Polisi wanataka kupindua serikali ya JK: Tafsiri yangu

Polisi wanataka kupindua serikali ya JK: Tafsiri yangu

Lukolo

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
5,143
Reaction score
3,199
Ndugu zangu,

Naamini kila mtanzania hivi sasa ni shahidi wa matukio ambayo yamekuwa yakijitokeza nchini kwa kuwahusisha polisi. Pamoja na mfululizo wa polisi kuua watu kwenye mikutano ya CHADEMA, yakiwemo mauaji ya Arusha, Morogoro, Mwangosi na mfululizo wa kuwapiga mabomu na kuwakamata wanachadema wasio na hatia, bado hivi mapema tumesikia jinsi ambavyo polisi wamevamia mkutano wa CHADEMA huko Mabibo na kujeruhi watu.

Kwa tafsiri yangu polisi hawafanyi haya kwa bahati mbaya. Ni dhahiri kwamba polisi pia wameichoka sana serikali ya JK, lakini kwa kuwa hawana namna ya kuipindua basi wanaamua kuwapandisha hasira wananchi ili hatimaye waseme yatosha. Huu uonezi, ubabe na ukatili uliopita kiasi wa polisi kwa raia ndiyo uliomng'oa Rais Ben Ali wa Tunisia. Kwa hakika mbinu kama ile ya Tunisia naona ndiyo inatengenezwa hivi sasa hapa Tanzania kupitia jeshi la polisi.

Hawa watanzania hawataweza kuvumilia kuzika ndugu zao kila siku, hawataweza kuvumilia kuuguza ndugu zao kila siku, hawataweza kuvumilia kuishi katika hali ya ukiwa na ujane eti kwa kuwa tu ndugu zao wamekamatwa na kufungwa na polisi kwa makosa ya kusingiziwa. Hawatavumilia kuona ndugu zao wanauliwa na kumwagiwa tindikali halafu kesi ikifika polisi inapotezewa tu. Hawatavumilia kuona ujambazi na uharamia unaofanywa mitaani kwetu ukiendelea huku jeshi la polisi likiwa linaonekana kutokujali.

Ukivamiwa na majambazi, ukapiga simu polisi daima watafika dakika tano hadi kumi mara tu baada ya majambazi kutoka. Jambo ambalo linaashiria kwamba polisi na majambazi daima huwa na mawasiliano ya karibu juu ya kile kinachotupata. Mambo haya watanzania hawataweza kuendelea kuyavumilia. Definitely watajiunga kuikataa serikali hii isiyoweza kuwalinda, inayowaua, inayowaumiza, inayofunga bila kosa, na inayokandamiza haki zao.

Si rahisi sana kwa jeshi la polisi kufanya mambo ya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kiasi kikubwa hivi katika hali ya kawaida. Kwa hakika jeshi la polisi linafanya haya ili kuwaudhi watanzania, ili watanzania wakose uvumilivu waseme sasa yatosha. Ni hakika kwamba jeshi la polisi limeichoka serikali hii, lakini halina namna yoyote ya kuwaambia watanzania kwamba walichagua serikali mbovu, kilichobaki ni kuwachapa hawa watanzania hadi waichukie serikali yao, na kuingia barabarani kuitaka itoke.

Mimi si nabii, lakini tukijifunza kutoka kwa wenzetu, basi tutajua ni nini kinachofuata katika nchi yetu iwapo vitendo hivi vya kikatili vitaendelea.
 
Ulichosema kimeanza onesha viashiria tz,tuombe mungu kwan si tutavikabil viwanja na mipaka ili kuteketeza watawala
 
Ndugu zangu,

Naamini kila mtanzania hivi sasa ni shahidi wa matukio ambayo yamekuwa yakijitokeza nchini kwa kuwahusisha polisi. Pamoja na mfululizo wa polisi kuua watu kwenye mikutano ya CHADEMA, yakiwemo mauaji ya Arusha, Morogoro, Mwangosi na mfululizo wa kuwapiga mabomu na kuwakamata wanachadema wasio na hatia, bado hivi mapema tumesikia jinsi ambavyo polisi wamevamia mkutano wa CHADEMA huko Mabibo na kujeruhi watu.

