Polisi Mbeya wamkamata Joseph Ngoya akiwa na noti bandia za Tsh. 10,000

Polisi Mbeya wamkamata Joseph Ngoya akiwa na noti bandia za Tsh. 10,000

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia JOSEPH NGOYA mwenye umri wa miaka 34, Mkazi wa Mbozi Mkoa wa Songwe kwa tuhuma za kupatikana na Noti bandia za shilingi elfu kumi.

Kuzaga.JPG

Ni kwamba mnamo tarehe 23.02.2023 huko maeneo ya Kituo cha Mafuta (Sheli) ya Kazibure iliyopo barabara Kuu (Tunduma Road) katika Mji mdogo wa Mbalizi mtuhumiwa alikamatwa akiwa na karatasi 15 alizozikata kwa mfano wa noti ya TSH 10,000/= akiwa katika harakati ya kuziingiza kwenye mzunguko.

Mtuhumiwa amehojiwa amekiri kujihusisha na matukio ya utapeli katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya.
 
Back
Top Bottom