Polisi wa TZ wanasingizia makosa kulazimisha rushwa

Polisi wa TZ wanasingizia makosa kulazimisha rushwa

Nchimbi J

Senior Member
Joined
Jun 16, 2008
Posts
132
Reaction score
20
Leo mida ya saa kumi nimeenda kibaha kwa mathias. Nikiwa narudi maeneo ya kibaha stand nikasimamishwa na trafiki. Wakasema kosa langu niliovertake maeneo ya miembe saba nikasimamishwa nikakimbia. Nikamwambia nitakuwa sio mie labda mtu mwingine kwa kuwa mie nimeishia kwa mathias na miembe saba ni mbele zaidi ya hapo ambako sikufika...yule polisi akasema basi mngoje alietoa order ukamatwe. Nikakaa hapo kibaha kituoni kwa zaidi ya saa moja uku wadada mapolisi wakinidhihaki kwa maneno ya taarab.baadae akaja huyo alieniona na sura yake ikilazimisha rushwa akinitishia kunipeleka mahakamani.Bahati nzuri akatokea askali mmoja akiitwa Mikidadi akamsihi sana huyo afande aniachie. Ndipo akaniachia kwa shingo upande baada ya kuwa kanisumbua kwa masaa mawili bila kosa....nikasema hawa ndio polisi wa Tanzani wenye kiu ya rushwa kwa kiwango cha kusingizia watu makosa. Naamini siku moja Watanzania watasema NO enough is enough.
 
Upigwe tu kama huwezi kuti sheri manaake hatuna jinsi upigwe tu

Hapana natii sheria lakini hio sehemu ambayo wanasema nilionekana ni kwamba hata sikufika huko..nimetoka dar nikageuzia sehemu ya kwa Mathias na wao wanadai kuniona miembe saba ambako sikufika
 
nchimbiJ, jina lako linafanana sana na jina la waziri wa mambo ya ndani, mko related kwa namna yeyote?
 
Polisi hata baba yake mzazi anaweza mdai rushwa ni hatari kuliko ukoma lo
 
Kwa hiyo unategemea ufanye uhalifu halafu uje hapa jf kusema umesingiziwa??

Watu kama wewe enzi zangu nilikuwa natupa lupango tu na kesho yake mahakamani mpaka uache uhalifu
 
Kwa hiyo unategemea ufanye uhalifu halafu uje hapa jf kusema umesingiziwa??

Watu kama wewe enzi zangu nilikuwa natupa lupango tu na kesho yake mahakamani mpaka uache uhalifu

Kumbe wewe ni polisi basi si kosa lako kuandika ujinga hapa
 
Pole sana kwa matatizo na pia pole kwa vile hii issue imechukuliwa kama mzaha na wengine.

Rushwa imeshika hatamu sasa katika idara zote nchini mwetu!

Mpaka lini tutakubali!! na kusema ENOUGH IS ENOUGH AND STOP!!
 
Leo mida ya saa kumi nimeenda kibaha kwa mathias. Nikiwa narudi maeneo ya kibaha stand nikasimamishwa na trafiki. Wakasema kosa langu niliovertake maeneo ya miembe saba nikasimamishwa nikakimbia. Nikamwambia nitakuwa sio mie labda mtu mwingine kwa kuwa mie nimeishia kwa mathias na miembe saba ni mbele zaidi ya hapo ambako sikufika...yule polisi akasema basi mngoje alietoa order ukamatwe. Nikakaa hapo kibaha kituoni kwa zaidi ya saa moja uku wadada mapolisi wakinidhihaki kwa maneno ya taarab.baadae akaja huyo alieniona na sura yake ikilazimisha rushwa akinitishia kunipeleka mahakamani.Bahati nzuri akatokea askali mmoja akiitwa Mikidadi akamsihi sana huyo afande aniachie. Ndipo akaniachia kwa shingo upande baada ya kuwa kanisumbua kwa masaa mawili bila kosa....nikasema hawa ndio polisi wa Tanzani wenye kiu ya rushwa kwa kiwango cha kusingizia watu makosa. Naamini siku moja Watanzania watasema NO enough is enough.


Pole sana mkuu, nami nimewahi kusingiziwa namna hiyo hiyo,nimetoka kwenye sherehe za mahafali OUT, nikakamatwa kiluvya kwamba nimekimbia polisi kongowe kwa kosa la ku overtake sehemu isiyoruhusiwa, nikapatwa na mshangao,kwani hata baada ya kumweleza yule askari ukweli juu ya kile kilichonileta huku kibaha,na kuwepo kwa mhusika wa Mahafali ndani ya gari bado aling'ang'ania kunirudisha Kibaha Polisi. Ikawa bahati njema ni kwamba katika ule ubishani kuna askari mwenye cheo cha juu wa polisi kibaha alivutiwa akiwa kwenye foleni na kuja kuuliza kinachoendelea,bila aibu yule trafic akabadili maelezo ya kuwa mimi nilitaka kuwagonga askari waliokuwa wakinisimamisha kibaha mizani,wao ndio wakapiga simu mimi nikamatwe,huku askari mwingine akijaribu sana kutaka nisiweze ongea na yule mkuu wao, mkuu wao alikuwa muelewa,wakati wao wanasisitiza wanipeleke ofisini nikaandike maelezo aliamua kutaka maelezo toka kwangu pale pale, niakamwomba apate maelezo toka kwa mmoja wa abilia wangu aliyekuwa ameshuka nami kwenmye gari kwani alikuwa anajua kosa lililoniweka hapo tofauti na hilo walilomwambia, akakubali na kumuuliza huyo abiria wangu,baada ya kupata jibu alimwita trafik mwingine na kumuuliza kwanini mimi nimekamatwa,huyu akatoa maelezo ya kosa la awali tofauti na lile alilioambiwa la kutaka kuwagonga trafic wa mizani, kilichofuata ni yule mkuu wao kuwaamulu warejee ofisini na kuniruhusi mimi kuendelea na safari...hawa ni majambazi walioewa leseni
 
