Pombe....

Pombe....

GP

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2009
Posts
2,049
Reaction score
161
.....Inasaidia Kupunguza Magonjwa ya Moyo


Matokeo ya utafiti uliofanyika hivi karibuni kuhusiana na unywaji pombe umeonyesha kuwa wanaume wanaokunywa pombe kila siku wana uwezekano mdogo wa kupata matatizo ya moyo kulinganisha na wanaume wasiokunywa pombe kabisa. Utafiti uliofanyika nchini Hispania na kuwashirikisha wanaume 15,000 na wanawake 26,000 umeonyesha kuwa pombe inasaidia kupunguza theluthi moja magonjwa ya moyo kwa wanaume wanaokunywa pombe kila siku.

Hata hivyo pombe haikuonekana kuwa na faida yoyote kwa wanawake wanaokunywa kila siku.

Utafiti huo ulifanyika nchini Hispania ambako wakazi wake wengi ni walevi huku kukiwa na wagonjwa wachache wa matatizo ya moyo.

Utafiti huo ulihusisha wanawake na wanaume wenye umri kati ya miaka 29 na 69 ambao walitakiwa kuandika historia yao ya unywaji pombe na kisha kufuatiliwa afya zao kwa kipindi cha miaka 10.

Aina ya pombe walizokuwa wakinywa washiriki wa utafiti huo hazikuonyesha tofauti yoyote kati yao.

Jinsi pombe inavyosaidia kupunguza matatizo ya moyo bado haijakuwa wazi ingawa inajulikana kuwa pombe husaidia kuongeza kiwango cha lipoproteins mwilini ambacho huzuia kolestro zinazosababisha matatizo ya moyo kujijenga kwenye mishipa ya kusafirishia damu.

Hata hivyo wataalamu wameendelea kuonya kuwa unywaji wa pombe uliopita kiwango ni hatari na husababisha matatizo mengi ya kiafya ambayo husababisha vifo vya watu milioni 1.8 kila mwaka.

wapwa hii mnasemaje??

source
 
Sasa Porjie ndo umeamua wawe wanaenda kulala hukohuko Zer pub au??
 
Sasa Porjie ndo umeamua wawe wanaenda kulala hukohuko Zer pub au??

hahahaaaa, sio mchezo jamaa hapa wamepruvu kwamba biere ziko poa kwenye magonywa ya moyo, ntazinywa sana!!.
wapwa wanajua mambo ya chuichui ndio maana tuko fit kiafya, TRY IT AT ANY BAR!
 
hahahaaaa, sio mchezo jamaa hapa wamepruvu kwamba biere ziko poa kwenye magonywa ya moyo, ntazinywa sana!!.
wapwa wanajua mambo ya chuichui ndio maana tuko fit kiafya, TRY IT AT ANY BAR!

chui lazima wakulipe hii 'air time' haki ya nani vile....in cash or 'kind'
 
Ulevi wangu ni maji ya K'njaro
hahahaaaaa, naskia tena unachangamka baraaaaa!, itabidi kwenye get tugeza tukuagizie boza zima pale sayansi kwa ajili yako!.
 
Utafiti uliofanyika nchini Hispania na kuwashirikisha wanaume 15,000 na wanawake 26,000 umeonyesha kuwa pombe inasaidia kupunguza theluthi moja magonjwa ya moyo kwa wanaume wanaokunywa pombe kila siku

Kuwa makini na hiyo theluthi moja na sidhani kama utafiti ulihusisha pombe kama zetu hizi , mwisho kumbuka bado haijajulikana jinsi pombe inavyoweza kupunguza magonjwa ya moyo so wakati unalitafakari hili pia ujue pombe ina madhara mengi sio magonjwa ya moyo tu, kunywa kwa afya!!!
 
Utafiti wenu na uishie kuzimu! Sitakunywa pombe na uwezekano wa kupata magojwa ya moyo kwasababu ya kutokunya pombe haupo!Naamini waliofanya huo utafiti ni maajenti au wajukuu wa shetani
 
Utafiti wenu na uishie kuzimu! Sitakunywa pombe na uwezekano wa kupata magojwa ya moyo kwasababu ya kutokunya pombe haupo!Naamini waliofanya huo utafiti ni maajenti au wajukuu wa shetani

karibu sana JF!,
wewe ni HE/SHE?
 
Utafiti wenu na uishie kuzimu! Sitakunywa pombe na uwezekano wa kupata magojwa ya moyo kwasababu ya kutokunya pombe haupo!Naamini waliofanya huo utafiti ni maajenti au wajukuu wa shetani

Barikiwa ndg yangu,waache hao waendelee kusikiliza uongo wa baba wa uongo (shetani) na maajenti wake ambao wako kazini wakijua wanao muda mchache uliobaki wa kutimiza kazi yao hapa duniani.
 
Back
Top Bottom