Pombe sio sehemu ya mchezo wa mpira, chezeni mpira acheni ulevi wa pombe

Covax

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2021
Posts
10,198
Reaction score
35,323
Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA Gianni Infantino amezungumza na waandishi wa habari huko Qatar kuhusiana na malalamiko ya kutokuwepo kwa pombe viwanjani kwenye michuano ya Kombe la Dunia.

Infantino amesema kuwa,“Kama pombe ndilo suala kubwa tulilonalo kwa Kombe la Dunia basi nitajiuzulu mara moja na kwenda ufukweni kupumzika."

"Usipokunywa bia kwa masaa mawili matatu, bado unaweza kuishi, kwa sababu utaratibu huu pia upo hata kwenye nchi za Ulaya, ukienda Ufaransa, Ureno hata Uswisi sheria hizi zipo.Hapa imekuwa jambo kubwa sijui ni kwanini au ni kwa kuwa sababu ni nchi ya Kiislamu."

#WorldCupQatar
 
Tunakoelekea, nchi zenye mazingira kama QATAR hazitapigiwa kura tena kufanyia kombe la duni huko..!!
 
Mayahudi na manasara hawawi radhi mpaka ufuate mila zao. Yaani BBC wameshikilia bango Qatar kisa wamekataa mapenzi ya jinsia moja. Walivomajeuri Qatar wamewaambia mashoga wana matatizo ya akili. Hawa Qatar achana nao kabisa wana jeuri hatari, walikua wanaagiza maziwa kutoka Saudia, wakawazingua , walienda kupandisha ndege ngombe elfu 15 kutoka Marekani mpaka Qatar
 
Kwa waarabu michezo ni haramu na ndio maana hata yale makundi ya kigaidi hayaruhusu michezo na elimu dunia kwenye sera zao.
 
Inaongelewa pombe hapa sio ushoga
 
Akili kama hizo tungekua nazo waafrika angalau 55% zingetusaidia kusimamia kikamilifu rasilimali zetu kwa ustawi wa jamii zetu. Lakini wapi bwana!
Heko kwa Qatar japo wana ushenzi wao kwenye suala la treatment ya migrants kwenye maeneo ya kazi hasa wasio na ujuzi rasmi.
 
Mkuu

Agenda ya Wamagharibi kulazimisha haki za LGBTQ ndani ya Qatar ndio mzozo ulipo. LGBTQ wameamua liwalo na liwe. Mamlaka za Qatar zimekataa. Hata kisingizio eti ni pombe imetusababisha nacho kimepigwa pini.

Kifupi: Pombe sio issue kabisa. Inasingiziwa.
 

Attachments

  • Screenshot_2022-11-19-16-37-05-61.jpg
    27.5 KB · Views: 5
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…