Kwa tafsiri yangu polisi hawafanyi haya kwa bahati mbaya. Ni dhahiri kwamba polisi pia wameichoka sana serikali ya JK, lakini kwa kuwa hawana namna ya kuipindua basi wanaamua kuwapandisha hasira wananchi ili hatimaye waseme yatosha. Huu uonezi, ubabe na ukatili uliopita kiasi wa polisi kwa raia ndiyo uliomng'oa Rais Ben Ali wa Tunisia. Kwa hakika mbinu kama ile ya Tunisia naona ndiyo inatengenezwa hivi sasa hapa Tanzania kupitia jeshi la polisi.

Hawa watanzania hawataweza kuvumilia kuzika ndugu zao kila siku, hawataweza kuvumilia kuuguza ndugu zao kila siku, hawataweza kuvumilia kuishi katika hali ya ukiwa na ujane eti kwa kuwa tu ndugu zao wamekamatwa na kufungwa na polisi kwa makosa ya kusingiziwa. Hawatavumilia kuona ndugu zao wanauliwa na kumwagiwa tindikali halafu kesi ikifika polisi inapotezewa tu. Hawatavumilia kuona ujambazi na uharamia unaofanywa mitaani kwetu ukiendelea huku jeshi la polisi likiwa linaonekana kutokujali.

Ukivamiwa na majambazi, ukapiga simu polisi daima watafika dakika tano hadi kumi mara tu baada ya majambazi kutoka. Jambo ambalo linaashiria kwamba polisi na majambazi daima huwa na mawasiliano ya karibu juu ya kile kinachotupata. Mambo haya watanzania hawataweza kuendelea kuyavumilia. Definitely watajiunga kuikataa serikali hii isiyoweza kuwalinda, inayowaua, inayowaumiza, inayofunga bila kosa, na inayokandamiza haki zao.

Si rahisi sana kwa jeshi la polisi kufanya mambo ya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kiasi kikubwa hivi katika hali ya kawaida. Kwa hakika jeshi la polisi linafanya haya ili kuwaudhi watanzania, ili watanzania wakose uvumilivu waseme sasa yatosha. Ni hakika kwamba jeshi la polisi limeichoka serikali hii, lakini halina namna yoyote ya kuwaambia watanzania kwamba walichagua serikali mbovu, kilichobaki ni kuwachapa hawa watanzania hadi waichukie serikali yao, na kuingia barabarani kuitaka itoke.

Mimi si nabii, lakini tukijifunza kutoka kwa wenzetu, basi tutajua ni nini kinachofuata katika nchi yetu iwapo vitendo hivi vya kikatili vitaendelea.

Hizo ni ndoto za mchana kweupe, endeleeni kujipa moyo na CHADEMA yenu
 
Gadaf aliwaita mende, panya nk. Akafia katka mtaro wa maji machafu.... Tarehe zenu zipo filed
Bora umwambie. Haitakuwa rahisi hata kidogo kwa wanaCCM kujua kwamba watu wakichoka huwa wapo tayari kwa lolote. Kwa hakika KITOMONDO, hakuna risasi zitakazotosha kuwazuia watanzania mara baada ya kuchoka na manyanyaso haya yanayofanywa na polisi. Watu wakishakata tamaa watatamani kupigwa risasi ili waingie katika historia ya wapigania ukombozi wa taifa kuliko kuishi katika hali ya shida na mateso.
 
