikali kutumia polisi kunyamazisha upinzani, kudumaza demokrasia na kuzuia huru wa kupashana habari. Nilitegemea katika jamii ya watu wastaarabu ,mtu anapotoa tuhuma atatakiwa azithibitishe. akishindwa mahakama ziko wazi. Hii tunayofanya ni tabia ya kuonea aibu kwani si ya kibinadamu na haiendani na jinsi jumuiya ya kimataifa inavyotuchukulia.

Na labda mimi ndiyo nakosea kufikiria au uelewa wangu ni mdogo. Basi ni kwa nini Polisi isikanushe tuhuma zote kuwa haihusiki na hayo?


Nimalizie na kuwakumbusha polisi kuwa wana wajibu wa kuwatumikia wananchi. Siyo vyama vya siasa. Na hapa ninamaanisha hawapaswi kitumikia CCM leo, wala chama chochote kesho, kwani kwa kufanya hivyo polisi inachagua kuwabagua wengine na hii ni kuvunja katiba na haki za wasi wa vyama hivyo na za wasio na vyama kabisa. Na haina tija sana kwani hakuna chama kitakachotawala milele ingawa Wananchi watakuwepo milele! Kwa hiyo kitu pekee polisi inaweza kufanya kurudisha imani ya wanachi iliyopotea ni kuacha kutumika kwa mslahi ya kisiasa. Polisi ifanye kazi ya ulinzi kama inavyotegemewa. Iache vyama vya siasa vifanye siasa. Polisi iwe wazi kuwa imezidiwa na haina uwezo wa kupambana na wahalifu badala ya kuwadanganya wanachi waliwaajiri na wanowalipa mishahara kwa kodi za jasho lao, kwa kuwabambika kesi watu wengine ili wananchi waridhike ilihali siyo kweli. Hii ni aibu kwa jeshi la polisi na kukosa uadilifu kwa kiwango kikubwa. Na kwa mtindo huu wa sasa polisi itegemee nini kutoka kwa wananchi?
 
Chadema mnapanga maandamano nyie jioni ikifika mnapokelewa na wake zenu na watoto mkiwa na mkate na sukari, sisi tulioandamana ikifika jioni tunaingia nyumbani tukiwa tunajificha na ukuta hadi kitandani tunawaacha watoto wakipiga miayo sebuleni wakimngojea baba atoke kazini, kumbe baba alikuwa anarukaruka huko njiani na bendera, siwi tena mtumwa wa bendera , sasa hivi ninafanya kazi
 
Chadema mnapanga maandamano nyie jioni ikifika mnapokelewa na wake zenu na watoto mkiwa na mkate na sukari, sisi tulioandamana ikifika jioni tunaingia nyumbani tukiwa tunajificha na ukuta hadi kitandani tunawaacha watoto wakipiga miayo sebuleni wakimngojea baba atoke kazini, kumbe baba alikuwa anarukaruka huko njiani na bendera, siwi tena mtumwa wa bendera , sasa hivi ninafanya kazi


kababu inaoneka ww ni mpezi sana wa kababu!
 
unaweza kutaja polisi ambao wanakadi za vyama vya siasa na namba za hizo kadi au unaandika tu kwa sababu wazee wamekutuma kuandika hivyo.
 
Chadema mnapanga maandamano nyie jioni ikifika mnapokelewa na wake zenu na watoto mkiwa na mkate na sukari, sisi tulioandamana ikifika jioni tunaingia nyumbani tukiwa tunajificha na ukuta hadi kitandani tunawaacha watoto wakipiga miayo sebuleni wakimngojea baba atoke kazini, kumbe baba alikuwa anarukaruka huko njiani na bendera, siwi tena mtumwa wa bendera , sasa hivi ninafanya kazi

Jaribu kuelewa hoja ndugu yangu. Sioni kama hilo la maandamano linahusiana na tabia ya polisi kushindwa kutenda haki! Wala sidhani kuwa ni sahihi wewe kudhani kila anayeposti thread humu ni CHADEMA. Think out of the box. Otherwise ukinyamaza tu watu hawatajua hayo ndiyo mawazo yako!
 
unaweza kutaja polisi ambao wanakadi za vyama vya siasa na namba za hizo kadi au unaandika tu kwa sababu wazee wamekutuma kuandika hivyo.

Simiyu Yetu,

Nadhani umeuliza kwa kukurupuka. Sijasema polisi wana kadi za chama chochote. Nimesema Polisi iache kujihusisha na siasa ili iwape wananchi wote (Wa CCM na Wasio CCM) haki. Kwani wewe unaona kuna uhalali gani na hayo inayotuhumiwa polisi? Sijui tunaelewana vile?

