Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limetoa sababu ya kuendelea kumshikilia bondia maarufu nchini Hassan Mwakinyo (29), anaetuhumiwa kumshambulia mkazi wa jijini Tanga Mussa Ally akimtuhumu kuwa ni mwizi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Jumatatu Machi 10,2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi amesema Mwakinyo anatuhumiwa kumshambulia na kumjeruhi Mussa Ally ambae anadai ni mvuvi alipopita kwenye makazi yake.
Kamanda huyo amesema uchunguzi utakapokamilika atatoa taarifa kwa vyombo vya habari ikiwa ni sambamba na kumfikisha mahakamani ili ajibu tuhuma zitakazomkabili.
Amesema wamemkamata kwa tuhuma za kumjeruhi mvuvi, ambapo ni tuhuma za jinai mtu yeyote akifanya makosa kama hayo bila kuangalia nafasi yake kwenye jamii, anatakuwa kuchukuliwa hatua za kisheria na suala la umaarufu haliwezi kubadili kile kilichotendeka.
"Jeshi la polisi Mkoa wa Tanga linamshikilia Hassan Mwakinyo (29) mkazi wa Sahare jijini Tanga kwa kumshambulia na kumjeruhi Mussa Ally mkazi wa eneo hilo ambae ni mvuvi,uchunguzi wa tukio hili unaendelea na ukikamilika mtuhumiwa atapelekwa mahakamani," amesema Mchunguzi.
Soma, Pia
Amesema wamemkamata kwa tuhuma za kumjeruhi mvuvi, ambapo ni tuhuma za jinai mtu yeyote akifanya makosa kama hayo bila kuangalia nafasi yake kwenye jamii, anatakuwa kuchukuliwa hatua za kisheria na suala la umaarufu haliwezi kubadili kile kilichotendeka.
"Jeshi la polisi Mkoa wa Tanga linamshikilia Hassan Mwakinyo (29) mkazi wa Sahare jijini Tanga kwa kumshambulia na kumjeruhi Mussa Ally mkazi wa eneo hilo ambae ni mvuvi,uchunguzi wa tukio hili unaendelea na ukikamilika mtuhumiwa atapelekwa mahakamani," amesema Mchunguzi.
Soma, Pia