Pongezi Rais Magufuli na Awamu Yake ya Tano, Wafanya Maajabu Vita Dhidi ya Umasikini, Tanzania Yaongoza Dunia Kupunguza Umasikini Uliotopea-WB.

Mimi nafikiri ni bora ripoti ingesema "Umaskini umepungua kwa Paskali Mayalla na wanufaika wa system, kwani sisi waTz bado tunao umaskini.
Kiukweli kama hajawahi kuizunguka Tanzania haswa kule deep interiors huwezi kuujua umasikini uliotopea. Mimi mwenyewe niliushuhudia baada ya kupata tender ya TASAF kuzunguka nchi nzima kuripoti kazi ya uhaulishaji fedha kwa kaya masikini.
Katika kundi la wenye umasikini uliotopea, kipimo cha kwanza ni kuishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku. Kwenye kundi hilo, kiukweli mimi ni tajiri mkubwa. Ile kumiliki tuu smart phone ni kipimo tosha wewe sio mtu wa kundi hili.
P
 
Ndi maana nikasema wanufaika wa system, nyie mnakula hizo hela za Tasaf bila jasho, ni lazimu muwe wapiga filimbi wa serikali, Eti umasikini umepunguzwa
 
Pascal Mayalla , umeona eh! uliuliza swali la nguvu, ila siku hizi umekengeuka!
 
Ndi maana nikasema wanufaika wa system, nyie mnakula hizo hela za Tasaf bila jasho, ni lazimu muwe wapiga filimbi wa serikali, Eti umasikini umepunguzwa
Aliyesema Tanzania tunaongoza duniani katika kupunguza umasikini sio mimi wala sio Magufuli, ni Bank ya Dunia, na hawa taarifa zao ni data oriented, numbers don't lie. Sio bla bla ni ripoti ya utafiti wa kina uliofanywa na watafiti wa ukweli.
P
 

Mambo mengi anayofanya Magu bado hayajaenda kwa mtu wa kawaida na hakuna mradi mkubwa hata mmoja umekamilika. Hivyo jitihada zake zitaonekana mbele baada ya watu kuanza kutumia umeme nafuu, treni kwa mizigo, maji safi, kutibiwa kirahisi na ongezeko la elimu. Hivyo credit kwa sasa na kwa Maraisi wa nyuma
 
Kwa hili naona Mayalla ameweka pamba masikioni yaani hasikii la mtu. Na cha ajabu anakuja na mifano ya ajabu ajabu kweli. Cha kufurahisha ana amini kuwa karibu jeshi zima lililo changia hapa ni vilaza wanashindwa kuelewa kitu kidogo kama hicho. Kwa mwandishi wa habari nilitegemea angejiuliza tena na kuvuta pumzi lakini yeye hilo si hoja. Sasa naamini mapenzi yame mpofua.
Somo kwa wana JF mapenzi yanayopitiliza hupofua huu ni mfano hai na pia chuki inayopitiliza hupofua.
 
Vipaumbele na malengo kwa wakati huo (2000-2011) vilikuwa tofauti sana na wakati tulionao. Wakati huo, lengo lilikuwa kupunguza umaskini wa kipato kwa kaya maskini na leo hii malengo ni upatikanaji wa huduma mbalimbali za jamii bila kujali vipato vyao. Sasa hivi tukaamua kukusanya data kwa sample space ile ile, kwa vigezo vya kupunguza umaskini wa kipato, ripoti inaweza kutupa matokeo tofauti sana. Hivyo sifa hizo haziakisi uhalisia tulionao sasa.
 
Mkuu Masiya, kiukweli tuna vilaza wengi kuliko tunavyojidhania. Kwenye Economics data kati ya World Bank na sisi humu jf, who would be right kuhusu economic dataz?.

Nimeweka ripoti humu na kuweka ile chart, watu hamsomi the report, what does it say kuhusu Tanzania bali mnasoma tuu chart na kuishia kukomaa na data collection period.

