posa yetu imekataliwa

neyl

Senior Member
Joined
Nov 23, 2011
Posts
127
Reaction score
19
habari, mimi ni kaka yangu ambae ni pacha yangu, yeye alitokea kumpenda kabinti chetu cha kazi ana miaka 2O elimu yake ni darasa la 7, baada ya kuwa na uhusiano wa siri kwa miaka miwili osidai akaamua kutangaza nia wazee wakatuma mshenga mpaka tanga kwa binti kupeleka barua afta cku mbili tukarudishiwa majibu kuwa hawataki binti yao aolewe kwetu kisa muoaji ni mtoto wa bosi na bint yao ni mfanyakazi et tutamdharau, pia sisi ni wamasai wao ni wabondei... iv jaman bado kuna ukabila tz mpaka leo?
 
  • ukabila upo, na culture zipo zinazuia hayo mambo. labda hofu yao ni kwamba binti yao atadharaurika, wanadhani anaolewa na familia nzima?
 
  • ukabila upo, na culture zipo zinazuia hayo mambo. labda hofu yao ni kwamba binti yao atadharaurika, wanadhani anaolewa na familia nzima?

atadharaurika = atadharaulika
 
ukwel hilo jambo linaniumiza simply bkoz sisi ni wamasai
 
Unajua mambo haya mlikosea mwanzo, kwa hiyo mnatakiwa mfanye vizuri na kwa utaratibu.
1. Wanatakiwa watu wazima wafunge safari mpaka huko Tanga na mkaongee nao ana kwa ana, na hilo watajua mmewaheshimu.
2. Inawezekana kunamaneno furani wanayasikia kuhusu familia yenu, yanayowafanya waone binti yao atadharauliwa hawawezi kusema hivi, hivi bila sababu. Kwa hiyo kitendo cha kwenda Tanga na kuongea nao itasaidia sana kujisafisha.
 
Pole mwaya, mtoto wa kitanga kakupagawishi mpaka basi Loh! Huambiwi wala husiki kwa mtoto wa ki Tanga... Ebu lilia Hali kwa mama mkwe huenda akakuelewa akaongea na baba mkwe anzaa pole pole usikurupuke.....
 
Hakuna cha mtoto wa bosi hapo, ni ukabila 2, unajua mila na desturi za kabila lenu bado hazijazaeleweka kwa wengi, wanajua mabaya mengi zaidi ya mazuri, mf utumikishwaji wa wanawake, kukosa maamuzi ndani ya familia nk .
 
Pole mwaya, mtoto wa kitanga kakupagawishi mpaka basi Loh! Huambiwi wala husiki kwa mtoto wa ki Tanga... Ebu lilia Hali kwa mama mkwe huenda akakuelewa akaongea na baba mkwe anzaa pole pole usikurupuke.....

arabian huyo ni mchumba wa kaka angu cyo wangu me ni msichana
 
Braza amedata na mtoto wa kitanga eeh!!! Komaeni.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…