Na ni kwa nini kila unapotokea kuchangia mada yoyote humu huwa unachangia pumba nyepesi. Una tatizo gani mwenzetu? Ukiona jambo haunalo hoja siyo vibaya ukaliacha lipite! Otherwise kujibu bila hoja ni kufanya watu wakudharau
 
Chadema mnapanga maandamano nyie jioni ikifika mnapokelewa na wake zenu na watoto mkiwa na mkate na sukari, sisi tulioandamana ikifika jioni tunaingia nyumbani tukiwa tunajificha na ukuta hadi kitandani tunawaacha watoto wakipiga miayo sebuleni wakimngojea baba atoke kazini, kumbe baba alikuwa anarukaruka huko njiani na bendera, siwi tena mtumwa wa bendera , sasa hivi ninafanya kazi

mkuu vijana wangeiga mfano tungepiga hatua mapema hawa wanasiasa wengine wahuni tu wanatumia watu kutafuta umarufa halafu hawana msaada kwa watu wanaowatumia.
 
Binafsi, kama ilivyo kwa wananchi wengi wa nchi hii, naendelea kusikitishwa na tabia ya Polisi kutumiwa na Serikali kwa maslahi ya CCM. Tabia hii siyo tu inawakosesha wengine haki, bali inafanya wananchi wakose Imani na uadilifu wa Polisi ilinayotakiwa kulinda usalama wa raia na mali zao (siyo chama na mali zake).

Siku za karibuni kumeibuka tabia ya ajabu ya watu kubambikiwa kesi kwa maslahi ya chama tawala au wakati mwingine kwa lengo la kuficha aibu ya kushindwa kazi yao.

Tumeona jinsi kesi ya utekaji wa Dr.Ulimboka ilivyokuwa na mafinyufinyu ya aina yake tangu kukamatwa kwa Mulundi kule Kawe. Kwa mtu wa kawaida kabisa ilikuwa ni ngumu kuanza kuamini acha kuelewa, kuwa mtu atatoka Kenya na kujua Mabwepande iko wapi, kwa Ulimboka ni wapi, anatumia namba gani na anatembela viwanja gani. Na hasa atoke kwao kuja kumteka Dr. Ulimboka kwa baya lipi alilowatendea Wakenya? Ni wazi kama nilivyowahi kusema siku za nyuma hii ilikuwa ni njia ya kuwapumbaza wananchi wa nchi hii, ambao wamezoeleka kwa kusahau haraka mara baada ya kuzuka jambo jipya. Kwa hiyo wana imani sasa wameshasahau kila kitu! Hata baada ya mahakama kuthibitisha kuwa Mulundi Joshua hana hatia bado Polisi haioni aibu kwa tabia yake ya ajabu! Ni vema ikakumbukwa kulikuwa na tume ya IGP ambayo mpaka leo haijatoa majibu kama ilivyoahidiwa. Mimi nadhani ni muda muafaka kwa polisi kuwaambia wananchi ni nani alimteka Dr.Ulimboka kama Mulundi hana hatia. Vinginevyo Wananchi hawataona ni uwongo kuwa serikali ina mkono katika zoezi lile. Vinginevyo ni kwa nini hiyo tume au hata CID wasimhoji Dr. Ulimboka mpaka leo?

Halafu kuna hili la Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri, Absalom Kibanda kutekwa na kuumizwa vibaya. Kuna ushahidi wa kuonyesha kuna mkono wa dola hata nyuma ya zoezi lile kwani Absalom alishapata kutahadharishwa mapema na alikuwa tayari kutoa ushirikiano. Mbona hatuoni maendeleo ya lolote? Ni kweli polisi ya Tanzania ni hopeless kiasi cha kushindwa kumpata hata mhalifu mmoja wa hayo matukio?

Siku za hivi karibuni kumekuja hili la Ugaidi! Ni ajabu kuwa kila anayekamatwa anatoka mahabusu na kulalamikia kuteswa huku akilazimishwa kukubali kuwa Mwenyekiti, Katibu au wengineo katika CHADEMA ni Waratibu wa mipango ya ugaidi. Wengine utasikia wanasema hadharani walikamatwa na makosa mengine na kuunganishwa na kesi za ugaidi eti kwa sababu una namba ya mtu wa CHADEMA! Kesi zote zikipelekwa mahakamani zinafutwa kwa kutokidhi vigezo vya Ugaidi. Hivi ni kweli ofisi ya DPP na DCI zimeshindwa kubaini ukweli wa mashtaka au kuna shinikizo nyuma ya hayo mahsitaka? Ni kweli DPP ameshindwa kuelewa sheria kiasi cha kushindwa kupambanua ni kesi ipi ni ya jinai na ipi ni ya Ugaidi? Siamini hilo. Ninachoona ni muendelezo tu wa tabia ya kubebeshana kesi feki.

