Pongezi kwa TPB na Vodacom Tanzania kwa huduma ya M-Koba

Pongezi kwa TPB na Vodacom Tanzania kwa huduma ya M-Koba

Mlenge

R I P
Joined
Oct 31, 2006
Posts
2,125
Reaction score
2,306
Pongezi nyingi kwa TPB na Vodacom Tanzania kwa huduma maridhawa ya M-Koba. Nimefurahi kukuta sasa mtu mwenye laini ya simu ya mtandao wowote anaweza kuwa mwanachama wa M-Koba. Mbona kimyakimya? Hili ni jambo kubwa sana. Lilipaswa kuzinduliwa kwa mashamsham yote.

Fursa ya Kuboresha: Wekeni uwezekano wa makato kutoka kwenye mishahara ya watumishi wa umma na wa sekta binafsi, au kupitia 'standing orders' za benki, kuhamisha sehemu ya mshahara au kipato cha kila muda fulani, e.g., mwezi automagically kutoka benki kwenda kwenye mfuko wa M-Koba.
 
Hiyo M-Koba wengine hatuifahamu.

Hii ni moja ya huduma muhimu sana kuwahi kutolewa Tanzania. Inakata urasimu mwingi. Inaleta ufanisi. Inaongeza uwazi.

Chukulia kwa mfano Kikundi cha Kijamii kinataka kuwa na mfuko maalum kwa malengo maalum. Unaweza kuanzisha mfuko huo kwa M-Koba. Ukiwa na laini ya Vodacom *150*00# Chagua 6 Huduma za Kifedha kisha Chagua 5 M-KOBA.

Ukiwa na huduma ya M-KOBA, Katibu anaanzisha muamala, Mweka Hazina akiuidhinisha, na Mwenyekiti akikubali ndipo muamala hufanyika. Wanachama wote huweza kuona salio la kwenye mfuko na michango yao. Na huona nani kalipwa nini (hili sina hakika nalo kwa sasa). Mambo hayo yote hufanyika kupitia USSD ya simu za kiganjani -- kwa hiyo hata mwenye kitochi huweza kutumia.

Mambo ya kijumbe kukimbia na hela hakuna tena. Masharti yote ya kikundi yanaweza kuwekwa kwenye akaunti ya M-KOBA, kwa hiyo adhabu za kuchelewa, mambo ya hisa kwenye VICOBA, nk. yanaweza kufanyika kupitia simu-tochi ya kiganjani.

TPB na Vodacom Tanzania IMHO wamejizolea pointi nyingi sana kwa jambo hili la M-KOBA.
 
Pongezi nyingi kwa TPB na Vodacom Tanzania kwa huduma maridhawa ya M-Koba. Nimefurahi kukuta sasa mtu mwenye laini ya simu ya mtandao wowote anaweza kuwa mwanachama wa M-Koba. Mbona kimyakimya? Hili ni jambo kubwa sana. Lilipaswa kuzinduliwa kwa mashamsham yote.

Fursa ya Kuboresha: Wekeni uwezekano wa makato kutoka kwenye mishahara ya watumishi wa umma na wa sekta binafsi, au kupitia 'standing orders' za benki, kuhamisha sehemu ya mshahara au kipato cha kila muda fulani, e.g., mwezi automagically kutoka benki kwenda kwenye mfuko wa M-Koba.
System yao ya mtandao inasumbua mpaka inakera. Sijui kama wameboresha
 
System yao ya mtandao inasumbua mpaka inakera. Sijui kama wameboresha

Kwa vile M-KOBA inatumia USSD, mara chache sana mtandao wa Vodacom kusumbua eneo hilo. Binafsi laini ninayotumia sana ni ya Vodacom, na ninatumia USSD kila mara, na sipati matatizo. Nadhani ni hivyo pia kwa watumiaji wengine.
 
Dijitalisation ni Jambo jema sna kwenye sekta ya kifedha na issue kubwa ni gharama za kuhamisha fedha kwa wanachama wa vikundi hasa ukichukulia faida kwenye hivi vyama vyakuweka na kukopa ni ndogo Sana.
Bado uhamisjaji na utumaji wa fedha miongoni mwa wanachama na chama ni changamoto na hivyoo kuwafanya wanachama wengi kuhisi kuwa ni mzigo kuliko suluhu.

