KERO Precision Air mnatukosea sana Abiria, tangu Saa 12 Asubuhi Dar-Arusha tumeshindwa kuondoka kwa wakati na hamtoi maelezo

KERO Precision Air mnatukosea sana Abiria, tangu Saa 12 Asubuhi Dar-Arusha tumeshindwa kuondoka kwa wakati na hamtoi maelezo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
Precision Air wawajibike kwa kuwachelewesha abiria 'airport' bila maelezo yanayoeleweka, "tumekaa zaidi ya masaa matatu"

Abiria ambao tulikuwa na tiketi za kusafiri na ndege ya Precision Air kutoka Dar es Salaam - Arusha, Oktoba 14, 2024, Saa 12 Asubuhi tumeshindwa kuondoka kwa wakati na wahusika hawatoi maelezo yoyote kwetu yanayoeleweka kuhusu changamoto hiyo.

Abiria tumekaa tu hatuelewi nini kinaendelea, wengine tulikuwa tunawahi kwenye majukumu, lakini kibaya zaidi ambacho sio jambo rafiki kwa Kampuni kama hiyo ni kwamba wahusika hawakutueleza kwa wakati kama kuna changamoto zaidi ya saa tatu.

Baadaye wanaanza kutufaulisha bila utaratibu wowote na abiria wengine wamepandishwa ndege zisizoendana na hadhi ya tiketi zao, lakini cha kusikitisha zaidi ndege ambazo wengine tumepandishwa zinapita route tofauti mpaka kufika Arusha.

Kwa kweli jambo hili ni kero siwezi kulikalia kimya, naamini zipo mamlaka ambazo zinatetea na kulinda haki za abiria kama ilivyo kwao ukichelewa kidogo huna chako lakini wao wanaenda kinyume na makubaliano kupitia tiketi hata kutoa maelezo yanayoeleweka wanashindwa, sijui kama hata kumekuwepo na uwajibikaji kwa mamlaka kuwachukulia hatua kampuni zenye changamoto hizo.

Wito wangu kwa mamlaka naomba wafuatilie kwa ukaribu kero hiyo, inapobainika uzembe kampuni husika ziwajibike kama abiria anavyowajibika inapotokea changamoto ambayo ameisababisha yeye hususani kuchelewa, tukikalia kimya suala hili tunakuza na kubariki uzembe.
 
Precision Air wawajibike kwa kuwachelewesha abiria 'airport' bila maelezo yanayoeleweka, "tumekaa zaidi ya masaa matatu"

Abiria ambao tulikuwa na tiketi za kusafiri na ndege ya Precision Air kutoka Dar es Salaam-Arusha leo October 14, 2024 saa 12 asubuhi tumeshindwa kuondoka kwa wakati na wahusika hawatoi maelezo yoyote kwetu yanayoeleweka kuhusu changamoto hiyo.

Abiria tumekaa tu hatuelewi nini kinaebdelea, wengine tulikuwa tunawai kwenye majukumu, lakini kibaya zaidi ambacho sio jambo rafiki kwa Kampuni kama hiyo ni kwamba wahusika hawakutueleza kwa wakati kama kuna changamoto zaidi ya masaa matatu.

Baadae wanaanza kutufaulisha bila utaratibu wowote na abaria wengine wamepandishwa ndege zisizoendana na hadhi ya tiketi zao, lakini cha kusikitisha zaidi ndege ambazo wengine tumepandishwa zinapita root tofauti mpaka kufika Arusha.

Kwa kweli jambo hili ni kero siwezi kulikalia kimya, naamini zipo mamlaka ambazo zinatetea na kulinda haki za abiria kama ilivyo kwao ukichelewa kidogo huna chako lakini wao wanaenda kinyume na makubaliano kupitia tiketi hata kutoa maelezo yanayoeleweka wanashindwa, sijui kama hata kumekuwepo na uwajibikaji kwa mamlaka kuwachukulia hatua kampuni zenye changamoto hizo.

Wito wangu kwa mamlaka naomba wafuatilie kwa ukaribu kero hiyo, inapobainika uzembe kampuni husika ziwajibike kama abiria anavyowajibika inapotokea changamoto ambayo ameisababisha yeye hususani kuchelewa, tukikalia kimya suala hili tunakuza na kubariki uzembe.
 
Pole Mliogwa, wameshawahi kuninyoosha.. Safari ya saa moja asubuhi ikapelekwa saa nne asubuhi.. kuulizwa kwanini msingepiga simu ili na sisi abiria tu-reschedule muda wa kufika airport wakadai walituma email nane usiku.

Kuangalia email wanayosema hamna lakini pia msafiri anaanzaje kupekua email alfajiri badala ya kuwaza kujiandaa na safari! Ule mkoa haukuwa na bolt, nikachukua taxi kwa 50k kwenda mjini na kurudi airport kwa kitu ambacho wangenitaarifu mapema ningeendelea kuvuta shuka langu hotelini. Customer service dunia ya tatu bado sana hadi kwa private entities.
 
Ndio muache viherehere kwenda airport. Huo muda wa saa 3 uliokaa hapo Airport pamoja na waiting time ya saa 3 ungechukua boda ungekuta umeshafika mapema sana. Tumieni hata akili bandia kama vipi. 6 hours umekaa hapo unasubiri ndege?
 
Ungepanda Aboud
Precision Air wawajibike kwa kuwachelewesha abiria 'airport' bila maelezo yanayoeleweka, "tumekaa zaidi ya masaa matatu"

Abiria ambao tulikuwa na tiketi za kusafiri na ndege ya Precision Air kutoka Dar es Salaam-Arusha leo October 14, 2024 saa 12 asubuhi tumeshindwa kuondoka kwa wakati na wahusika hawatoi maelezo yoyote kwetu yanayoeleweka kuhusu changamoto hiyo.

Abiria tumekaa tu hatuelewi nini kinaebdelea, wengine tulikuwa tunawai kwenye majukumu, lakini kibaya zaidi ambacho sio jambo rafiki kwa Kampuni kama hiyo ni kwamba wahusika hawakutueleza kwa wakati kama kuna changamoto zaidi ya masaa matatu.

Baadae wanaanza kutufaulisha bila utaratibu wowote na abaria wengine wamepandishwa ndege zisizoendana na hadhi ya tiketi zao, lakini cha kusikitisha zaidi ndege ambazo wengine tumepandishwa zinapita root tofauti mpaka kufika Arusha.

Kwa kweli jambo hili ni kero siwezi kulikalia kimya, naamini zipo mamlaka ambazo zinatetea na kulinda haki za abiria kama ilivyo kwao ukichelewa kidogo huna chako lakini wao wanaenda kinyume na makubaliano kupitia tiketi hata kutoa maelezo yanayoeleweka wanashindwa, sijui kama hata kumekuwepo na uwajibikaji kwa mamlaka kuwachukulia hatua kampuni zenye changamoto hizo.

Wito wangu kwa mamlaka naomba wafuatilie kwa ukaribu kero hiyo, inapobainika uzembe kampuni husika ziwajibike kama abiria anavyowajibika inapotokea changamoto ambayo ameisababisha yeye hususani kuchelewa, tukikalia kimya suala hili tunakuza na kubariki uzembe.
Ungepanda Aboud, Esther au Kilimanjaro bus saa nne usiku Jana ungekuwa Arusha saa kumi na mbili asubuhi Leo tena kwa bei chini maradufu ya ndege.
Kupanga ni kuchagua.
 
Back
Top Bottom