Na kuna hii tabia ya aibu kabisa iliyozaliwa siku hizi ya polisi kumkamata mtuhumiwa, kumpiga mpaka kumwua na kutelekeza maiti bila hata kuwataarifu ndugu zake. Hivi ni nani aliyesema ukiwa polisi unakuwa siyo binadamu tena?
Labda ni kweli huyo ni mhalifu, lakini ni kwa nini asifikishwe mahakamani ahukumiwe kwa sheria kuliko kumpa hukumu bila kuzingatia uzito wa kosa wala sheria? kuna tofauti gani sasa kati ya polisi wanaoua watuhumiwa na raia wanaoua wahalifu bila kuwapeleka kwenye vyombo husika? Hii ni aibu kwa jeshi la polisi.

Ni wazi wanaobambikwa kesi ni wengi kuliko tunavyoweza kusikia kwani siyo wote wamepata nafasi ya kutoka mahabusu, Siyo wengi wanapata dhamana na ni wachache wanaoweza kushauriwa na mawakili.

Kinachonistua ni hii hali ninayoona ya kuwa wote walotekwa na wote walibambikwa kesi wana mwelekeo mmoja wa kukosoa seriakli aidha kwa magazeti yao na vyombo vya habari au kwenye majukwaa ya siasa, jambo ambalo linafanya niamini kuwa hakuna la ziada zaidi ya serikali kutumia polisi kunyamazisha upinzani, kudumaza demokrasia na kuzuia huru wa kupashana habari. Nilitegemea katika jamii ya watu wastaarabu ,mtu anapotoa tuhuma atatakiwa azithibitishe. akishindwa mahakama ziko wazi. Hii tunayofanya ni tabia ya kuonea aibu kwani si ya kibinadamu na haiendani na jinsi jumuiya ya kimataifa inavyotuchukulia.

Na labda mimi ndiyo nakosea kufikiria au uelewa wangu ni mdogo. Basi ni kwa nini Polisi isikanushe tuhuma zote kuwa haihusiki na hayo?


Nimalizie na kuwakumbusha polisi kuwa wana wajibu wa kuwatumikia wananchi. Siyo vyama vya siasa. Na hapa ninamaanisha hawapaswi kitumikia CCM leo, wala chama chochote kesho, kwani kwa kufanya hivyo polisi inachagua kuwabagua wengine na hii ni kuvunja katiba na haki za wasi wa vyama hivyo na za wasio na vyama kabisa. Na haina tija sana kwani hakuna chama kitakachotawala milele ingawa Wananchi watakuwepo milele! Kwa hiyo kitu pekee polisi inaweza kufanya kurudisha imani ya wanachi iliyopotea ni kuacha kutumika kwa mslahi ya kisiasa. Polisi ifanye kazi ya ulinzi kama inavyotegemewa. Iache vyama vya siasa vifanye siasa. Polisi iwe wazi kuwa imezidiwa na haina uwezo wa kupambana na wahalifu badala ya kuwadanganya wanachi waliwaajiri na wanowalipa mishahara kwa kodi za jasho lao, kwa kuwabambika kesi watu wengine ili wananchi waridhike ilihali siyo kweli. Hii ni aibu kwa jeshi la polisi na kukosa uadilifu kwa kiwango kikubwa. Na kwa mtindo huu wa sasa polisi itegemee nini kutoka kwa wananchi?

Mkuu kwa mfumo uliopo sasa ni ngumu sana majeshi yote tuliyonayo yakafanya kazi pasipo kutumika na wana siasa. Hapa ni kutokana na mapungufu kwenye katiba tulionao sasa. Tunawalaumu bure tu hawa polisi au hata majeshi mengine. Wakuu wa hizi taasisi zote wanateuliwa na mtawala aliye madarakani hivyo hawana jinsi zaidi ya kuchukua na kufuata maelekezo ya mtawala.

Kikubwa hapa ni hiyo katiba mpya kuyaona haya mapungufu na kuyafanyia kazi ili kama tukipata katiba mpya basi suala hili la majeshi kuwatumikia wananchi na wala sio vyama na watawala litakuwa limepata ufumbuzi.
 
Chadema mnapanga maandamano nyie jioni ikifika mnapokelewa na wake zenu na watoto mkiwa na mkate na sukari, sisi tulioandamana ikifika jioni tunaingia nyumbani tukiwa tunajificha na ukuta hadi kitandani tunawaacha watoto wakipiga miayo sebuleni wakimngojea baba atoke kazini, kumbe baba alikuwa anarukaruka huko njiani na bendera, siwi tena mtumwa wa bendera , sasa hivi ninafanya kazi

Jiandae, maana unatumika sijui utarekodiwa lini??? maana mliwakamata Wana CDM mkaanda na waandishi wa uhuru na Mzalendo kwa ajili ya kurekodi kama wana CDM hawa wangesema kwa shinikizo kuwa viongozi wetu wanafanya ugaidi. Milion 30 na U-DC vimeshindwa ku-work.

