kilambimkwidu
JF-Expert Member
- Jul 21, 2017
- 6,097
- 7,199
Wanajukwaa,
Nashea na nyie jinsi mseto wa pombe ulivoniaibisha nikatukana siku nilipoitwa kutoa nasaha kwa niaba ya baba wa bibi harusi kwakua mzazi wake anakigugumizi asingeweza kuendana na kasi lakn pia wageni wasingemuelewa.
Ilikua mwaka 2016 mwezi Mei Nzega nilihudhuria harusi ya mtoto wa Binamu yangu, kama kawaida nilipania sana pombe. Siku ile nilikunywa sana Balimi nikamix na mzinga wa K-Vant. Nilikua na wananzengo tu wife ye hakuja harusini.
Mara paa, akaja shangazi yake na baba wa bwn harusi akaniomba nikatoe nasaha kwa niaba ya mzazi wa bibi harusi kwakua babake hua anakigugumizi sugu. Sikujietathmin hata kama ntaweza ile kaz au la, nikaendelea kula bia nikijua ntapambana na hali yangu, labda tena ntakua na konfidensi zaidi kutokana na nilivochapa mtungi.
Skumbuki ilikuaje wakat wa nasaha, ila nilisikitika kuambiwa kwamba nilimuasa bibi harusi kwa ukali sana na nilitumia maneno makali kupitiliza. Naambiwa nilitamka visivyotamkwa na nilirudia mara kwa mara maneno "https://jamii.app/JFUserGuide you".
Naambiwa kwamba bibi harusi alifedheheka sana na alikua akilia wakat waalikwa wengine walikua wanaangua kicheko na kwakua nilikua nataka sifa kwaajili ya pombe, nilikua hata simuangalii bi harusi, niliwageukiwa wageni waalikwa na kutoa maneno ya kuudhi sana. Kwenye ile ya CD ya harusi nimeambiwa wamekata hotuba yangu japo kipande kilichopo najiona nikiwa nimekunja ndita na kuongea kwa ukali huku mate yaliyogeuka mapovu meupe yamenijaa.
Nilijutia na kuomba msamaha kwenye kikao cha ukoo. Walinisamehe wengine kwa shingo upande
Balimi mixer K-Vant
Nashea na nyie jinsi mseto wa pombe ulivoniaibisha nikatukana siku nilipoitwa kutoa nasaha kwa niaba ya baba wa bibi harusi kwakua mzazi wake anakigugumizi asingeweza kuendana na kasi lakn pia wageni wasingemuelewa.
Ilikua mwaka 2016 mwezi Mei Nzega nilihudhuria harusi ya mtoto wa Binamu yangu, kama kawaida nilipania sana pombe. Siku ile nilikunywa sana Balimi nikamix na mzinga wa K-Vant. Nilikua na wananzengo tu wife ye hakuja harusini.
Mara paa, akaja shangazi yake na baba wa bwn harusi akaniomba nikatoe nasaha kwa niaba ya mzazi wa bibi harusi kwakua babake hua anakigugumizi sugu. Sikujietathmin hata kama ntaweza ile kaz au la, nikaendelea kula bia nikijua ntapambana na hali yangu, labda tena ntakua na konfidensi zaidi kutokana na nilivochapa mtungi.
Skumbuki ilikuaje wakat wa nasaha, ila nilisikitika kuambiwa kwamba nilimuasa bibi harusi kwa ukali sana na nilitumia maneno makali kupitiliza. Naambiwa nilitamka visivyotamkwa na nilirudia mara kwa mara maneno "https://jamii.app/JFUserGuide you".
Naambiwa kwamba bibi harusi alifedheheka sana na alikua akilia wakat waalikwa wengine walikua wanaangua kicheko na kwakua nilikua nataka sifa kwaajili ya pombe, nilikua hata simuangalii bi harusi, niliwageukiwa wageni waalikwa na kutoa maneno ya kuudhi sana. Kwenye ile ya CD ya harusi nimeambiwa wamekata hotuba yangu japo kipande kilichopo najiona nikiwa nimekunja ndita na kuongea kwa ukali huku mate yaliyogeuka mapovu meupe yamenijaa.
Nilijutia na kuomba msamaha kwenye kikao cha ukoo. Walinisamehe wengine kwa shingo upande
Balimi mixer K-Vant