Eneo hili likiboreshwa zaidi tunaweza kuona mapinduzi makubwa Sana ukizingatia hizi taasisi za vikoba ,Sacco's na vikundi vya kuweka na kukopa vinazungusha fedha nyingi Sana mitaani kwetu.
 
Dijitalisation ni Jambo jema sna kwenye sekta ya kifedha na issue kubwa ni gharama za kuhamisha fedha kwa wanachama wa vikundi hasa ukichukulia faida kwenye hivi vyama vyakuweka na kukopa ni ndogo Sana.
Bado uhamisjaji na utumaji wa fedha miongoni mwa wanachama na chama ni changamoto na hivyoo kuwafanya wanachama wengi kuhisi kuwa ni mzigo kuliko suluhu.

Eneo hili likiboreshwa zaidi tunaweza kuona mapinduzi makubwa Sana ukizingatia hizi taasisi za vikoba ,Sacco's na vikundi vya kuweka na kukopa vinazungusha fedha nyingi Sana mitaani kwetu.

M-KOBA haina gharama za kuhamisha hela kutoka M-Koba kwenda kwenye simu ya mwanachama. Wao Vodacom wanapata hela zao kwa wanachama kulipia gharama za kuangalia salio.
 
M-KOBA haina gharama za kuhamisha hela kutoka M-Koba kwenda kwenye simu ya mwanachama. Wao Vodacom wanapata hela zao kwa wanachama kulipia gharama za kuangalia salio.
Katika kufanya malipo kuna haja ya kwenda katika ofisi za vodacom??
 
Katika kufanya malipo kuna haja ya kwenda katika ofisi za vodacom??
Hakuna mkuu...umetusaidia sana kwenye kikoba chetu...na hawana longolongo...hakuna makato ya kijinga jinga..kikundi chetu kidogo since tumeanza tumeshafanya miamala genye thamani yenye thamani ya sh. Milioni 20.
 
M-KOBA haina gharama za kuhamisha hela kutoka M-Koba kwenda kwenye simu ya mwanachama. Wao Vodacom wanapata hela zao kwa wanachama kulipia gharama za kuangalia salio.
Kikundi kinapaswa kuanzia na watu wangapi? Je mikopo ipo?
 
Hii ni moja ya huduma muhimu sana kuwahi kutolewa Tanzania. Inakata urasimu mwingi. Inaleta ufanisi. Inaongeza uwazi.

Chukulia kwa mfano Kikundi cha Kijamii kinataka kuwa na mfuko maalum kwa malengo maalum. Unaweza kuanzisha mfuko huo kwa M-Koba. Ukiwa na laini ya Vodacom *150*00# Chagua 6 Huduma za Kifedha kisha Chagua 5 M-KOBA.

Ukiwa na huduma ya M-KOBA, Katibu anaanzisha muamala, Mweka Hazina akiuidhinisha, na Mwenyekiti akikubali ndipo muamala hufanyika. Wanachama wote huweza kuona salio la kwenye mfuko na michango yao. Na huona nani kalipwa nini (hili sina hakika nalo kwa sasa). Mambo hayo yote hufanyika kupitia USSD ya simu za kiganjani -- kwa hiyo hata mwenye kitochi huweza kutumia.

Mambo ya kijumbe kukimbia na hela hakuna tena. Masharti yote ya kikundi yanaweza kuwekwa kwenye akaunti ya M-KOBA, kwa hiyo adhabu za kuchelewa, mambo ya hisa kwenye VICOBA, nk. yanaweza kufanyika kupitia simu-tochi ya kiganjani.

TPB na Vodacom Tanzania IMHO wamejizolea pointi nyingi sana kwa jambo hili la M-KOBA.
Jambo jema, ila mimi nionapo mdudu anaitwa voda huwa sikanyagi kabisa anakugeuza miguu juu dakika yoyote
 
Naomba msaada waungwana:
Mimi ni Mwenyekiti wa kikundi kipya tulichosajili M-Koba. Nahitaji kuwajua wanachama waliojiunga (waliokubali mwaliko wa kijiunga) kati ya wanachama wengi niliowaunga. Nikiingia kwenye Menyu ya WANACHAMA inaonesha Wanachama hai ni 10 na kuna majina 3 ya viongozi. Hao wanachama 7 wa kawaida haioneshi majina yao? Nayapata wapi?
 
Ikitokea mwenyekiti au mweka hazina amefariki je nani mwingine anauwezo Wa kuanzisha muamala au kutoa pesa?.
 
Back
Top Bottom