Polisi Zanzibar walichora Mchoro wa wasiojulikana wakakamatwa, bara tunashindwa nini kwa Lissu?

Polisi Zanzibar walichora Mchoro wa wasiojulikana wakakamatwa, bara tunashindwa nini kwa Lissu?

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Heshima kwenu wakuu,

Kigugumizi cha nini baba?

Padri wa Kanisa Katoliki, Evaristus Mushi aliyefariki dunia baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akiegesha gari kando na Kanisa la Mtoni mwaka 2013, rais Jakaya Kikwete katika salamu zake za rambirambi baada ya mauaji ya Padri Mushi, aliagiza Jeshi la Polisi kutumia nguvu zake zote pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya usalama vya ndani na mashirika ya upelelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji hayo.

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alihusisha tukio hilo na vitendo vya ugaidi wakati akitoa tamko la Serikali na kueleza kuwa Rais Kikwete ameidhinisha Serikali kugharamia wapelelezi kutoka nje kufanyia kazi swala hilo.

Serikali ya Marekani iliyokuwa tayari kusaidia upelelezi wa mauaji hayo, ambapo haraka sana ASKARI wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), waliwasili Zanzibar kufanya uchunguzi wa kuwabaini waliomuua kwa kumpiga risasi, Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.

Napenda kujua kwanini awamu hii ya tano wanakuwa na kigugumizi kuwashughulikia watu wasiojulikana?

Hii ilikuwa mara ya pili kwa FBI kuja nchini kufanya operesheni kubwa ya upelelezi. Mwaka 1998 walifika kuchunguza kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani na kugundua kuwa Kundi la Al-Qaeda lilihusika.

Aidha hiyo ni mara ya tatu kwa wapelelezi wa Tanzania kushirikiana na wageni kuchunguza matukio ya uhalifu baada ya mwaka 1984, Idara ya Upelelezi ya Uingereza, Scotland Yard ya Uingereza kuchunguza kuungua kwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Watu wasiojulikana wanaenda kuiweka Tanzania roho juu. Kwanini Mwigulu hachukui hatua aliyoichukua mwenzake Nchimbi 2013?

Baada ya FBI kufanya uchunguzi Zanzibar, ilitoa picha ya mchoro ya mtu anayedaiwa kumuua kwa kumpiga risasi Padre Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.
mchoro.jpg

Mchoro huo ulisambazwa katika vyombo vya habari kutoka ofisi ya Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Mussa Ali Mussa na ulimuonesha ‘mtu’ aliyevaa baraghashia….

Tunaomba Serikali ya Magufuli itusaidie kutupatia japo mchoro tu wa watu wasiojulikana.

Jisomee=>Muuaji wa Padri Evarist Mushi Akamatwa kwa msaada wa picha iliyochorwa na FBI

FBI waondoka Zanzibar bila polisi kujua

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Watajulikana tu nakumbuka libya baada ya mambo kuwa mazito watu wasiojulikana wakaamuwa kujiunga na wananchi
 
Heshima kwenu wakuu,

Kigugumizi cha nini baba?

Padri wa Kanisa Katoliki, Evaristus Mushi aliyefariki dunia baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akiegesha gari kando na Kanisa la Mtoni mwaka 2013, rais Jakaya Kikwete katika salamu zake za rambirambi baada ya mauaji ya Padri Mushi, aliagiza Jeshi la Polisi kutumia nguvu zake zote pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya usalama vya ndani na mashirika ya upelelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji hayo.

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alihusisha tukio hilo na vitendo vya ugaidi wakati akitoa tamko la Serikali na kueleza kuwa Rais Kikwete ameidhinisha Serikali kugharamia wapelelezi kutoka nje kufanyia kazi swala hilo.

Serikali ya Marekani iliyokuwa tayari kusaidia upelelezi wa mauaji hayo, ambapo haraka sana ASKARI wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), waliwasili Zanzibar kufanya uchunguzi wa kuwabaini waliomuua kwa kumpiga risasi, Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.

Napenda kujua kwanini awamu hii ya tano wanakuwa na kigugumizi kuwashughulikia watu wasiojulikana?

Hii ilikuwa mara ya pili kwa FBI kuja nchini kufanya operesheni kubwa ya upelelezi. Mwaka 1998 walifika kuchunguza kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani na kugundua kuwa Kundi la Al-Qaeda lilihusika.

Aidha hiyo ni mara ya tatu kwa wapelelezi wa Tanzania kushirikiana na wageni kuchunguza matukio ya uhalifu baada ya mwaka 1984, Idara ya Upelelezi ya Uingereza, Scotland Yard ya Uingereza kuchunguza kuungua kwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Watu wasiojulikana wanaenda kuiweka Tanzania roho juu. Kwanini Mwigulu hachukui hatua aliyoichukua mwenzake Nchimbi 2013?

