Polisi wanaruhusiwa kupokea kesi za madai?

Jakoredo

New Member
Joined
Aug 27, 2022
Posts
1
Reaction score
0
Nilikopa pesa kwa maandishi nikarejesha kiasi cha pesa muda ukapita sikurejesha kiasi kilichobaki kulingana na tulivyoahidiana.

Mdai akaja nyumbani na Police kunikamata nikalala kituo cha police hadi kesho yake. Nikatolewa kwa kudhaminiwa, police wakagoma kunipa simu yangu kwa madai mara nitakapo rejesha deni ndio watanipatia simu yangu, nikawaambia hiyo simu ndio naweza kupata shughuli itakayopelekea kulipa hilo deni police wakakataa nikaomba japo line wakakataa pamoja na mkuu wa kituo katakata, na wakasema tutakufungulia kesi ya wizi wa kuaminika.

Je, ni haki mdaiwa akafanyiwa hivyo na police, je kesi kama hizo zinapaswa ziendeshweje.

Naomba ushahuri wenu wadau wa sheria.
 
Lipa deni la watu...
 
Inaelekea ulijibu shiit, jamaa ameamua Bora wale police mkose wote
 
Ikiwa wamekuachia na wanasema ni kesi ya wizi wakati kuna mkataba wa kukopeshana, wewe nenda peleka malalamiko kwa RCO wao hapo mkoani hilo jambo litaondolewa polisi

Hapo yule anayekudai ndio kaamua kuwatumia polisi kinyume na taratibu za kawaida ili kushinikiza ulipe deni

Lakini kwa upande mwingine kama iko ndani ya uwezo wako lipa deni la watu. Mara nyingi wadai hufanya hivyo inapotokea wanaona mdaiwa ana uwezo wa kulipa lakini hataki kulipa deni
 
Huo ni wizi wa kuaminika dhahiri,lipa uachane na bughudha.
 
Nenda mahakamani kafungue kesi ya kuporwa simu na polisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…