Mmelaaniwa. siku hizi siamini taarifa yoyote ya POLICE. Siku za nyuma watu wengi wameuawa kwa kisingizio cha walikuwa wanarushiana RISASI na police kumbe yaweza kuwa kinyume.
 
Mkuu kwa mfumo uliopo sasa ni ngumu sana majeshi yote tuliyonayo yakafanya kazi pasipo kutumika na wana siasa. Hapa ni kutokana na mapungufu kwenye katiba tulionao sasa. Tunawalaumu bure tu hawa polisi au hata majeshi mengine. Wakuu wa hizi taasisi zote wanateuliwa na mtawala aliye madarakani hivyo hawana jinsi zaidi ya kuchukua na kufuata maelekezo ya mtawala.

Kikubwa hapa ni hiyo katiba mpya kuyaona haya mapungufu na kuyafanyia kazi ili kama tukipata katiba mpya basi suala hili la majeshi kuwatumikia wananchi na wala sio vyama na watawala litakuwa limepata ufumbuzi.

Nakubaliana na wewe asilimia zote. Ninajua ni vipi kwao ni ngumu. Lakini hakutakuja nafuu kwa wao kukaa kimya tu. Ni kati ya mambo ambayo ningependa wayashikiea kidedea kwenye katiba mpya! Hii ni changamoto kwao kama wanakubali. Vinginevyo watendelea kujenga gap kati yao na wananchi.
 
Simiyu Yetu,

Nadhani umeuliza kwa kukurupuka. Sijasema polisi wana kadi za chama chochote. Nimesema Polisi iache kujihusisha na siasa ili iwape wananchi wote (Wa CCM na Wasio CCM) haki. Kwani wewe unaona kuna uhalali gani na hayo inayotuhumiwa polisi? Sijui tunaelewana vile?

Na ni kwa nini kila unapotokea kuchangia mada yoyote humu huwa unachangia pumba nyepesi. Una tatizo gani mwenzetu? Ukiona jambo haunalo hoja siyo vibaya ukaliacha lipite! Otherwise kujibu bila hoja ni kufanya watu wakudharau

tupe uthibitisho kuwa polisi wanajihusisha na siasa mimi nilijua kujihusisha na siasa ni pamoja na kuwa mwanachama wa chama fulani sas wewe unauthibitisho gani au ni ule mpango wa kibavicha wakuandika vitu ambavyo havina uthibitisho.
 
tupe uthibitisho kuwa polisi wanajihusisha na siasa mimi nilijua kujihusisha na siasa ni pamoja na kuwa mwanachama wa chama fulani sas wewe unauthibitisho gani au ni ule mpango wa kibavicha wakuandika vitu ambavyo havina uthibitisho.

Simiyu yenu,

Soma Posti ya msingi. imejibu yote hayo. Ndiyo maana nikasema umekurupuka hujasoma ukaelewa!

But No offence
 
jiandae, maana unatumika sijui utarekodiwa lini??? Maana mliwakamata wana cdm mkaanda na waandishi wa uhuru na mzalendo kwa ajili ya kurekodi kama wana cdm hawa wangesema kwa shinikizo kuwa viongozi wetu wanafanya ugaidi. Milion 30 na u-dc vimeshindwa ku-work.

Mmelaaniwa. Siku hizi siamini taarifa yoyote ya police. Siku za nyuma watu wengi wameuawa kwa kisingizio cha walikuwa wanarushiana risasi na police kumbe yaweza kuwa kinyume.

utasubiri unayosema mpaka uzeeke na umasikini wako ukimsuburia kababu atoe record, mimi maisha yanaendambele nachapa kazi kwa kwenda mbele, hata leo niko kazini, njoo arusha tuchape kazi mwana, niko hapa hapa nina reply booking, nice time
 
unaweza kutaja polisi ambao wanakadi za vyama vya siasa na namba za hizo kadi au unaandika tu kwa sababu wazee wamekutuma kuandika hivyo.

Wapo baadhi ya wakuu wa mikoa na Wilaya ambao ni askari,na hicho ndicho kinawafanya wanafanya kazi kisiasa huku wakitegemea kupewa vyeo vya ukuu wa wilaya na mkoa au ubalozi. Na wakipewa moja kwa moja ni makada wa ccm. Huo ni ushahidi tosha kuwa majeshi yetu yanaendeshwa kisiasa. Mfano wa watu hao ni Adadi Rajabu, Shimbo,Simbakalia,na wengine wengi tu. Kwa hapo tu huwezi kutenganisha CCM na majeshi yetu.Ukweli wanatumika sana na CCM kwa fadhila hizo.
 
Back
Top Bottom