Mapolisi wetu wana matatizo mengi sana na kama unavyosema kuwa wamekukwamisha zaidi ya masaa mawili ni wazi kwa muda huo kuna mchango ambao ungetoa kwenye ujenzi wa taifa. Zaidi akikukamata hivyo anawaza elfu tano na uwezo wao wa kujua kuwa anaingizia nchi hasara kwa wewe kutofanya kazi zako hawana. Inasikitisha ila sama kwa mfumo wa sasa wa serikali hakuna pa kusemea haya labda kidogo hapa jf!
 
Humu ndani hakuna Polisi! Watusaidie kwa hili la rushwa,,,
Mbaya zaidi virushwa wanavotaka n vdogo, mpaka unahis hawa ni njaa inawasumbua,,,utazan hawapewi mishahara,,,,,
 
Pole sana mkuu, nami nimewahi kusingiziwa namna hiyo hiyo,nimetoka kwenye sherehe za mahafali OUT, nikakamatwa kiluvya kwamba nimekimbia polisi kongowe kwa kosa la ku overtake sehemu isiyoruhusiwa, nikapatwa na mshangao,kwani hata baada ya kumweleza yule askari ukweli juu ya kile kilichonileta huku kibaha,na kuwepo kwa mhusika wa Mahafali ndani ya gari bado aling'ang'ania kunirudisha Kibaha Polisi. Ikawa bahati njema ni kwamba katika ule ubishani kuna askari mwenye cheo cha juu wa polisi kibaha alivutiwa akiwa kwenye foleni na kuja kuuliza kinachoendelea,bila aibu yule trafic akabadili maelezo ya kuwa mimi nilitaka kuwagonga askari waliokuwa wakinisimamisha kibaha mizani,wao ndio wakapiga simu mimi nikamatwe,huku askari mwingine akijaribu sana kutaka nisiweze ongea na yule mkuu wao, mkuu wao alikuwa muelewa,wakati wao wanasisitiza wanipeleke ofisini nikaandike maelezo aliamua kutaka maelezo toka kwangu pale pale, niakamwomba apate maelezo toka kwa mmoja wa abilia wangu aliyekuwa ameshuka nami kwenmye gari kwani alikuwa anajua kosa lililoniweka hapo tofauti na hilo walilomwambia, akakubali na kumuuliza huyo abiria wangu,baada ya kupata jibu alimwita trafik mwingine na kumuuliza kwanini mimi nimekamatwa,huyu akatoa maelezo ya kosa la awali tofauti na lile alilioambiwa la kutaka kuwagonga trafic wa mizani, kilichofuata ni yule mkuu wao kuwaamulu warejee ofisini na kuniruhusi mimi kuendelea na safari...hawa ni majambazi walioewa leseni

Hawa ndo wanachafua jina la Tanzania,
 
Kwa hiyo unategemea ufanye uhalifu halafu uje hapa jf kusema umesingiziwa??

Watu kama wewe enzi zangu nilikuwa natupa lupango tu na kesho yake mahakamani mpaka uache uhalifu

Sasa ilikuwaje ukafukuzwa upolisi kwa kuiba vidhibiti vya watuhumiwa??

Mwizi ni mwizi tu hata awe polisi. Kinacholiponza jeshi letu na polisi ni kuwa kuna majizi mengi tu kama wewe Chris Lukosi yako katika jeshi kwa kupewa kazi kiujomba na ushemeji sasa yanaendeleza ujizi wao na kusahau maadili ya jeshi. Na wewe ungebakia kuwa polisi wananchi wangekuchoma moto kama wale walichomwa moto kule Karagwe wakiwa na meno ya tembo a.k.a Kinana
 
nilikua nadrive kutoka arusha kwenda mwanza nilifika maeneo ya misungiw kama saa 11 ivi nikasimamishwa gari ilikua mpya kabisa double cabin... akaanza kunikomali reflector kwa nyuma ipo ila imefifia so haionyeshi vizuri inaweza sababisha ajari... wakati it was so obvious itakua inaonekana imefifia kwa sababu ya vumbi la safari ndefu... nilibisha alinikomali hadi tukaenda kituoni ikabidi nitake kuonana na ocs wakadai hayupo baada ya kama 2 hrs kwa hasira badala ya kumpa rushwa nikalipa fine tu!!! its was a joke of a season jinsi alivyokua anaonyesha njaa ya wazi.
 
Back
Top Bottom