Baada ya FBI kufanya uchunguzi Zanzibar, ilitoa picha ya mchoro ya mtu anayedaiwa kumuua kwa kumpiga risasi Padre Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.
View attachment 713900
Mchoro huo ulisambazwa katika vyombo vya habari kutoka ofisi ya Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Mussa Ali Mussa na ulimuonesha ‘mtu’ aliyevaa baraghashia….

Tunaomba Serikali ya Magufuli itusaidie kutupatia japo mchoro tu wa watu wasiojulikana.

Jisomee=>Muuaji wa Padri Evarist Mushi Akamatwa kwa msaada wa picha iliyochorwa na FBI

FBI waondoka Zanzibar bila polisi kujua
Hahahaha hivi ulifuatilia ile kesi imefikia wapi? wacheni ujinga wa mawazo.
 
Samahani wakuu naomba nitoke nje ya mada kidogo na mwenye idea na jambo hili anisaidie,hivi hawa jamaa huwa wanatumia sayansi gani kuhisi hadi wanachora picha ya mtu anayeweza kufanana au anayefanana na mtuhumiwa wa tukio fulani?inaniumizaga sana akili hii.
 
Ukivaa nguo yenye maandishi yanayo someka pray for Lissu unakamatwa!
 
Baada ya CIA kumaliza kazi iligundulika Mtu waliemchora ni Mgonjwa wa Akili na ndio Ukawa Mwisho wa Matumizi ya mchoro huo
 
Heshima kwenu wakuu,

Kigugumizi cha nini baba?

Padri wa Kanisa Katoliki, Evaristus Mushi aliyefariki dunia baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akiegesha gari kando na Kanisa la Mtoni mwaka 2013, rais Jakaya Kikwete katika salamu zake za rambirambi baada ya mauaji ya Padri Mushi, aliagiza Jeshi la Polisi kutumia nguvu zake zote pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya usalama vya ndani na mashirika ya upelelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji hayo.

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alihusisha tukio hilo na vitendo vya ugaidi wakati akitoa tamko la Serikali na kueleza kuwa Rais Kikwete ameidhinisha Serikali kugharamia wapelelezi kutoka nje kufanyia kazi swala hilo.

Serikali ya Marekani iliyokuwa tayari kusaidia upelelezi wa mauaji hayo, ambapo haraka sana ASKARI wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), waliwasili Zanzibar kufanya uchunguzi wa kuwabaini waliomuua kwa kumpiga risasi, Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.

Napenda kujua kwanini awamu hii ya tano wanakuwa na kigugumizi kuwashughulikia watu wasiojulikana?

Hii ilikuwa mara ya pili kwa FBI kuja nchini kufanya operesheni kubwa ya upelelezi. Mwaka 1998 walifika kuchunguza kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani na kugundua kuwa Kundi la Al-Qaeda lilihusika.

Aidha hiyo ni mara ya tatu kwa wapelelezi wa Tanzania kushirikiana na wageni kuchunguza matukio ya uhalifu baada ya mwaka 1984, Idara ya Upelelezi ya Uingereza, Scotland Yard ya Uingereza kuchunguza kuungua kwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Watu wasiojulikana wanaenda kuiweka Tanzania roho juu. Kwanini Mwigulu hachukui hatua aliyoichukua mwenzake Nchimbi 2013?

Baada ya FBI kufanya uchunguzi Zanzibar, ilitoa picha ya mchoro ya mtu anayedaiwa kumuua kwa kumpiga risasi Padre Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki.
View attachment 713900
Mchoro huo ulisambazwa katika vyombo vya habari kutoka ofisi ya Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Mussa Ali Mussa na ulimuonesha ‘mtu’ aliyevaa baraghashia….

Tunaomba Serikali ya Magufuli itusaidie kutupatia japo mchoro tu wa watu wasiojulikana.

Jisomee=>Muuaji wa Padri Evarist Mushi Akamatwa kwa msaada wa picha iliyochorwa na FBI

FBI waondoka Zanzibar bila polisi kujua
Duh hapa serikali inahusika mkuu tunajua ilo
 
Ungetumia tu busara yako kusema ilipoishia badala ya kutaja ujinga wa mawazo wa watu
Tatizo watu wa Jamii forums wanajifanya wajuaji sana kwa kuongea vitu ambavyo hawavielewi..na hawataki kueleweshwa kwani wao wako juu ya kila kitu.
 
Kwani Mwigulu, bashite na kundi lao hamuwajuwi mpaka mchorewe?
 
Hao watu wanashindwa nini kufanya sasa hiyo michoro? kwani wamekataa kuja?

unataka waumbuke, uchunguzi mfano wa lissu hata kijana w aprimary anweza fanya.
hivi ukijua kwanini sikuhiyo Polisi hawakuwepo lindo, hiyo haitoshi kupata jibu?
kwanini CCTV camera imepotea hujapata jibu tu ?
 
Back
Top Bottom