Kati ya hawa World Bank walio collect data za 2000-2015 na kuja kutoa report 2019, na watu humu wanaosoma report ya 2019 kuilazimisha iwe ya mwaka wa data collection, nani mjinga?.

Nasisitiza kama hujui reason behind data za 2000-2015 kuja kutolewa report 2019, please don't argue.
Ushindi wowote unaotolewa kwa nchi yoyote, mwaka wa ushindi huo unapotangazwa pongezi zinakwenda kwa serikali iliyopo Madarakani wakati ushindi ulipotangazwa.
Hivyo Tanzania ndio nchi iliyoongoza duniani kwa kupunguza umasikini uliotopea kwa mujibu wa taarifa ya Benki ya Dunia ya mwaka huu 2019.
Pongezi kwa rais Magufuli wa Tanzania, na serikali yake.
P
 
maendeleo kwa mtanzania mmoja mmoja uchagizwa na juhudi za serikali katika kuimarisha na kuboresha miundombinu ya mawasiliano na usafiri, huduma mbalimbali kama maji, umeme na afya na awamu hii imejitahidi kiasi chake. huenda ripoti ijayo ikawa nzuri au mbaya



Hasara Umfika Mwenye Mabezo
 
Sijajua unatumia principal ipi Ku reason yaani data zikusanywe 2000 -2011 then to be published 2019 , halafu unasema hayo matokeo ni ya 2019 na sio 2000-2011? Yaani kwa lugha nyingine unamaanisha gesi inayo zalishwa mtwara na kusafilishwa mpka dar es salaam via pipe line, halafu uaminishe watu hii gesi inachimbwa dar na sio mtwara. Naomba uniambie unatumia ubongo gani ku-reason, na kupost katka jukwaa la ma elites kama hili .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu P. mapenzi yakizidi hupofusha.
 

You are wrong my bro!! Pongezi ziende kwa wale waliokuwa hicho kipindi. Mkuu unapotosha kwa makusudi. Taifa linawategemea wasomi kama ninyi, ila mnatuangusha, hata habari mnazotoa ni za kupotosha badala ya ukweli. Ni kwa nini usingetafuta ripoti currently ili ku-validate unachosema mkuu?!
 
Mkuu Masiya, Ripoti hii ni Ripoti ya 2019!. Jambo lolote jema au baya, siku linapotangazwa, pongezi au lawama zinakwenda kwa utawala uliopo madarakani kipindi ripoti inatolewa.

Mfano sisi tumepata uhuru mwaka 1961. Tanzania ni mwanachama wa EAC nyenye nchi 5. Ukifanywa Research ya Nchi za EAC zilizoongoza kwa hukumu ya kunyonga ndani ya miaka 50, Nyerere alinyonga watu wawili, Mwamwindi na yule mhindi aliyemua mkewe ili alipwe bima. Mwinyi alinyonga kadhaa idadi haikutangazwa, Mkapa hakunyonga, Kikwete hakunyonga, Magufuli hakunyonga na wala hatanyonga. Lakini kutokana na walionyongwa kipindi cha Mwinyi, ripoti ikitoka mwaka huu 2019, na kuonyesha Tanzania ndio nchi iliyoongoza Afrika Mashariki kwa kunyonga ndani ya kipindi cha miaka 50 iliyopita, ni nani atalaumiwa?. Ni rais wa sasa wa Tanzania, hata kama katika kipindi chake hajanyonga hata mtu mmoja!. Unadhani Magufuli atasoma ripoti na kusema msinilaumu mimi, mlaumuni Mwinyi ndiye aliyenyonga, mimi sijanyonga!.

Ripoti ni ya mwaka huu inaonyesha Tanzania ndio inaongoza dunia kwa kupunguza umasikini, maadam ripoti ni ya mwaka huu, then pongezi kwa ushindi huu ni kwa serikali iliyopo madarakani kwa sasa.
Hongera Magufuli.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…