Gadaf aliwaita mende, panya nk. Akafia katka mtaro wa maji machafu.... Tarehe zenu zipo filed

Walibwa ni wao na Watanzania ni sisi tunaojijua wenyewe,so bado haujatumia convising power ya kutosha ya kunifanya niamini usemacho
 
huja kosea hata chembe....posil ndio chanzo cha kuvunjika kwa amani hapo tz
 
unacho ongea na mimi nafikiri hivyo hivyo
polisi now wanapokea maagizo kutoka kwa mtu mwingine
ambae anataka nchi itokee vurugu kuubwa ili katika vurugu hiyo
yeye afanye lake...
 
huja kosea hata chembe....posil ndio chanzo cha kuvunjika kwa amani hapo tz

unacho ongea na mimi nafikiri hivyo hivyo
polisi now wanapokea maagizo kutoka kwa mtu mwingine
ambae anataka nchi itokee vurugu kuubwa ili katika vurugu hiyo
yeye afanye lake...
Kuna viashiria vyote kwamba kuna underground campaign inaendelea ya kuhakikisha kwamba serikali ya JK haifiki 2015. Sema tu ndiyo hivyo hatujui ni nani anaendesha hii kampeni. Lakini ni wazi kwamba wakubwa kadhaa wa jeshi hili wanamdanganya JK na viongozi wa CCM kwamba wanaidhibiti CHADEMA na wale wanaoipinga serikali (refer Ulimboka) ilihali wanaamsha hasira za wananchi dhidi ya serikali.
 
Kuna viashiria vyote kwamba kuna underground campaign inaendelea ya kuhakikisha kwamba serikali ya JK haifiki 2015. Sema tu ndiyo hivyo hatujui ni nani anaendesha hii kampeni. Lakini ni wazi kwamba wakubwa kadhaa wa jeshi hili wanamdanganya JK na viongozi wa CCM kwamba wanaidhibiti CHADEMA na wale wanaoipinga serikali (refer Ulimboka) ilihali wanaamsha hasira za wananchi dhidi ya serikali.

JK ni mtu rahisi kudanganywa
ndo maana kampa nishani Said Mwema
yeye hajui hata nini kinaendelea
analetewa information na hao hao amba anawaamini na ambao ndo wanam undermine
kazi ipo
 
Walibwa ni wao na Watanzania ni sisi tunaojijua wenyewe,so bado haujatumia convising power ya kutosha ya kunifanya niamini usemacho

Who are you before 44,900,000 population of Tz... We akili imeshaoza. Hata ukilia watu tunakomaa tu!
 
JK ni mtu rahisi kudanganywa
ndo maana kampa nishani Said Mwema
yeye hajui hata nini kinaendelea
analetewa information na hao hao amba anawaamini na ambao ndo wanam undermine
kazi ipo
Kuna wakati ni vigumu hata kuamini kama ni kudanganywa au ni makusudi. Maana utaangalia kwenye tukio kama la Kamuhanda, hivi kweli linahitaji hata ushahidi kweli ili ujue kwamba hafai? Badala yake yeye JK anampandisha cheo? Mimi naona kama JK naye ni kichwa ngumu tu. Na yoyote yatakayotokea kwa hakika yatakuwa yamechochewa na JK mwenyewe. Tuombe tu Mungu hayo mapinduzi ya umma yasiwe na madhara makubwa kwa waandamanaji.
 
Kuna wakati ni vigumu hata kuamini kama ni kudanganywa au ni makusudi. Maana utaangalia kwenye tukio kama la Kamuhanda, hivi kweli linahitaji hata ushahidi kweli ili ujue kwamba hafai? Badala yake yeye JK anampandisha cheo? Mimi naona kama JK naye ni kichwa ngumu tu. Na yoyote yatakayotokea kwa hakika yatakuwa yamechochewa na JK mwenyewe. Tuombe tu Mungu hayo mapinduzi ya umma yasiwe na madhara makubwa kwa waandamanaji.

Ukiwa Rais hamna watu unao waamini kama watu wa Intelligence
so hao wakiwa wamenunuliwa..you are done
 
Who are you before 44,900,000 population of Tz... We akili imeshaoza. Hata ukilia watu tunakomaa tu!
Hivi ndiyo wanaCCM wote wanavyoamini. Kwamba watanzania ni mazuzu tu, unaweza ukawaua ukawanyanyasa na wataendelea tu kuwa wapole.
 
Back
Top Bottom